MKUTANO WA KAMPENI ZA VYAMA VINAVYOUNDA UMOJA WA KATIBA UKAWA VIKINDU GETINI LEO
NEC YATAHADHALISHWA JUU YA UCHAGUZI MKUU 2015

Yamesemwa hayo na viongozi wa makanisa ya katoliki akiwemo Askofu Anthony Banzi, ambaye ni askofu wa Katoliki jimbo la Tanga pamoja na Askofu Thomas Tarimo ambaye ni askofu Kanisa la Pentekoste jijini Tanga.
HARRISON MWAKYEMBE ALIA NA EDWARD LOWASSA JANA
UZINDUZI WA KAMPENI NA MAFUNZO YA CHAMA CHA ACT
SHULE ZAFUNGWA WAKIHOFIA KIPINDU PINDU DAR
Baadhi ya shule katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam zimelazimika kufungwa kwa mda wa wiki mbili
MOTO WASABABISHA VIFO VYA WATU 9 BUGURUNI JANA

Kwa niaba ya familia yangu nawapa Pole sana wafiwa wote na Mungu awape subra katika kipindi hiki kigumu. Wenye taarifa kamili tunaomba mtujuze.
WATU 109 WAMEPOTEZA MAISHA YAO KWA KUNYONGWA
Watu 109 wamepoteza maisha yao kwa mda miezi 8 tangu mwezi January 2015 kwenye ukanda wa nchi za Kiarabu. (Arabic State )
Watu hao wamekufa kwa kifo cha kunyongwa, eidha adharani au kwasili kutokana na ukubwa wa makosa yao, huku ikitajwa kuwa asilimia kubwa kati ya hao wengi ni wageni kutoka mataifa mbalimbali.
DEO FILIKUNJOMBE APITA BILA KUPIGWA.
Mgombea ubunge kupitia jimbo la Ludewa mkoani Njombe mhe.Deo Filikunjombe, amepita bila kupingwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
CHADEMA YAIBUA TUHUMA MPYA DHIDI YA NEC
NAPE ATAFSILIWA VIBAYA KWA MANENO YAKE JANA
WARIOBA: TANZANIA INAHITAJI KIONGOZI MWADILIFU
TUME YA TAIFA NEC YAWEKA HESHIMA YA KUJENGA TAIFA
MHE.JOSEPH JOHN POMBE MAGUFULI AREJESHA FOMU YAKE LEO
MGOMO BARIDI WA MADREVA NCHI NZIMA
Chama cha madreva wa mabasi yaendayo mikoani kimetangaza mgomo baridi kwa nchi nzima kusimamisha zoezi la kusafirisha abilia kwa siku zaidi ya tano 5 kwa madai wanaenda kuudhulia mafunzo ya usalama barabarani.
LOWASSA ATOA POLE KWA WANA CUF SOMA ZAIDI
Aidha, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe ameonya kuwa, hawatamvumilia yeyote atakayeonekana kutaka kukwamisha umoja wao unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD.
Lowassa aliwapa pole wanaCUF akisema endapo watatetereka, safari yao ya kuelekea Ikulu itakuwa ngumu.
Alitumia fursa hiyo kuwaomba wafuasi wa CUF kumsindikiza kwa wingi leo kwenda ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua fomu ya kuwania urais baadaye mwaka huu, huku akisisitiza ana imani ya kushinda.
Awali, mgombea mwenza wa Lowassa, Juma Duni Haji ambaye alijiunga Chadema hivi karibuni akitokea CUF alikokuwa Makamu wa Mwenyekiti wa Taifa, alisema endapo wanachama wa vyama vinavyounda Ukawa watakosea katika kupiga kura zao na kushindwa kuingia madarakani, basi watalazimika kusubiri miaka 50 ijayo ili kuingia Ikulu.
“Tusipoweza kuingia Ikulu sasa litakuwa kosa kubwa na itatulazimu kusubiri miaka 50 ijayo ili kuweza kuchukua madaraka. Vijana pekee ndio watakaoweza kuleta mabadiliko,” alisema Duni.
Lowassa alisema endapo Ukawa itashinda na kuchukua madaraka wataendesha nchi kwa utulivu na kubadilisha maisha ya Watanzania kwa kuwaondolea umasikini ambao umekuwa ukipigwa vita tangu mwaka 1962. Naye Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe alisema kiongozi ndani ya Ukawa ambaye atakuwa akipingana na malengo yao kutokana na kukosa fursa binafsi, mtu huyo hafai kuwa katika umoja huo.
Alisema pamoja na umoja huo kukumbwa na misukosuko, bado wamekuwa wamoja na kutetea hatua ya wao kumteua Lowassa ambaye wiki mbili zilizopita alikuwa CCM kwa sababu ni Mtanzania. Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alisema silaha pekee ya ushindi kwa Ukawa ni kuwa na umoja, ushirikiano na mshikamano na kuwa ana uhakika Lowassa atashinda, sambamba na yeye kwa upande wa Zanzibar.
ADAM KIMBISA AKANUSHA HABARI YA KUAMA CCM
Aliyasema hayo jana mjini hapa kutokana na kuwapo kwa taarifa amekihama chama hicho. Awali, jana kulikuwa na taarifa za Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole kuhamia Chadema, kama ilivyokuwa kwa Mgana Msindai, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida aliyetangulia Chadema wiki iliyopita baada ya kushindwa kura za maoni ndani ya CCM.

Katika kuthibitisha hayo, Kimbisa jana alikuwa akiendesha vikao vya Kamati ya Siasa ya Mkoa akiwa katika sare zake za chama. Taarifa hizo zimekuja huku Kimbisa akiwa na habari nyingine katika gazeti hili (ukurasa wa 21) akielezea kushangazwa na wanaokihama chama baada ya kushindwa katika michakato ya kuwania uongozi, huku akisema kamwe yeye hawezi kufanya hivyo.
“Mwaka 2010 niligombea ubunge Jimbo la Dodoma Mjini nikahesabu kura zangu mwenyewe nyumbani nikajiona nimeshinda nikalala, asubuhi nilipoamka kumbe wagombea wenzangu wakaunganisha matokeo yao mgombea mmoja akaonekana ameshinda, lakini bado sikuhama na hadi leo nina damu ya kijani.
“Mtu akihangaika kuondoka CCM baada ya kushindwa tutamfuata hukohuko na tutampiga kwa kura tu,” alisisitiza Kimbisa.
JOTO LA KUWAPATA WAGOMBEA UBUNGE CCM KUPANDA
Mbali na hayo, viongozi wa ngazi ya wilaya na mikoa wanaodaiwa kuwabeba kinyume na utaratibu nao wapo hatarini kuvuliwa nyadhifa zao.
Taarifa kutoka ndani ya CCM ilisema kuwa kikao cha Sekretarieti kilichokutana mjini hapa, kilijadili baadhi ya taarifa na rufaa za wagombea, huku wengine wakiwalalamikia wenzao pamoja na viongozi kwa kucheza rafu wakati wa uchaguzi wa kura za maoni.
Miongoni mwa jambo ambalo limekuwa likizua mjadala, ni hatua ya baadhi ya wabunge kupata kura nyingi katika maeneo yao kinyume na idadi halisi ya wanachama wa CCM kwenye jimbo husika.Moja kati ya majimbo ambayo wagombea walilalamikia hatua hiyo, ni Jimbo la Iramba ambapo Juma Kilimbah ambaye alikuwa ni moja ya wagombea, alisema pamoja na kura kupigwa bado kura alizopata mgombea mwenzao, Mwigulu Nchemba ni tofauti na idadi ya wapiga kura.
Alidai wakati wa mchakato huo, baadhi ya viongozi wa CCM akiwemo msimamizi wa uchaguzi, walikuwa wakigawa kadi kinyume na utaratibu kwa lengo la kumwezesha Mwigulu kushinda.
MWENYEKITI NA KATIBU WA CCM WAJIUNGA NA CHADEMA
Ole Nangole na Joseph walifikia uamuzi huo jijini hapa jana na kusema kwa nyakati tofauti wamelazimika kuchukua uamuzi huo kwa kuwa utaratibu wa kumpata mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ulikiukwa.
Kwa mujibu wa wana CCM hao, wakati wa mchakato huo baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho walikuwa na wagombea wao mifukoni waliotaka wagombee nafasi hiyo.
Ole Nangole aliyejiondoa CCM akiwa kwenye kipindi cha awamu ya pili cha uenyekiti wake, alisema alijiunga CCM mwaka 1977 ambapo alifanikiwa kushika nyadhifa mbalimbali zikiwamo mwenyekiti wa CCM wilaya kwa miaka kumi.
“Ndugu zangu waandishi wa habari nimewaita leo kuwaambia jambo moja kwamba ninahama CCM kuanzia sasa. Najiuzulu nafasi yangu ya mwenyekiti niliyoitumikia kwa miaka saba na ninajiunga na Chadema kuanzia sasa.
“Nashindwa kuwa na moyo wa chuma wa kuendelea kuwa ndani ya CCM kwa sababu CCM niliyoifahamu tangu enzi za TANU siyo hii ya sasa.
“Kuondoka kwangu kumechangiwa na kikundi cha viongozi wachache kuiongoza CCM kwa mabavu, nguvu na kwa kutumia fedha walizokwapua serikalini.“Miaka yote tangu nilipojiunga CCM mwaka 1977, sikuwahi kukiona chama hiki kikiendesha mambo yake bila kufuata kanuni na taratibu za vikao kama kilivyofanya wakati wa vikao vya kupitisha mgombea urais mjini Dodoma hivi karibuni.
“Mkutano mkuu wa CCM uliongozwa kwa kukiuka haki na misingi kwa wanachama kwani hata nyinyi mtakumbuka kulikuwa na mchakato wa urais na wagombea 40 walijitokeza akiwamo Edward Lowassa.
“Kwa mapenzi yake Lowassa alivyokitumikia chama na Taifa, wananchi tuliamini mchakato ule kama jina lake lisingekatwa angekuwa mmoja wa wagombea ambao wangefika mbali ndani ya chama.
“Lakini jina lake lilikatwa bila sababu japokuwa sababu tulizijua tangu alipotoka kwenye uwaziri mkuu kwa vile kuliendelea kusambazwa maneno na hujuma za kisiasa dhidi yake kupitia kwa viongozi wa chama na Serikali wakiwamo vijana wadogo waliopewa fedha na madaraka ili wamchafue,” alisema Ole Nangole.
Kwa upande wake, Joseph alimnyooshea kidole Katibu wa CCM, Abdulrahman Kinana na kumtaka achunge ulimi wake pindi anapowaita Watanzania makapi ndani ya nchi yao.
Joseph ambaye ni Diwani wa Kata ya Monduli Mjini aliyemaliza muda wake na kupita bila kupingwa ndani ya CCM, alisema hakuna Mtanzania aliye makapi kwani wote wana haki ya kidemokrasia ya kuhama vyama kwa jinsi watakavyoona inafaa.
“Watasema mengi na tumeondoka watatuita makapi. Naomba niwaambie, sisi siyo makapi, wakitaka tuzungumze suala la makapi hao wanaosema hivyo wao ndio makapi halisi.
“Sisi Watanzania si makapi kwani tukichambuana kwa suala la makapi na kuangalia wewe umetokea wapi, tutakwenda kusiko. Kwanza aliyesema hiyo kauli yeye ni Msomali. Hivyo tukisema nani ni makapi yeye ndiye makapi halisi anayeishi Tanzania kwani asili yake ni Somalia,” alisema Joseph.
Joseph alitoa kauli hiyo zikiwa ni siku chache baada ya Kinana kunukuliwa na vyombo vya habari akisema wanachama wa CCM wanaohamia Chadema ni makapi.
LIPUMBA ASEMA CCM INA WAGOMBEA URAIS WAWILI
KAMA HAUNA KAZI MAARUMU USIENDE MJINI, SOMA HII
SASA THIERRY HENRY AJIBU SWALI LA WANA ARSENAL



WAFANYAKAZI WA TAZARA WALIPWE MISHAHARA YAO
BUNDUKI 16 KATI YA 21 ZA STAKISHARI ZIMEKAMATWA
MKE WA DK.WILLLIBROAD SLAA AKANUSHA YALIYOSEMWA
UVCCM ZANZIBAR WASEMA CCM ITASHIKA DOLA OCTOBER
NANI RAIS, MBUNGE, DIWANI MWAKA HUU OCTOBER 25?
HABARI KUU KUTOKA MAGAZETINI IKIWA NI AUGUST 7
Prof. Ibrahim Lipumba ango’ka hali tete UKAWA, ajiuluzu uwenyekiti wa miaka 16 CUF akimpinga Edward Lowassa adai UKAWA washindwa kuenzi uadilifu na uzalendo.
CCM kupitisha wagombea Ubunge leo…Edward Lowassa aipasua vipande UKAWA…NEC yaonya kampeni nyumba za ibada…Siri yafichuka CUF watoa taamko…na mke wa Dk. Wilbroad Slaa afunguka.

UKAWA wapata mtikisiko mkubwa baada ya Prof. Ibrahim Lipumba kujiuzulu uwenyekiti wa chama cha CUF na kuamua kubaki kuwa mwanachama wa kawaida wa Chama hicho…idadi ya Wabunge 51 waanguka kura za maoni ndani ya vyama vyao.
Zaidi ya majambazi 10 waliohusika na tukio la Sitakishari wakamatwa na Polisi…Wamachinga wanaendelea na ujenzi wa vibanda Jangwani pamoja na Serekali kusisitiza kuwa wanapaswa kuhama eneo hilo.










