Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

IDADI YA WAHANDISI NCHINI TANZANIA WAFIKIA 15,364

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Idadi ya wahandisi waliosajiliwa nchini imeongezeka kutoka 6,868 na kufikia 15,364 katika kipindi cha miaka 10. Kati ya wahandisi hao 15,364, wahandisi wazalendo ni 13,901 na wa kigeni 1,463.Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Steven Mrope, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi.

Mhadisi Mrope alisema katika kipindi hicho, jumla ya kampuni za ushauri wa kihandisi 279 zilisajiliwa na kati ya hizo, 201 ni ya kizalendo na 78 za kigeni.
Aidha, alisema idadi ya wahandisi washauri ni 459 ambapo kati yao, 356 ni wazalendo na 103 wageni.

“Bodi imeendelea kutembelea na kukagua hali ya uhandisi katika halmashauri zote Tanzania bara, ukaguzi huo umewezesha halmashauri nyingi kutambua umuhimu wa kuajiri wahandisi na kuwatumia katika miradi ya ujenzi,” alisema Mrope.


Alisema hiyo pia imewezesha idadi ya wahandisi katika halmashauri kuongezeka kutoka 129 mwaka 2003 hadi kufikia 508 mwaka 2015.
“Ingawa idadi hiyo ya wahandisi bado ni ndogo, lakini ni dhahiri ubora wa kazi katika halmashauri umeongezeka,” alisema.

Aliongeza kuwa Bodi imefanikiwa pia kuongeza  idadi ya wahandisi wataalam wanawake kutoka 20 waliosajiliwa mwaka 2011/12 hadi 80 waliosajiliwa mwaka 2013/14 mpaka kufikia 176 kwa sasa.

Aliongeza kuwa baada ya mabadiliko ya Sheria, Bodi imeanza kusajili mafundi sanifu ambao ndiyo wasaidizi wakuu wa wahandisi na mpaka sasa mafundi sanifu 157 wamesajiliwa. Mhandisi Mrope alisema moja ya majukumu ya Bodi ni uendelezaji wa taaluma ya kihandisi ili kufanya wahandisi waende sambamba na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top