MINI SHOP CHETA
UNAWAZO LA KUANZISHA BIASHARA YAKO BINAFSI?
Hakuna mwanaume mkorofi kwa mwanamke mnyenyekevu, bofya hapa ujifunze kitu
YALIYONIKUTA SITAKI YAKUKUTE WEWE, EBU JIFUNZE KUPITIA HAPA
Kwa wale watu kwa ujumla wanaoingia kwenye mahusiano hasa ya kudumu, yanaweza kuwa ndoa au ya mwelekeo wa ndoa ni vyema tukawa tumejiandaa kwa lolote litakalotokea na kulichukulia hata kama ni nzito namna gani.
Kumbuka hakuna kitu kisichokuwa na mapito au changamoto kosa kubwa tunalolifanya pale tunapoingia kwenye mahusiano hayo ni pale tunapofikiri kuwa mwenzi wako huyo ni malaika na hawezi kukosea kwa namna yoyote ila wewe ndio binadamu ukikosea usamehewe na muendelee kuvumiliana ila wewe uvumilivu huna.
Pale mnapompenda mtu jua kuwa na yeye anamadhaifu yake ambayo unatakiwa kumvumilia hata kama ni ya namna gani, hata iwe ni usaliti wa ndoa ni lazima mvumilie na sio kumuacha au kumkashifu.Utakuta mtu anasema kwa jambo hili siwezi vumilia na anasahau hata yeye anavumiliwa tu.
Ni lazima tujue kuwa huwa tunakutana na watu wanaotufaa kwa yale madhaifu yetu na sio watu wakamilifu wa madhaifu yetu, yaani mfano unaweza kukuta mwanamke hawezi labda kufua nguo vizuri na wewe swala la kufua nguo sio shida sana.
So unachotakiwa kufanya sio kudharirisha na kuwa na akili mgando ya mfumo dume hapo ni kuweka mfanya kazi au fua na sio kudharirishwa kwani mke sio mfanyakazi na kuna tofauti ya majukumu ya mfanyakazi na mke pia na heshima zao zinatofautiana, au mwanaume ni bwana mipango mzuri lakini utekelezaji wako ni ziro nawe unaweza kusimamia. Hivyo we simamia na usiwe na dharau, kwani sifa ya kwanza ya mwanamke ni utii.
KWANINI NDOA HAZIDUMU?? MAJIBU YOTE YAKO HAPA
Kwanini ndoa hazidumu?? Majibu yako hapa
Ndoa zina haribiwa na vitu vingi sana ila kwa siku ya leo tutazungumzia juu ya kitu kinachoitwa "USHIRIKINA" kwenye ndoa zetu za kiafrika.
Ushirikina ndani ya ndoa pia ni jambo ambalo kwa kiasi kikubwa sana huchangia ndoa nyingi sana kuvunjika, na kuleta madhara makubwa kwa wale waliofanyiwa ushirikina huo.
Ushirikina huo hufanyiana wao wanandoa wenyewe kwa wenyewe au hufanywa dhidi yao (yaani hufanyiwa na watu baki).
Tukianza na wanandoa wenyewe kwa wenyewe kufanyiana ushirikina, na itatubidi tuangalie pande zote mbili ili kuweka mambo sawa, upande wa wanaume, pia na upande wa wanawake.
Tuanze na upande wa wanawake: Wanawake wengi wamekuwa wakienda mbio kufanya ushirikina wakiwa ndani ya ndoa au wakiwa wameachika, na wakiwa ndani ya ndoa zao huwa wanafanya hivyo kwa malengo mengi miongoni mwa malengo hayo ni pamoja na;
1. Kuwafanya waume wao wazidishe mapenzi zaidi kwao. Kwa dhana zao mbovu kuwa mapenzi huzidishwa kwa kupitia uchawi, ndugu zangu akina mama na akina dada, mapenzi ya kweli na ya dhati hayazidishwi kwa nguvu za giza (uchawi), wala limbwata, ilo mlitambue.
Sio mapenzi ya dhati kwa sababu kinachofanywa ni kuwa mume huyo anavishwa jini ambalo huumfanya imma, apende, achukie, aache, awe mtiifu na mambo mengine kama hayo.
Ila utambue kuwa mapenzi ya kweli huzidishwa kwa kuhurumiana, kuenziana na kustahamiliana katika shida, raha na kusameheana kwa kosa kubwa au dogo na hayo yote ili yapatikane kwenye ndoa yenu lazima mume na mke wote kwa pamoja muwe ni wachamungu.
2. Kuwafanya waume zao kuwachukia wake wengine kama ni ndoa ya wake zaidi ya mmoja, ili aachike au waachike wengine abakie mwenyewe, na hii kutokana na wivu wa kipumbavu, uchoyo, roho mbaya na hasadi walizonazo wenye mioyo yao.
Picha kutoka maktaba
3. Kufanya mume asiwe na maamuzi yeyote katika ndoa yake, badala yake abaki kuwa mtekelezaji tu wa chochote kile atakachoamrishwa na mkewe, kiwe cha halali au cha haramu, kiwe kinawepesi au kinauzito bwana huyo atafanya kwa sababu sio yeye bali anakuwa chini ya nguvu za jini alilovishwa.
4. Anapokuwa mwanamke ameachika lengo kubwa la kufanya ushirikina ni kumfanya mume huyo amrejee, au kumtia matatizo huyo mwanaume ili asiweze kuoa tena, au kila akioa mke mwingine asiweze kudumu naye, au kumfanyia ushirikina wenye kumpunguza nguvu za kiume, au kumuathiri kiuchumi, au kumfanya apate wazimu, au hata kumuua, au kumsababishia matatizo mengi.
Sasa tuangalie ushirikina kwa upande wa wanaume; pia nako huku tunakuta kuwa wanaume nao wanafanya ushirikina katika ndoa zao wakiwafanyia wake wao kwa malengo kama yafuatayo hapo chini.
1. Kumdhibiti mke muovu ili awe mwema. Jambo ambalo halina ukweli wowote kwa sababu njia ya kumuelekeza na kumsaidia mtu si kwa kutumia ushirikina, bali ni kurekebisha ufahamu wake kwa kutumia maneno yenye nguvu ya Mungu.
(Hakuna kitabu cha dini kinacho mruhusu mwanadamu kutenda dhambi au maovu).
2. Vile vile wanaume hufanya ushirikina kwa lengo la kuwafanya wake wawe watiifu zaidi na waogope kuzini nje ya ndoa zao, hufanya vile wakimaanisha kwamba wake zao wakizini tu nje ya ndoa basi waume hao wajue, au wakizini nje ya ndoa zao wagandane na hao waliozini nao, watu wa pwani wanaita/sema “tego”.
3. Pia kama watakuwa wamewaacha hao wake zao hufanya ushirikina kwa lengo la kurudiana nao, au kumhusudu katika mambo mbalimbali kama kumtia maradhi kama vile; kutokwa damu nyingi sehemu za siri, kumfanya asizae, au asiolewe na mume mwingine nk.
Mara nyingi ushirikina kama huu hufanywa na wanaume hao hasa kama ukorofi wao ndio uliopelekea wake zao kudai talaka, au kuachishwa kinguvu, hali ya kuwa wao bado walikuwa wanawahitaji hao wake zao.
Ebu tuangalie ushirikina ambao unakuwa ni dhidi ya wanandoa; ushirikina ambao unakuwa ni dhidi ya wanandoa ni ule ushirikina wa watu wenye husuda wasiotaka kuona ndoa za watu zinadumu, na watu kuishi kwa raha na maelewano.
Na wakati mwingine watekelezaji wa ushirikina wa namna hii ni wanafamilia au wana ukoo kama Baba, Mama, Dada, Shangazi, Mjomba au watu wengine wa nje ya familia na ukoo huo.
Niwakati wako wa kujitafakari ukiwa kama mwana ndoa, je uko upande gani? Na kwa nini umeamua kuwa upande huo?
EVERYTHING IN MARRIAGE IS POSIBLE, GO HERE FOR MORE INFO
Nowadays incidences of heart break between couples is increasing probably because of long distance between couples, and cheating, also cheating is not being accepted for all parents in our families.
Money greedy, religious and race reasons, endless fights, loss of feelings, death of one you loved and so other things.
Those incidences have caused a lot of problems in our families community like confusion, suicide, poor performance in the offices, in the class, in the decision, also loss of focus in the life, quitting of job and etc.
Generally, heart breaking can't be prevented but complications coming from heart break can be prevented and someone can go back in his or her previous normal life as before. So in order you win in this progress please try to avoid the following in your marriage.
1. Delete your ex contact, this is main source of conflict in your marriage, keep on calling or texting his or her will make things worse especially if she or he doesn't want you anymore and probably you are replaced ready by someone else, so just keep quite and even if you have the number in your head don't write them any ware because silence is the best weapons.
2. Be busy with other things, go out with friends, visit places where you was never visited before, watch action movies, and avoid to listen love songs or movies by the time being because they will eat you and don't just stay alone thinking all day long.
3. Don't hide your feelings, tell your friends or other members of your families or relative and other people what happened to you and what will easy your pain and you will feel at least relaxed, but hiding things won't do any good to you.
4. Don't stop your tears, if you feel like crying please don't force your heart to stop what you support to do is cry it.
Remember this is not only what you should avoid in your marriage, there is so many things what you must be avoided for anyone who are in marriage, but for today I feel to let you know this four things. If you like Swahili news Go Here
PICHA IKIAMBATANA NA UJUMBE WA SIKU YA LEO INASEMA IVI
URAFIKI WA MASHAKA HUTOWEKA MARA SABABU HIYO IKITOWEKA
MAMA MKWE HATAKI KUNIONA, BOFYA HAPA KUJUA KISA NA MKASA
Ndugu zangu, Mimi nina tatizo na mama mkwe wangu kwa kifupi nimeishi na mtoto wake kwa miaka 15, sasa na tumepata watoto wawili lakini jambo la kushangaza ametoa kauli nzito kwangu akisema kuwa ataniua, kunifunga jela, au kuniroga.
Ugomvi wetu ni watoto wangu ambao niliondoka nyumbani kwenda Morogoro kutafuta maisha, mke wangu akabaki nyumbani kama miezi miwili akaja kunifuata.
Tumekaa kama miezi 6 akarudi nyumbani kuchukua watoto ambao aliwaacha kwa mama yake mzazi lakini mama akamnyima watoto na aliporudi tukajadiliana na kupata jibu kuwa niende.
Mimi nikaondoka, lakini nilikutana na matusi mazito. Kwa hekima sikumjibu chochote nikaaga na kuondoka.
Ikapita miaka minne bila kuulizana chochote! Jambo la kushangaza mwanzo wa mwezi wa 8 tulikuja wote kwa ajili ya kusalimia na kuomba watoto lakini katamka wazi mbele ya mke wangu kuwa hanipendi na hataki nikanyage kwake niwe na mwanae.
Mke wangu alijua utani kumbe mama yake alikuwa hatanii. Sasa mimi nataka kuondoka nimuache mke wangu yeye hataki na anataka kujiua.
NI VIBAYA HOUSE GIRL KUOLEWA NA BABA MWENYE NYUMBA? BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI
Ivi ni vibaya House girl kuolewa na baba mwenye nyumba?
Ndugu msomaji wa Mutalemwa Blog, karibu kwenye makala hii maalumu, nimeamua kuandika habari hii ili kujaribu kupunguza mifarakano kwenye familia zetu especially familia zenye wafanyakazi wa ndani wanaojulikana kama house girl.
Katika mada hii Mutalemwa Blog imekuwa ikikutana na maswali mengi sana ambayo mda mwingine yalikuwa yakituchanganya hata sisi wenyewe katika kuwajibu wahusika, maswali haya malanyingi yalikuwa yakiulizwa na akina mama.
Na kwa upande wa akina baba maswali yao sio mengi ukilinganisha na akina mama, sasa napenda nianze kwa kusema mambo yafuatayo ili wote twende sawa.
WAJIBU WA MWANAUME KATIKA FAMILIA: Mwanaume anawajibu wa kutimiza mahitaji yote ya msingi katika familia yake, moja ya majukumu hayo ni pamoja na kutoa pesa za matunzo ya familia yake kadri ipasavyo, kuonyesha upendo wa dhati kwa mama pamoja na watoto wake, na mambo mengineyo nk.
WAJIBU WA MWANAMKE KATIKA FAMILIA: Mwanamke ndiye mtendaji mkuu wa familia kwa upande wa nyumbani ukiachilia mbali ya kwamba baba ndiye kichwa cha familia, mwanamke anamajukumu mengi kwa upande wa nyumbani moja ya majukumu yake ni pamoja na kupika chakula cha familia, kufua nguo za mumewe pamoja na nguo za watoto, kuakikisha nyumba pamoja na eneo linaloizunguka nyumba ni safi, kuonyesha upendo wa dhati kwa mumewe pamoja na watoto wake, nk.
Picha kutoka maktaba
Ndugu msomaji wa makala hii, nadhani mpaka hapo tayari umeisha anza kupata mwanga kuhusu jibu la swali la makala yetu, sasa twende kuona wajibu wa mfanya kazi wa ndani kama house girl.
House girl wajibu wake ni kuakikisha anafanya usafi wa kuizunguka eneo la nyumba kwa nje na kufanya usafi huo kwa upande wa ndani kwa baadhi tu ya maeneo ya nyumba hiyo pamoja na kuwaogesha watoto, kufua nguo za watoto, na kufanya kazi ndogo ndogo za nyumbani.
House girl hatakiwi kufanya usafi chumbani kwa mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kufua au kupiga pasi nguo za mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kumuandalia chakula au chai mume wa mama mwenye nyumba, nk.
Sasa ukiona house girl anafanya kazo zote nilizosema kuwa hatakiwi kuzifanya pindi awapo nyumbani kwako, ukiwa kama mama mwenye akili timamu jua kabisa tayari umeamua kumuletea mumeo mke mdogo na pia usipige kelele wala kulaumu maana jitihada zote za kumuandaa mke mwenzio umezifanya wewe mwenyewe.
Ushauri wangu kwenu akina mama na akina dada nikwamba, hatukatai kuwa wafanyakazi wa ndani hawafai, ila jitaidi mfanyakazi wako awe na mipaka ya kazi, mwanaume anaamua kumuoa house girl kwa sababu yeye amechukua majukumu yote ya mama mwenye nyumba, sasa wewe mama usianze kumtupia maneno mtoto wa watu pamoja na mumeo maana yote hayo umeyataka wewe mwenyewe.
Kama umependa makala hii tafadhali Share na wenzio wajifunze kitu. Endelea kutembelea tovuti zetu zifuatazo kwa kubofya kwenye jina la tovuti husika.
1. (TAZAMA LINE) 2. (MIKOA YETU)
HUU NI UJUMBE MAALUMU KWA AKINA DADA, ILA NA AKINA KAKA MNAWEZA KUUPITIA
Mimi sina mengi sana ya kuongea zaidi ya kukutakia usomaji mzuri na utafakari mzuri baada ya kumaliza kusoma habari hii.
SIMU YA MKONONI UTENGENEZWAJI WAKE NI MATESO KWA BINADAMU, ZAIDI BOFYA HAPA
Upande mchafu wa simu yako ya mkononi. Wanaharakati wa haki za kibinadamu wanailaumu sekta ya utengezaji simu kwa kupuuzia ukiukaji wa haki za kibinadamu unaofanywa katika makampuni ya simu nchini China na kwenye machimbo ya madini nchini Congo.
Simu ya mkononi inaweza kuwa chombo kizuri cha mawasiliano lakini utengenezwaji wake una siri kubwa ya mateso ya kibinaadamu.
Yanayoendelea nyuma ya sekta hiyo ya kisasa na inayokua ni unyanyasaji wa wafanyakazi, au madini yaliyojaa matone ya damu kutoka maeneo yenye machafuko. Hayo ni kwa mujibu wa afisa wa shirika la SETEM linalojumuisha mashirika 10 yasiyo ya kiserikali yanayoendesha kampeni ya maonyesho mbadala yenye taswira ya kukuza maadili.
Ni makampuni machache tu miongoni mwa washiriki katika kongamano hilo la simu ulimwenguni yaani Mobile World Congress (MWC) ambayo yameonyesha simu zao za kisasa “The Fairphone 2” ambayo kampuni ya Uholanzi inajaribu kuitengeneza kwa kuzingatia maadili.
Kulingana na meneja wa utangamano na umma, Daria Koreniushkina, kufuata mikondo ambayo madini ya kuunda simu hufuata si rahisi.
Mkondo huo hujumuisha zaidi ya wahusika mia moja duniani, na kwa kila madini yanayotumika hupitia hatua zisizopungua tano. Hivyo ni changamoto kubwa kuhakikisha kila hatua ni salama. Zaidi soma kupitia habari hii kwa {KUBOFYA HAPA}
UNAJUA KWA NINI WAGANGA WANAWEZA KUWASAIDIA WATU KUWA MATAJIRI WAKATI WAO NI MASIKINI?? BOFYA HAPA KUJUA MBINU ZAO
Unajua Kwa Nini Waganga Wanaweza Kuwasaidia Watu Kuwa Matajiri Wakati Wao Ni Masikini? Soma Hapa Ili Uweze Kutumia Mbinu Hiyo.
Karibu msomaji kwenye mfululizo huu wa makala za uchawi na mafanikio. Kama tulivyoona wiki iliyopita ni kweli kwamba kuna watu ambao wanapata mafanikio makubwa kwa kutumia uchawi. Ila mafanikio yale hayaletwi na uchawi bali imani ya mtu husika.
Wiki hii tutajadili kwa nini waganga wanaweza kuwapatia watu wengine dawa au mbinu za kuwa matajiri wakati wao ni masikini? Na pia tutaangalia jinsi ambavyo unaweza kutumia mbinu hizi wanazotumia waganga bila ya wewe kuwa mchawi na ukafikia mafanikio makubwa.
Kila mmoja wetu anaelewa kwamba kuna watu wanakwenda kwa waganga na wanasaidiwa kupata utajiri. Japokuwa utajiri huu haudumu, lakini angalau wanaupata kwa kiwango fulani.
Wakati waganga hawa wanawasaidia watu kuweza kujenga magorofa, wao bado wanakaa kwenye vibanda vya nyasi. Sasa kwa nini wao wasingetumia uchawi wao na kuwa matajiri zaidi ya hao wateja wao? Ina maana wao hawapendi utajiri huo?
Mbinu za waganga kuwasaidia watu kupata utajiri. Watu wanaokwenda kwa waganga ili kupata utajiri au mafanikio yoyote hupewa masharti ambayo ni magumu kwa kiasi fulani. Na watu hawa huambiwa wakivunja masharti hayo tu utajiri wao unaisha mara moja.
Ni masharti haya ambayo humjengea mtu nidhamu kubwa sana na kumfanya aweze kufanya kazi kwa juhudi kubwa kuliko wengine ambao wanafanya anachofanya. Kwa mfano mganga anamwambia mtu kila siku aamke asubuhi na mapema sana na apasue nazi barabarani ndio aende kwenye biashara zake.
Kupasua nazi hakuna uhusiano wowote na mafanikio yake ila kuamka asubuhi na mapema kila siku ina msaada mkubwa kwenye mafanikio yake. Hivyo mtu huyu atafuata masharti haya kila siku na hata kama kuna siku hajisikii itambidi afanye tu kwa sababu ameshaaminishwa akiacha atafilisika.
Sasa wewe ambaye huna sharti la aina hii siku ukiwa hujisikii vizuri unalala, siku nyingine unachelewa na hivyo kushindwa kufikia mafanikio makubwa. Masharti mengine kama kutokufanya starehe, kutokunywa pombe, kuvaa nguo moja na mengine mengi yanapelekea mtu kupunguza matumizi na kupata muda mwingi wa kufikiria kazi au biashara yake.
Masharti mengine yanayotolewa na waganga ni kumfanya mtu aweze kuondoka kwenye woga wake(comfort zone). Kila mmoja wetu kuna vitu fulani anaogopa kufanya, lakini vitu hivi ndio vinaweza kumletea mafanikio.
MAMBO 13 YA KUDUMISHA MAHUSIANO YAKO EWE MWANAMKE, YAKO HAPA BOFYA KWENYE PICHA
1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubutu wako.
2. Mwanamke anaemuheshimu mumewe ni mwanamke bora ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae.
3. Tabia yako na misimamo yako ndio itakayomfanya mumeo ajute au afurahie kukuoa wewe.
4. Kuwa mke bora inakubidi uwe vizuri katika maarifa ya kutawala hasira zako na sio kuwa mtu wa kulipiza visasi.
5. Kuwa kiongozi huko kazini kwako lakini kuwa mtu wa kunyenyekea nyumbani kwako kwa mumeo. Hiyo ni busara.
6. Usiweke mashindano na mumeo, mpe hongea na mtie moyo kwa kila hatua anayopiga katika maisha.
NOBODY IS A TOTAL FAILURE IF HE DARES TO TRY TO DO SOMETHING
WASANII WANAMALIZWA NA KITU HIKI HAPA, SOMA ZAIDI UJUE
Kullu nafsin zaikatul maut! Huo ni mstari katika kitabu kitakatifu cha Quran unaomaanisha kila nafsi itaonja mauti. Wimbi la vifo vya wasanii linazidi kuitingisha tasnia ya burudani Bongo. Ndani ya kipindi kifupi cha miaka michache iliyopita, tumeshuhudia wasanii wengi wa filamu na muziki, maarufu na wasio maarufu, wakipoteza maisha kwa sababu mbalimbali.
Marehemu Recho Haule enzi za uhai wake. Wataalamu wa afya akiwemo Dk. Mandai A. Mandai wa hospitali ya Temeke ambaye alitaja sababu zinazosababisha wasanii wengi kufariki: 1. KUKOSA TABIA YA KUPIMA AFYA MARA KWA MARA, Wasanii wengi wa Kibongo hawana utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara. Wengi huenda hospitali wakiwa tayari wanaumwa na matokeo yake, hata yale maradhi ya kawaida ambayo yangeweza kutibika mapema na kupona, yakiwemo malaria, kifua kikuu na mengineyo, huwasababishia vifo. JIHADHARI, HAYA NI MAZINGIRA KISHERIA AMBAPO ALIYEKUUZIA ARDHI ANAWEZA KUDAI TENA UMILIKI NA AKAUPATA
Kisheria yapo mazingira ambapo mtu aliyeuza ardhi anaweza kuidai tena ardhi ileile aliyouza kutoka kwa mnunuzi na akaipata. Na hapa haijalishi kama mnunuzi ameiendeleza ardhi kwa kiasi gani au amebadilisha hati na kuingia jina lake na vitu vingine kama hivyo.
Sheria imetoa haki hii kwa muuzaji hasa iwapo masharti katika mkataba wa mauziano yamevunjwa. Kwa kawaida kila mkataba wa mauziano ya ardhi huwa na masharti ambayo hupaswa kutekelezwa na kila upande. Masharti haya huwa ni ya msingi na hupaswa kutekelezwa vilevile kama ilivyokubaliwa.
SERIKALI YA PUNGUZA TOZO YA ARDHI KWA ASILIMIA 50% LEO
HAIJAWAI KUTOKEA KWA WATOTO KUWA NA KIPAJI KAMAHIKI

JIFUNZE JAMBO JIPYA KUTOKA KWENYE KITABU KITAKATIFU






























