Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MINI SHOP CHETA

Mini ShopCheta au Duka Dogo

Ni duka dogo kweli kama jina lake linavyojieleza hapo juu. Duka hili linatoa huduma ya mahitaji ya kawaida ya kila siku kwa wakazi wa Kitongoji cha Cheta pamoja na maeneo ya jirani au kwa lugha nyingine tunaweza kusema Mini Shop inatoa huduma ya jamii kwa watu wote. Mini Shop ilianzishwa tangu mnamo tarehe 18/01/2018.

Tulianza tunauza bidhaa chache sana, bidhaa izo ilikuwa ni pamoja na Dawa ya Mbu zile za vidonge za kuchoma, Viberiti, Karanga, Ubuyu pamoja na Tauro za wanawake (Ped). Na kipindi icho tulikuwa tunauza bidhaa izo kutokea nyumbani kabla ya kujenga Frem hii rasmi ya kufanyia biashara kama inavyo onekana hapo kwenye picha.

Mini Shop a.k.a Duka Dogo tunauza bidhaa mbali mbali ila kwa ucheche tu, zifuatazo ni baadhi ya bidhaa tunazouza. 

Maji
Pipi
Unga
Tambi
Ngano
Amira
Juice
Mikate
Sigara

Chumvi
Mchele
Sukali
Karamu
Battery
Viwembe
Vitunguu
Viberiti
Biscuits
Madaftari

Vichongeo
Majani ya Chai
Dawa ya Mswaki
Jumbo Ball Gum
Sabuni za kuogea
Mafuta ya kupaka
Viungo vya Pirau
Mafuta ya kupikia
Sabuni za kufuria

Maharage ya Njano
Maharage ya Kombati
Tauro za wanawake (Ped)
Pon Pon au Bambino za watoto wachanga
Pia Mini Shop ni wakala wa Vodacom M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.

Karibu sana dukani kwetu, karibu sana Mini Shop_Cheta tukuhudumie leo.


(TCRA), has fined two radio stations

THE Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), has fined two radio stations, including Dodoma based FM radio station (RASI FM), 6m/- for violating content regulations.
TCRA’s Content Committee Vice-Chairman, Joseph Mapunda, said in Dar es Salaam that the two radio stations violated the regulations in January, saying RASI FM violated the regulation on June 6 while the other radio station, Dar es Salaam based Magic FM did so on May 18.
Mr Mapunda said the two stations have been given the penalty due to various misconduct charges imposed by the communication’s watchdog.

Speaking at a news conference in Dar es Salaam yesterday, the TCRA Content Committee Vice-Chairman said on June 6 this year RASI FM in its mid day programme aired a topic on sexual matters, where the radio station’s presenter blatantly disregarded the broadcasting ethics and regulations by discussing the topic in inappropriate hours as per electronic broadcasting regulations.
He said that the topic was aired at the wrong time of day because at that time most children and teenagers are usually listening to various programmes aired by various radio stations, so it was inappropriate and against the country’s culture and could lead to moral decay among children and teenagers.
“Promoting sexual acts is an unlawful offence, so RASI FM has confessed and apologised for the misconduct and have already taken some disciplinary measures against the presenter who conducted the programme by firing him,” said Mapunda.
However, the committee has also slapped a fine of 2m/- on the radio station for the misconduct after establishing that the station failed to protect children’s rights by promoting sexual activity and setting adult topics during inappropriate time.

source Daily News Tanzania

Kutoka CHETA KAZOLE kwenda VIKINDU GETINI ni 6.749Km Pekee.

Ukweli ni kwamba kutoka Vikindu Getini kwenda kijiji cha Kazole sio mbali, ni wastani wa 6.749Km au 7Km pekee kutoka Vikindu getini hadi Kazole kwenye kitongoji cha Cheta.

Ila panaonekana kuwa mbali kutokana na ubovu wa miundombinu iliyopo ikiwemo ubovu wa barabara, ukosefu wa umeme, hospital/ Zahanati nk.

 Leo naomba niupongeze uongozi wa kijiji cha Kazole kwa kuchonga Barabara yenye urefu wa wastani wa 4Km kutoka Kazole Magenge 20 hadi kitongoji cha Cheta. 

Zoezi ili lilianza juzi tarehe 21/2/18 na kumalizika jana tarehe 22/2/18.
 Kuchonga na kufunika Mashimo kwenye baadhi ya maeneo ya barabara hii kutasaidi kwa namna moja au nyingine kwa Magari yanayotoa huduma kwa abiria kutoka Vikindu mpaka Magodani. 
Maoni yangu nikwamba mmefanya vizuri kuchonga hii barabara lakini mnaonaje ikawekwa kifusi au Changarawe ili kuifanya iwe imara zaidi ili kuwaondolea adha ya usafiri wakazi wa Kazole, Cheta na Magodani kwa kipindi cha mvua kinacho karibia kuanza mwezi ujao? 

KAZOLE: MKOMBOZI WA NYATI CEMENT INDUSTRY NI BARABARA YA VIKINDU GETINI KUPITIA KAZOLE, CHETA, MAGODANI, MWASONGA HADI KIMBIJI.

Cheta: Mkombozi wa Nyati Cement Industry ni barabara ya Vikindu getini kupitia Kazole, Cheta, Magodani, Mwasonga hadi Kimbiji.

Kimbiji kuna muwekezaji wa kiwanda cha Nyati cement ambapo katika utoaji wa huduma yake kwa watanzania hulazimika kutumia barabara ya Kibada uku Kigamboni ili kusafirisha cement kutokea Kimbiji hadi mjini.

Lakini kuna barabara ambayo ni fupi sana kuliko ile anayoitumia muwekezaji uyo wa kiwanda cha Nyati Cement kwa sasa.

Barabara iyo fupi inayozungumziwa ni ile inayoanzia Vikindu Getini kupitia Kazole, Cheta, Magodani, Mwasonga hadi Kimbiji na kuunganisha maeneo mbali mbali ya katikati ambayo ayajatajwa.

Kuimarika kwa barabara hii ya Vikindu Getini kupitia Kazole, Cheta, Magodani, Mwasonga hadi Kimbiji kutampunguzia muwekezaji huyu adha ya usafirishaji wa Cement yake na kumuongezea nguvu ya kuzalisha cement nyingi zaidi.

Pia kuimarika kwa barabara hii ya Vikindu getini kupitia Kazole, Cheta, Magodani, Mwasonga hadi Kimbiji kutatoa fursa kwa wakazi wa maeneo tajwa kukua kibiashara, kiuchumi ata kisiasa nk.

Kwa sasa barabara hii ya Vikindu getini kupitia Kazole, Cheta, Magodani, Mwasonga hadi Kimbiji ipo kama unavyo iona kwenye picha hapo juu na chini.
KAZOLE: MKOMBOZI WA NYATI CEMENT INDUSTRY NI BARABARA YA VIKINDU GETINI KUPITIA KAZOLE, CHETA, MAGODANI, MWASONGA HADI KIMBIJI.

Pia wakazi wa maeneo tajwa wanapata shida sana katika kusafiri, ambapo kutoka Vikindu getini hadi Kazole magenge 20 ni umbali wa dakika 15 hadi 20 ila kila abiria hutozwa Tsh. 500 na mwanafunzi tsh. 200 hadi tsh. 250.

Huku Noah zinazoanzia Vikindu getini kwenda hadi Magodani zikipitia Kazole magenge 20 pamoja na Cheta kila abiria anatozwa Tsh. 1,000 ukiwa ni umbali wa kama dakika 30 hadi 35 tu.

Izo bei za nauri hutozwa kipindi cha kiangazi ila ikifika masika nauri upanda hadi mara 4, wakazi wa Kazole ulipa tsh. 2,000 na wakazi wa Cheta na Magodani ulipa tsh. 4,000 na Boda boda uwa ni kati ya tsh. 5,000 mpaka tsh. 10,000

Lakini mbali ya nauri kuwajuu namna hiyo japo sio viwango elekezi kutoka SUMATRA, bado kuna changamoto ya uchache wa magari yanayotoa huduma, kwaiyo tunamuomba Mhe. Rais Magufuri na serikari yake kupitia wizara ya ujenzi walitazame swala hili kwa jicho la tatu.

Habari zaidi kuhusu Kazole, Cheta na Magodani zisome kupitia hapo chini.

Barabara ya Magodani, Cheta, Kazole, Kilongoni hadi Vikindu kufanyiwa ukarabati. 


WAKAZI WA CHETA WANATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI NA KANISA 

CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO.

KWA HABARI ZAIDI INGIA HAPO CHINI








CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO.
CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO. 
Cheta ni kitongoji kinachopatikana ndani ya kijiji cha Kazole kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, ni jirani kabisa na mkoa wa Dar es salaam.

Maendeleo huletwa na watu, watu wenyewe ndio sisi tukishirikiana na viongozi wetu ndipo tunaweza kupiga hatua chanya kuelekea kwenye kilele cha mafanikio.

Ila wazo ili naona linapingana na uhalisia wa maisha ya wananchi na wakazi wa eneo la Cheta pamoja na viunga vyake.

Ikiwa imepita miezi michache ndani ya mwaka huu wa 2017 tayari zimeonekana alama za vijiti zinazo ashiria njia za uwekaji wa nguzo za umeme.

CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO.
CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO. 
Alama izo zimetokea eneo la Vikindu zimepita eneo la Kazole mjini, Kazole shule ya msingi iliyopo mpakani na eneo la Hamidu na nguzo ya mwisho imeishia Kazole Magenge 20 eneo la njia panda ya kwenda kwa Bakhresa ambapo ndipo mpakani mwa Kazole na Cheta.

Sasa kuanzia hapo mpakani mwa Cheta na Kazole kwenda hadi mpakani mwa Cheta na Magodani hakuna alama yoyote inayo onyesha kuwa nguzo za umeme zitapita ili kwenda mpaka Magodani.

Cheta ipo ndani ya Kazole uku ikipakana na Magodani ila viongozi wa kazole kwa ujumla wamekuwa wakipasahau sana Cheta.

CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO.
CHETA TUNATAKA BARABARA, SHULE, UMEME, SOKO, HOSPITAL, MAJI, MSIKITI, KANISA NA VIWANJA VYA MICHEZO.
Baada ya uongozi wa Magodani kuchonga barabara yao kuanzia mpakani mwa Cheta kuelekea kwao ndipo Kazole wao walisimika alama za kuonyesha njia za nguzo za umeme zitakapo pita na wao wakaishia mpakani mwa Kazole na Cheta
Je Cheta inayoachwa katikati inaongozwa na akina nani?? Na je kama ina viongozi wake ivi wao wanatambulika upande wa Magodani au upande wa Kazole?? Wananchi wanataka kufahamu.

Kumbuka wakazi wote wa maeneo ya Mwasonga, Magodani, Cheta, Kazole na Vikindu wanategemea Barabara inayoanzia Vikindu hadi uko Mwasonga pamoja na maeneo mengine ambayo sikuyataja sasa je kama maendeleo na miundo mbinu vinawekwa mwanzoni mwa eneo na mwishoni bila kupaunganisha katikati je kunatengeneza kitugani jamani??
Wananchi wa Cheta wanataka maendelea ya kweli kwa vitendo nasio maendeleo ya kuongea mdomoni na kuwadanganya kwenye mikutano ya vijiji inayofanyika.

Wakazi wa Cheta wanataka Barabara safi, Shule ya msingi na ya Sekondari, Hospital, Soko, Umeme, Visima vya Maji masafi, Viwanja vya Michezo, Sehemu za ibada (Miskiti/Makanisa), Maziko nk.

Kauli ya mhe.Zitto Kabwe juu ya mbunge wa Mtama Nape Nnauye kuondolewa kwenye uwaziri iko hapa

"Nimezungumza ma mbunge wa Mtama Nape Nnauye na kudhibitisha ni kweli ameondolewa kwenye uwaziri.

Nape ni shujaa wa kizazi chetu" Zitto Kabwe.

KITUO CHA MABASI YAENDAYO MIKOANI KUAMISHIWA MKURANGA, INGIA HAPA.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa Wilaya za Temeke na Mkuranga kuangalia namna ya kupunguza msongamano uliopo katika eneo la Mbagala.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa wilaya za Mkuranga na Temeke, Ofisini kwake jijini Dar es salaam Februari 7, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Moja ya hatua alizowashauri kuchukua ni pamoja na kuhamisha kituo cha mabasi ya mikoa ya kusini ya Lindi, Mtwara na Ruvuma kutoka Temeke hadi Mkuranga.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Februari 7, 2017) alipokutana na viongozi wa wilaya hizo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutafua njia za kuondoa msongamano huo.

Amesema kwa sasa hakuna namna ambayo wataweza kuondoa msongamano huo zaidi ya kuhamishia kituo cha mabasi ya mikoa ya kusini wilayani Mkuranga.

Waziri Mkuu amesema eneo la Mbagala kwa sasa lina msongamano mkubwa ambao ni lazima Serikali ichukue hatua za haraka za kuuondoa.

“Ikiwezekana mabasi ya mikoa ya kusini yaishie Mkuranga, hivyo shirikianeni kutafuta eneo la kujenga kituo kikubwa cha kisasa cha mabasi,” amesema.

Amesema kituo hicho watakachokijenga kiwe na uwezo wa kuhudumia mabasi yote yatokayo mikoa ya kusini na kituo cha Mbagala kiwe cha daladala za kawaida.

Pia Waziri Mkuu amesema kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa kituo hicho kutawezesha kuongeza mapato ya Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga.

Aidha Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kwenda kujadiliana katika vikao vya mabaraza ya Madiwani juu ya mkakati huo na kisha kumpelekea taarifa ifikapo Februari 15 mwaka huu.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Bw. Filberto Sanga amesema wazo hilo ni zuri na wilaya yake ina maeneo ya kutosha kujenga miundombinu hiyo.

“Ni kweli wilaya ya Temeke imeelemewa kwa maana ya maeneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maendeleo na haina pa kupumulia zaidi ya Mkuranga , hivyo tupo tayari kushirikiana nao,” amesema.

Wakati huo huo, Bw. Sanga ameiomba Serikali itakapoanza awamu ya tatu ya ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendo kasi ufike hadi Mkuranga mjini badala ya kuishia Vikindu.

Amesema kwa sasa wilaya yake ina viwanda 67 ambavyo kati yake vipo vinavyofanya kazi na vingine vikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi, hivyo mabasi hayo yatarahisisha usafiri kwa wafanyakazi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva amesema amefurahishwa sana na mawazo hayo ya kuhamisha kituo cha mabasi cha Mbagala kwani katika vitu vilivyokuwa vinamnyima usingizi ni pamoja na msongamano wa mabasi na wafanyabiashara wadogo wadogo katika eneo hilo.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitaka Michuzi TV, AYO TV na Global TV kusitisha huduma zao za TV

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitaka Michuzi TV, AYO TV na Global TV kusitisha huduma zao za TV

mtandaoni hadi hapo kanuni za usajili rasmi ambazo mamlaka hiyo imesema inaandaa  kwa huduma hizo zitapokuwa tayari.

Barua hiyo, iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu Mhandisi James Kilaba tarehe 30 January mwaka huu, imevitaka vyombo hivyo ambavyo vinapendwa sana nchini na nje ya nchi kuacha mara moja kutoa huduma za TV mtandaoni.

“Kwa mujibu wa section 13 (1) of the electronic and postal communications Act Cap 306, sheria za Tanzania zinahitaji watoa huduma zozote za aina hiyo wanahitaji leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano,” imesema barua hiyo.

Wamiliki wa mitandao hiyo Millard Ayo, Ankal Issa Michuzi na Abdallah Mrisho wameeleza kushtushwa kwao kwa agizo hilo la ghafla, tena wakati hata kanuni zenyewe hazijawekwa.            

“Global TV ipo tayari hata leo kukamilisha taratibu za usajili kama zingekuwepo na kwa sababu bado kukamilika tunaomba kupewa muda zaidi chini ya uangalizi wakati tunasubiria kanuni hizo mpya,” alisema Abdallah Mrisho, Meneja Mkuu wa Global Publishers.

Ankal Michuzi na Millard  Ayo waliunga mkono kauli hiyo na kwa pamoja watatu hao wameomba kuonana na mkurugenzi wa TCRA ili kuwasilisha maombi rasmi ya kuruhisiwa kuendelea kutoa huduma hiyo kwa muda wakati kanuni zikisubiriwa.

Bahati mbaya Mhandisi Kilaba alikuwa safari na swala hilo limepangwa kushughuliwa ataporejea wiki ijayo.

“Ukizingatia kwamba tumekuwa tunatoa huduma hii kwa muda mrefu na haijulikani kanuni zitakuwa tayari lini tunaomba TCRA iangalie namna ya kufanya ili wananchi wanaotutegemea sana wasikose huduma hii,” alisema Ankal. Hata hivyo vituo hivyo vitatu vinaendelea kuhudumu nje ya mchakato wa TV mtandao.

Ayo TV, Michuzi TV na Global TV  ambazo zina watazamaji wengi ndani na nje ya nchi, ni TV mtandao pekee zilizoitikia mwito wa TCRA kati ya vituo mtandao  takriban 51 vilivyopata barua hiyo.

Na Sultani Kipingo, Globu ya Jamii

Gwajima: Lengo la kikao hiki cha leo ni kuwajulisha Maaskofu wenzangu kwamba ni nini kimetokea

Gwajima: Lengo la kikao hiki cha leo ni kuwajulisha Maaskofu wenzangu kwamba ni nini kimetokea baada ya mkuu wa mkoa kutamkwa kwamba ama anawahitaji watu wasaidie kuidentify swala la madawa ya kulevya au anawataka wanaojihusisha au kutumia madawa ya kulevya. Mimi likuwa safarini Mpwapwa jana nikasikia kwamba jina la Askofu Gwajima limetajwa na mkuu wa mkoa

Gwajima: Sijawahi kunywa Pombe wala sijawahi kuvuta sigara, Mimi nlikuwa mgonjwa hadi nlipookoka nikawa mchungaji moja kwa moja. Kama sijawahi kuvuta sigara siwezi kuwa natumia madawa ya kulevya.

Gwajima: Nakumbuka Kuna siku Makonda alikuwa anahutubia, akamwambia Waziri mkuu eti nlipiga marufuku shisha lakini imerudi, hawa wavuta shisha waliniletea Milion 5 nikakataa akasema lakini naamini kamanda Siro hizi milioni tano tano zimepita kwao. Makonda alidiliki kumtuhumu Waziri MKuu eti Karudisha Shisha!?. DC Makonda ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar, kwanini hakuisemea kwenye Vikao, Kwanini alisubiri Media?

Gwajima: Safari hii kamfikia kiongozi wa Kiroho, huu ni unafiki sana. Huweze kumuita rafiki yako kaka yako namna hii.

Gwajima: Sasa leo nataka niwambie kwanini Makonda anafanya hivi;

1. Nataka niwambie, Rais hajamtuma Makonda atutuhumu sisi

2. System za Serikali zimeparalyse kwa sababu watendaji wa Serikali na Mawaziri wanamuona Makonda ni Mkono wa kiume wa Rais. Wanafikiri labda kwakuwa Makonda ni Msukuma basi atakuwa anatumwa na rais, Rais hawezi kufanya hivyo. Mawaziri wamekosa neno wamekaa Kimya.

Gwajima: Nani anatakiwa kuniita mimi kama Askofu Mkuu Polisi? Ni Polisi sio Makonda. Makonda anajiona kama Mkuu wa Wakuu wa Mikoa yote na Mawaziri wote.

Gwajima: Sio desturi ya rais hata kidogo eti awatenge Mawaziri wake eti aongee na Makonda. Rais alikuwa anampongeza makonda kwa sababu kafanya Vizuri. Makonda anaujasiri na anajituma hivyo rais kumpongeza ni halali. Makonda anaweza kuwa Kiongozi Muu siku zijazo kama akiondoa baadhi ya Hitilafu.

Gwajima: Makonda angeweza kunipigia simu au Kuwagiza Polisi wakaniletea samasi au kuniita.

Gwajima: Nia ya Makonda ni kutaka jina la Gwajima liharibike. Kama Gwajima hafanyi na hajihusishi na Madawa ya kulevya watu wa Usalama wanajua. Nmefanya hii kazi ya Uchungaji kwa Miaka 20.

Gwajima: Si kweli kwamba makonda anatumwa na Rais Magufuli, rais ana tabia ya kupongeza saa nyingine anapiga simu Clouds kupongeza pale wanapofanya Vizuri.

Gwajima: Sisi tunamuunga mkono Mheshimiwa rais hata kama kwenye uchaguzi hatujamuunga mkono, Lakini kwa kuwa amechaguliwa yeye tunamuunga mkono

Gwajima: Naamin Makonda hajajificha kwenye "Usukuma" wake.

Gwajima: Namuomba rais amkanye Makonda. Chuki zake binafsi za mtu mmoja mmoja asiziingize kwenye system ya Serikali, ni hatari sana


Gwajima: Makonda ni Mchapakazi lakini Mambo ya Utawala hawezi, namuomba rais amtafutie kazi nyingine, nashauri umtafutie kazi nyingine, sio umfukuze.

Gwajima: Chini yangu kuna Maaskofu 125. Kesho wataogopa nao watasemwa

Gwajima: Kuna siku Paul Makonda, Sitta na Mwakyembe walikuja kanisani kwangu hata CD ninazo na alihutubia hapa kwenye Madhabahu akinisifia sana, Leo ni kitu gani kimemfanya anichafue?

Gwajima: Je ikiwa Gwajima hahusiki, itakuwaje?

Gwajima: Mimi nlikuwa mkali sana juu ya utawala wa awamu ya nne. Miaka kwa miaka Tembo walikuwa wanakufa na hakuna hatua zilizokuwa zinachukuliwa.

Gwajima: Kuna Kipindi Ridhiwani Kikwete aliwapeleka Mahakamani Dr. Slaa akitaka wakanushe habari kuhusu utajiri wake unaotokana na Madawa ya kulevya, hiyo kesi sijui iliishia wapi.

Gwajima: Nani anamtumia Makonda?

Gwajima: Makonda ana nia ovu juu yangu na juu ya Wakristo. Anataka kuwaaminisha watu kwamba wokovu haupo.

Gwajima: Mimi nataka kununua ndege nyingine ili nianzishe chuo cha ndege, mbona sipongezwi kwa hilo?

Gwajima: Jambo hili alilofanya si sawa na si sahihi.

Gwajima: Wabunge wamepiga kelele juu ya jambo hili, sisi wananchi tusio na sehemu ya kuongea tufanyeje?

Gwajima: Namfahamu rais Magufuli, hawezi kumpendelea kwa kuwa ni mtu wa kwao (Msukuma). Rais anawapenda watu wote anawapenda Mawaziri wote na watendaji wote wa Serikali. Naamin rais hajamtuma Makonda.

Gwajima: Nguvu katika mikono isiyo sahihi ni hatari sana.

Gwajima: Juzi kati tulikuwa na mechi kati ya maasikofu na viongozi, Mimi nlikuwa namba kumi yeye namba 09. Alikuwa ananiangalia macho baya sana mamcho alikuwa ananiangalia nayo nmekuja na helcopter ni macho ya chuki sana. Mimi, Makonda, kamanda Sirro Spika wa Bunge tulikuwa tunamechi si angenikamata hapo?

*Kuna watu walikuwa wanauza madawa ya kulevya, katika uongozi huu wale walikuwa wanauza madawa ya kulevya wamebadili majina na wanafanya biashara nyingine. Walikuwa na jina B sasa wamebadilisha jina.


Mh.Paul Makonda awataja wakubwa 65 leo wafike kituo cha polisi cha Dsm siku ya Ijumaa

Aliyozungumza Makonda mchana huu na waandishi wa habari!.

Anasema anaingia awamu ya pili ya mapambano ambayo siyo nyepesi,anasema itakuwa na mawimbi mengi!.

1.Yanaingizwa kutoka Pakistan kwa meli,ikishapakia mzigo wanachukua madawa kwenye mifukonya sukari inawekwa kwenye mapipa!

Meli zikikaribia kufika mapipa hutupwa huko Zanzibar,Tanga na Bagamoyo yakiwa na GPRS,baadae hurudi walipoyatupa na kuyachukua na huyasafirisha mpaka Mtwara na baadae Afrika kusini!.

2.Kwa kutumia maghari yanayoaguswa kutoka nje,

3.Ni kwenye meli za mafuta

4.Ni wale wenye maeneo yao ya kupack mizigo!

Wengine huwatumia akina dada ,hawa hupewa dolla elfu tano ili ziwasaidie kuingia China.

 
Waliotajwa leo wafike kituo cha polisi cha dar es salaam siku ya  Ijumaa kwa mahojiano ni pamoja na.

1.Mmiliki wa slipway
2.Mmiliki wa Yatchclub
3.Idd Azan
4.MMI Wine
5.Freeman Mbowe

6.Mwinyi Machapta
7.Mr Halfizi
8.Yusuph Manji
9.Mchungaji Gwajima
10.Wamiliki wote wa clubs na Cassino
11.Mzee Kiboko wa Mbezi chini
12.Rose ambaye anaishi Ghana

Jumla wapo 65 wanaotakiwa kuripoti polisi Ijumaa.

KAMA ULIKUWA UJAFANIKIWA KUYAONA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YA MWAKA 2016 BOFYA HAPA

Katika matokeo hayo, shule za Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam zimeonekana kung’ara zaidi kwa kushika nafasi za juu wakati huohuo  shule 6 za Dar es Salaam zikishika nafasi 10 za mwisho katika matokeo hayo.


Shule zilizoingia 10 bora Kitaifa.


Feza Boys Sec School – Dar es Salaam

St. Francis Girls Sec School -Mbeya

Kaizirege Junior Sec School – Kagera

Marian Gilrs Sec School – Pwani

Marian Boys Sec School- Pwani

St. Aloysius Girls Sec School – Pwani

Shamsiye Boys Sec School – Dar es Salaam

Anuarite Girls Sec School- Kilimanjaro

Kifungilo Girls Sec School- Tanga

Thomas More Machrina Sec School – Dar es Salaam


Shule za Dar es Salaam zilizoshika nafasi 10 za mwisho.


Kitonga Sec School

Nyeburu Sec School

Mbopo Sec School

Mbondole Sec School

Somangila Day Sec School

Kidete Sec School


BOFYA HAPA KUONA MATOKEO SASA

Katibu Mtendaji wa barza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372 waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana 135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26.


Kwa upande wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35 ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015.


Kwa upande wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60

Rais Magufuli leo ametengua rasmi uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme

Rais Magufuli leo ametengua rasmi uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini(TANESCO), Eng. Felchesmi Mramba. 

Aidha Rais amemteua Dkt. Tito Esau Mwinuka kukaimu nafasi hiyo. Kabla ya uteuzi huu Dkt. Mwinuka alikuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM).

Hakuna mwanaume mkorofi kwa mwanamke mnyenyekevu, bofya hapa ujifunze kitu

Hakuna mwanaume mkorofi kwa mwanamke mnyenyekevu hata ungekua umemkosea nini ukijishusha ukanyenyekea analainika labda awe na mapepo ndio unyenyekevu wako hautagusa moyo wake.

Mume hafokewi, mume hagombezwi, mume humfanyii jeuri na kiburi, akinuna na wewe unanuna asipokutafuta na wewe humtafuti,  utapoteza ndoa yako. 

Ni mume wako wa ndoa unaruhusiwa kumng'ang'ania kama ruba. Asipokutafuta mtafute, asipoongea na wewe ongea naye wewe. Hakunaga mke anaambiwaga anajipendekeza kwa mumewe.

Kunyenyekea hakukugeuzi housegirl  na ukapoteza nafasi yako ya kuwa mke, ila kiburi na jeuri ndio vitakufukuza kwenye hicho kiti na hiyo nafasi ya kuwa mke haraka sana. 

Ujeuri weka pembeni!
ndivyo wanavyofanya waliodumu kwenye ndoa zao

NOTE: Kuwa mnyenyekevu sio kuwa mpumbavu. Panapotakiwa hekima na akili zitumie!

EWURA imeridhia ombi la TANESCO la kupandishwa kwa bei ya umeme

Mamlaka ya udhibiti wa huduma  za  nishati  na maji EWURA imeridhia maombi ya shirika la umeme nchini TANESCO la kupandishwa kwa bei ya umeme ambapo Bei hiyo imeongezeka kwa wastani wa asilimia 8.5 tofauti na pendekezo la mwanzo la 18.19% huku watumiaji wa nishati hiyo ambao hawatumii zaidi ya unit 75 kwa mwezi wakiwa hawaguswi na ongezeko hilo.

Kwaiyo basi watumiaji wa umeme wa kawaida manyumbani watalazimika kununua Unit moja kwa Tsh 312 wakati kabla ya ongezeko ili unit moja ilikuwa ikinunuliwa kwa Tsh 292, bei izi zitaanza kutumika rasmi tarehe 01/01/2017 ikiwa ni ongezeko la Tsh 20 kwa kila unit moja.

TANESCO imetimiza agizo la Rais Magufuli la kukipatia umeme kiwanda cha Bakhresa

TANESCO imetimiza agizo la Rais Magufuli la kukipatia umeme kiwanda cha kusindika matunda mali ya mfanyabishara, Said Salim Bakhresa kabla ya muda wa miezi miwili waliyopewa kukamilisha kazi hiyo.

Rais alitoa agizo hilo Oktoba 6, 2016 alipokuwa anazindua kiwanda hicho kilichopo Mwandege, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.

ILE KATA FUNUA YA UKAWA YAIBUKIA KWENYE MAKAMPUNI 6 YA KIGENI YA KUCHIMBA MADINI NCHINI

Makampuni ya kimataifa yasiyopungua sita yamesema yanafikiria kupunguza kiwango cha uwekezaji nchini Tanzania, baada ya Rais John Magufuli kutangaza kufanya mabadiliko ya kiuchumi, ikiwemo kuongeza kodi kwa makampuni kutoka nje.

Kwa mujibu wa mahojiano yaliyofanywa na shirika la habari la Reuters pamoja na wakurugenzi wakuu wa makapuni ya kigeni yaliyowekeza nchini Tanzania, kiasi ya makampuni sita yanafikiria mipango mipya kuhusu uwekezaji katika sekta ya madini, mawasiliano ya simu au usafirishaji kwa kutumia meli. Hiyo yote inatokana na juhudi zinazofanywa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuubadili uchumi wa nchi hiyo.

Makampuni matatu yamesema huenda yakapunguza shughuli zake za uwekezaji kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki, huku makampuni mengine mawili yakisema yanafikiria kutanua zaidi shughuli zake katika nchi jirani na kampuni moja imesema inaandaa mchakato wa kujiondoa kabisa nchini Tanzania. Makampuni hayo yaliombwa kutotajwa majina kwa sababu ya umuhimu wa suala hili na kwa sababu mipango yao hiyo bado haijatangazwa hadharani.

Kampuni moja bado haijatoa msimamo wake jinsi ya kukabiliana na mageuzi hayo ya serikali ya Tanzania, huku makampuni matano yakisema kuwa mipango yao haikuathirika na mageuzi hayo, ikiwemo miradi miwili mikubwa, ule wa kiwanda cha kusindika gesi asilia-LNG wenye thamani ya Dola bilioni 30 na mradi wa kiwanda cha mbolea wenye thamani ya Dola bilioni 3.


Tanzania na uwekezaji wa kigeni

Tanzania inategemea zaidi uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja, kuliko nchi nyingine za ukanda huo, kutokana na ukubwa wa uchumi wake. Mwaka uliopita nchi hiyo ilipokea zaidi ya Dola bilioni 1.5, kwenye uchumi ambao thamani yake ilikuwa chini ya Dola bilioni 45. Hiyo ni kwa mujibu wa takwimu za Mkutano wa Biashara na Uwekezaji wa Umoja wa Mataifa pamoja na Benki ya Dunia.

Rais wa Tanzania, John Magufuli ambaye amepewa jina la utani ''Tingatinga'' kutokana na miradi yake ya miundombinu na aina ya uongozi wake, alizindua mchakato wa mageuzi yake ya kiuchumi, baada ya kuchaguliwa kuiongoza nchi hiyo mwaka uliopita, akiahidi kuubadilisha uchumi wa nchi hiyo, kuondoa urasimu na rushwa pamoja na kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi.

Mwaka huu serikali ya Magufuli iliongeza kodi katika utumaji wa fedha kwa kutumia simu za mkononi, mabenki, huduma za utalii na zile za usafirishaji wa mizigo. Kodi ya mapato kwa mwaka wa fedha 2014/2015 jumla ilikuwa Shilingi za Tanzania trillioni 9.8 ambazo ni sawa na Dola bilioni 4.5. Kwa mwaka wa fedha 2016/2017, serikali ina lengo la kukusanya kodi ya mapato zaidi ya trilioni 15.1, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 50.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Adolf Mkenda, amesema wameyasikia malalamiko yanayotolewa na milango iko wazi, lakini wanahakikisha kuwa kila mtu analipa kodi anayopaswa kulipa kwa kuzingatia haki. Amesema lazima kuwepo na mageuzi mapya ambayo ni magumu, ili kuufanya uchumi kuwa imara.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Richard Kayombo amesema ongezeko la kodi ya mapato lilihitajika kwa ajili ya kulipia miundombinu mipya nchini humo. Makampuni makubwa ya kigeni ambayo yamewekeza nchini Tanzania ni pamoja na yale ya nishati, uhandisi, mawasiliano ya simu, madini, na usafirishaji kwa kutumia meli.

Source: Reuters Africa

Kama uliikosa Ile habari ya madada poa wa Dar, basi iko hapa kwa ajili yako

Akiwa katika eneo hilo baada ya kukatiza vichochoro kadhaa, alifika eneo la klabu cha pombe za kienyeji, na kuzungumza na mmoja wa wateja waliokuwa wakinywa hapo.

“Hii achana nayo kabisa ni moto wa kuotea mbali. Hebu niikate kidogo uone”, Mzee aliyejitaja kwa jina la Mandela, alimtambia Makonda huku akipiga funda la pomne hiyo ya kienyeji hali inayoonyesha kuwa hakuwa akifahamu kuwa anayezungumza naye ni Mkuu wa mkoa.

Baadaye alienda eneo lenye vibanda vya chumba kimoja kimoja, amabavyo inaelezwa kuwa ni madanguro ambayo hutumika kufanyika biashara ya ukahaba hadi kwa wasichana wenye umri mdogo.

Hata hivyo kila mlango aliojaribu kugonga Makonda, ulikuwa umefungwa na hakuna aliyeitika hodi yake.

” Hawa wakijua watu wa serikali wanakuja hapa basi hufunga biashara zote. sasa na hapa wamefunga, si rahisi kumpata mtu” Kijana mmoja mwenyeji wa eneo hilo alieleza.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Shuleya Msingi Tandale Makonda alisema, serikali inafanya mipango ya kupata wawekezaji ili kununua eneo hilo la Uwanja wa Fisi na kuwalipa fidia wakazi wa eneo hilo ili vibanda vyote vivunjwe na kujengwa vitegauchumi. badala ya kuliacha eneo hilo liharibu maisha ya vijana.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alibisha hodi kwenye mlango mmoja katika banda linalodaiwa kutumiwa kwa biashara ya ukahaba, katika eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Fisi, lililopo, Tandale Kata ya Manzese, akiwa katika siku ya tisa ya ziara yake mkoani humo leo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Hapi. 

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, akimsaidia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kubisha hodi kwenye mlango mmoja katika banda linalodaiwa kutumiwa kwa biashara ya ukahaba, katika eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Fisi, lililopo, Tandale Kata ya Manzese. 

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alichunguza kwa makini bia ili kuthibitisha kama muda wake wa matumizi bado haujapita. Makonda alisema, kuna taarifa kwamba wafanya biashara za vileo katika Uwanja wa Fisi wamekuwa wakiuza viwaji hadi vilivyokwisha mda wake wa matumizi.

 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Salum Hapi, alimpatia maelezo Makonda baada ya kufika eneo la Uwanja wa Fisi, Tandale, kata ya Manzese.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alizungumza na wateja wa pombe za kienyeji kwenye kilabu cha pombe hizo kilichopo Uwanja wa Fisi, alipofanya ziara katika eneo hilo leo

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliondoka kwenye eneo la Uwanja wa Fisi baada ya kujionea mambo mbalimbali katika eneo hilo.

Viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza vyazidi kuongezeka nchini.Soma zaidi hapa


Viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza vyazidi kuongezeka nchini.Soma zaidi hapo chini kisha washirikishe na wenzio.

Asilimia kubwa ya wanawake tunapenda kuwa na wanaume wanaojiweza kiuchumi

Asilimia kubwa ya wanawake tunapenda kuwa na wanaume wanaojiweza kiuchumi. Lakini tunapotambua kwamba wameshaoa hushangaa sana na huumia na kusema wanaume wote ni mbwa tu.

Wanaume sio mbwa ni sisi wenyewe ndio tumeshindwa kufanya uchunguzi. 

Tulishaambiwa kwenye kila mafanikio ya Mwanaume nyuma yake Kuna mwanamke. Na wewe unataka Mwanaume mwenye mafanikio unategemea nini???

Huyo sio mumeo mtarajiwa huyo ni mume wa mtu Fulani Ni agharabu sana kukutana  na Mwanaume anayejiweza akawa single, either uwe shareholder au unyanganye share ya mwanamke mwenzio kitu ambacho sio busara.

Mume wako yupo anahangaika kutoka kimaisha anapigania ndoto zake. Huenda yuko shule, shambani, dukani au anabeti kimsingi yupo anapigania kutoka Kimaisha.

Anakusubiri tu wewe umpe support na back-up ya kutosha mtafute huyo uanze nae chini na sio kukimbilia waume za watu.

Zoezi la kusaka viroba feki na pombe nyingine haramu linaendelea, habari kamili iko hapa

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla, ambaye anaongoza timu ya Serikali yenye wataalamu na wanausalama, kusaka viroba feki na pombe nyingine haramu.

Amekamata shehena kubwa ya bidhaa hizo feki na haramu kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kukifuma kiwanda bubu kinachotengeneza konyagi  na Smirnoff feki maeneo ya Sinza jijini Dar es salaam.


Kiwanda hicho kinatengeneza vinywaji hivyo kwa kutumia 'spirit' ambayo inachanganywa na gongo.


Pia katika zoezi hilo wameweza kukamata chupa tupu na zilizojazwa pombe, vizibo, pamoja na vifungashio.


Polisi inawashikilia watu wawili ambao inasemekana wanafanya kazi pamoja na bwana Yusuf Abdul Kalambo, ambaye anatafutwa na polisi mpaka sasa.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top