Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

Kama uliikosa Ile habari ya madada poa wa Dar, basi iko hapa kwa ajili yako

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Akiwa katika eneo hilo baada ya kukatiza vichochoro kadhaa, alifika eneo la klabu cha pombe za kienyeji, na kuzungumza na mmoja wa wateja waliokuwa wakinywa hapo.

“Hii achana nayo kabisa ni moto wa kuotea mbali. Hebu niikate kidogo uone”, Mzee aliyejitaja kwa jina la Mandela, alimtambia Makonda huku akipiga funda la pomne hiyo ya kienyeji hali inayoonyesha kuwa hakuwa akifahamu kuwa anayezungumza naye ni Mkuu wa mkoa.

Baadaye alienda eneo lenye vibanda vya chumba kimoja kimoja, amabavyo inaelezwa kuwa ni madanguro ambayo hutumika kufanyika biashara ya ukahaba hadi kwa wasichana wenye umri mdogo.

Hata hivyo kila mlango aliojaribu kugonga Makonda, ulikuwa umefungwa na hakuna aliyeitika hodi yake.

” Hawa wakijua watu wa serikali wanakuja hapa basi hufunga biashara zote. sasa na hapa wamefunga, si rahisi kumpata mtu” Kijana mmoja mwenyeji wa eneo hilo alieleza.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Shuleya Msingi Tandale Makonda alisema, serikali inafanya mipango ya kupata wawekezaji ili kununua eneo hilo la Uwanja wa Fisi na kuwalipa fidia wakazi wa eneo hilo ili vibanda vyote vivunjwe na kujengwa vitegauchumi. badala ya kuliacha eneo hilo liharibu maisha ya vijana.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alibisha hodi kwenye mlango mmoja katika banda linalodaiwa kutumiwa kwa biashara ya ukahaba, katika eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Fisi, lililopo, Tandale Kata ya Manzese, akiwa katika siku ya tisa ya ziara yake mkoani humo leo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Hapi. 

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, akimsaidia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kubisha hodi kwenye mlango mmoja katika banda linalodaiwa kutumiwa kwa biashara ya ukahaba, katika eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Fisi, lililopo, Tandale Kata ya Manzese. 

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alichunguza kwa makini bia ili kuthibitisha kama muda wake wa matumizi bado haujapita. Makonda alisema, kuna taarifa kwamba wafanya biashara za vileo katika Uwanja wa Fisi wamekuwa wakiuza viwaji hadi vilivyokwisha mda wake wa matumizi.

 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Salum Hapi, alimpatia maelezo Makonda baada ya kufika eneo la Uwanja wa Fisi, Tandale, kata ya Manzese.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alizungumza na wateja wa pombe za kienyeji kwenye kilabu cha pombe hizo kilichopo Uwanja wa Fisi, alipofanya ziara katika eneo hilo leo

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliondoka kwenye eneo la Uwanja wa Fisi baada ya kujionea mambo mbalimbali katika eneo hilo.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top