Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

ADAM KIMBISA AKANUSHA HABARI YA KUAMA CCM

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa amekanusha uvumi kuwa ameungana na wenyeviti wengine wa mikoa wa CCM kukihama chama tawala nchini. Amesema wanaomzushia washindwe na walegee, kwani moyo na mwili wake upo CCM na kwamba kamwe hawezi kuhama.

Aliyasema hayo jana mjini hapa kutokana na kuwapo kwa taarifa amekihama chama hicho. Awali, jana kulikuwa na taarifa za Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole kuhamia Chadema, kama ilivyokuwa kwa Mgana Msindai, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida aliyetangulia Chadema wiki iliyopita baada ya kushindwa kura za maoni ndani ya CCM.

Katika kuthibitisha hayo, Kimbisa jana alikuwa akiendesha vikao vya Kamati ya Siasa ya Mkoa akiwa katika sare zake za chama. Taarifa hizo zimekuja huku Kimbisa akiwa na habari nyingine katika gazeti hili (ukurasa wa 21) akielezea kushangazwa na wanaokihama chama baada ya kushindwa katika michakato ya kuwania uongozi, huku akisema kamwe yeye hawezi kufanya hivyo.

“Mwaka 2010 niligombea ubunge Jimbo la Dodoma Mjini nikahesabu kura zangu mwenyewe nyumbani nikajiona nimeshinda nikalala, asubuhi nilipoamka kumbe wagombea wenzangu wakaunganisha matokeo yao mgombea mmoja akaonekana ameshinda, lakini bado sikuhama na hadi leo nina damu ya kijani.

“Mtu akihangaika kuondoka CCM baada ya kushindwa tutamfuata hukohuko na tutampiga kwa kura tu,” alisisitiza Kimbisa.


Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top