Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

NAPE ATAFSILIWA VIBAYA KWA MANENO YAKE JANA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Katibu Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, wakati wasanii mbalimbali wakitumbuiza katika uzinduzi huo, alikuwa aliwapiga vijembe vyama vinavyounda na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwamba vimebeba makapi akidai kuwa wanadhani watangia Ikulu.

Nape alikuwa akimaanisha makapi ni waliokuwa makada wa CCM ambao wamekihama chama hicho kwa nyakati tofauti na kujiunga upinzani kama  Chadema, na NCCR- Mageuzi na CUF.

Miongoni mwa makada hao walitimkia Ukawa ni waliokuwa mawaziri wakuu, Edward Lowassa (Chadema) na Frederick Sumaye (NCCR-Mageuzi).
Baada ya Lowassa kujiunga na Chadema, aliteuliwa kuwania urais akiwalisha Ukawa wakati Sumaye juzi baada ya kuhama CCM alisema amekwenda kuimarisha upinzani.

Naye Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Makongoro Nyerere, aliponda  makada wa CCM waliohamia upinzani wakiwamo Mawaziri Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye. ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara tangu mwaka 2007 hadi 2012, alidai kuwa Sumaye siyo mkweli kwani  alipokuwa CCM alinukuliwa akisema iwapo chama  hicho kitamteua Lowassa kugombea urais kwa  angekihama.

“Wakati wa mchakato wa kumtafuta mgombea urais Sumaye alisema hiki chama mkimpa Lowassa, atahama chama kwa kuwa tunamweshimu Sumaye hatukumpitisha Lowassa, lakini bado amehama na kwenda kumkumbatia fisadi,” alisema.


Alisema pale ambako mtu hazumgumzi ukweli anaitwa mwongo, hivyo kauli yake hiyo Sumaye hana tofauti na mwongo kwani katika kipindi cha miaka kumi iliyopita aliingia katika kinyang’anyiro cha urais na alifika tano bora, lakini kura hazikutosha badala yake zikatosha za Kikwete.

Alisema miaka kumi baadaye Sumaye ameingia katika kinyang’anyilo cha urais bahati mbaya hakuingia katika tano bora, lakini cha kushangaza anaanza kuishukutumu CCM kwamba ni chama kibaya 

“Mnaufahamu mchezo wa chandimu, ambao huchezwa na vijana tu na mzee akiingia akija anataka nini?alihoji na kuongeza;
“Sumaye kaingia katika mchezo huu wa chandimu mwenyewe, tutamsema.”
Mbali na Sumaye na Lowassa, wapinzani wengine waliohama CCM na kuiunga na upinzani ni wagunge waliomaliza muda wao wa Kahama, James Lembeli; Viti Maalum, Ester Bulaya; Arumeru Magharibi, Ole Medeye; Segerea, Dk. Makongoro Mahanga na wa Sikonge, Said Mkumba.

Wengine ni wenyeviti wa CCM wa mikoa ya Arusha, Onesmo Ole Nangole; Singida, Mgana Msindai na Shinyanga, Khamis Mgeja pamoja Mwenyekiti wa zamani wa Dar es Salaam, John Guninita.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top