Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UVCCM ZANZIBAR WASEMA CCM ITASHIKA DOLA OCTOBER

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) upande wa Zanzibar, umesema unaunga mkono kauli ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Kikwete kwamba CCM imejiandaa kushinda na kushika dola kwa sababu inao uzoefu wa kuongoza nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya UVCCM eneo la Gymkanna mjini hapa, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka alisema hotuba iliyotolewa na Mwenyekiti huyo wa CCM wakati wa kuwapokea wagombea wa chama hicho kuchukua fomu kutoka Tume ya Uchaguzi NEC katika ofisi ndogo za CCM Lumumba, imewavunja moyo wapinzani kwa kiasi kikubwa.

Shaka alisema CCM haibabaishwi na uamuzi wa kuhama kwa waliokuwa viongozi wake mbalimbali kwani tangu mwaka 1957 wakati wa harakati za kudai uhuru viongozi wa vyama vya TANU na ASP walikuwa wakihama vyama hivyo na kwenda upinzani.

“Tunaipongeza hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amewaambia ukweli wapinzani kwamba CCM imejiandaa kushinda katika uchaguzi mkuu kwa sababu inao viongozi safi wenye uwezo wa kuongoza dola,” alisema.


Aidha Shaka alitumia nafasi hiyo kusema kwamba UVCCM ipo imara huku ikiwaunga mkono wagombea wa CCM wa nafasi mbali mbali ikiwemo ya urais wa muungano.

Alisema umoja wa vijana katika mchakato wa wagombea wa nafasi ya urais wa muungano haukuwa na mgombea unayemuunga mkono, isipokuwa wanachama wenyewe walikuwa huru kutafuta mgombea wanayeona anafaa.

“Mchakato wa kuwania nafasi ya urais wa muungano umemalizika na sasa tunaye mgombea John Magufuli na mgombea mwenza Samia Suluhu. Hao ndiyo wagombea tunaowaunga mkono UVCCM katika harakati za kuwania urais wa muungano,” alisema.

Alisema mgombea aliyepitishwa na Mkutano Mkuu wa CCM, John Magufuli pamoja na mgombea mwenza Samia Suluhu ni viongozi wenye uwezo mkubwa wa kuongoza nchi ambao walipata kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top