Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WAFANYAKAZI WA TAZARA WALIPWE MISHAHARA YAO

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), hawajalipwa mishahara ya miezi mitatu kati ya miezi sita waliyokuwa wakiidai mamlaka hiyo.

Wafanyakazi hao hawajalipwa mishahara ya Januari, Juni na Julai, mwaka huu.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli Tanzania (TRAWU), Patrick Nyakeke, alisema baadhi ya wafanyakazi hawajalipwa mishahara ya kuanzia Januari hadi Mei, mwaka huu



“Wafanyakazi zaidi ya 1,500 bado hawajapewa mishahara ya miezi ya Januari, Juni na Julai huku wengine wakiwa wanaudai uongozi wa Tazara mishahara ya miezi mitano pamoja na malimbikizo mengine,” Nyakeke.
Aidha, alisema mishahara ya Januari na Juni, mwaka huu, utalipwa na Menejimenti ya Tazara na wa Julai mwaka huu, unatarajiwa kulipwa kupitia Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi ya 2015/16 iliyotengwa na serikali.

Hata hivyo, alisema baada ya wafanyakazi kuuhoji uongozi wa mamlaka hiyo kuhusu suala hilo, walielezwa kuwa watalipwa mishahara na malimbikizo ya fedha za likizo kupitia makusanyo ya Tazara ya Januari hadi Julai, mwaka huu.
Nyakeke alisema katika kukabiliana na changamoto hiyo, serikali imetenga Sh. bilioni 30 ili kuhakikisha wafanyakazi wanaondokana na adha ya kusotea mishahara.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top