Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

TUME YA TAIFA NEC YAWEKA HESHIMA YA KUJENGA TAIFA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeweka historia na kujenga heshima ya taifa kwa kuweza kuandikisha wananchi katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Mfumo wa BVR kwa mafanikio makubwa na kuyashangaza mataifa makubwa duniani.

Katika kufanikisha hilo, Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi (CUF) vimetajwa kuwashawishi wanachama na wafuasi wake kwa kiwango kikubwa kujiandikisha katika BVR.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kufuatilia Masuala ya Uchaguzi Tanzania (TEMCO), ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Kufuatilia Masuala ya Uchaguzi, Dk Benson Banna, alisema Dar es Salaam jana kuwa Nec inastahili pongezi kubwa kwa hatua hiyo.

Alisema utafiti uliofanywa na Temco kwa kupitia vituo 8,398 vya uandikishaji ambavyo ni asilimia 80.5 ya vituo vyote, umedhihirisha kuwa kazi hiyo ilifanyika kwa ukamilifu kwa wananchi wengi kupata nafasi ya kujiandikisha huku asilimia 64 ya vituo vikizidisha hadi muda wa kufunga katika kuwawezesha wananchi kujiandikisha.


Kwa hatua hiyo, Dk Banna alisema NEC imefuta aibu kwa Taifa, kutokana na mataifa mbalimbali ya nje kubeza uwezo wa nchi katika kufanikisha uandikishaji huo kabla ya kuanza na kwamba sasa kama Taifa, Tanzania imeanza kuonesha uwezo mkubwa wa kujitegemea katika uendeshaji wa shughuli za uchaguzi.

“Hili lazima nilisema wazi, ni aibu kwa mataifa makubwa kufadhili shughuli za uchaguzi maana kitendo hicho ni hatari kwa nchi kuweza kujiamulia mambo yake na kukuza demokrasia ya kweli, hivyo Nec wanastahili pongezi,”  Dk Banna.

Akielezea mlolongo mzima wa uandikishaji, mwanazuoni huyo alisema, Temco katika ufuatiliaji wake huo ilibaini kasoro mbalimbali ikiwemo fedha kutolewa kidogo na kwa kuchelewa hatua iliyofanya tarehe ya kuanza kwa uandikishaji kuchelewa na kusababisha usumbufu kwa wananchi.

Alisema pia wakati tathimini ya awali ilikuwa ni kuhitajika kwa visanduku vya BVR zaidi ya 15, 000, serikali ilikataa pendekezo hilo na kusema visanduku vinavyohitajika ni 14,000, lakini hata hivyo havikuweza kununuliwa badala yake vilinunuliwa visanduku 8,000 tofauti na ushauri wa Nec ambayo ilishauli kiwango cha chini kiwe visanduku 10,000

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top