Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

TUJIKUMBUSHE KIDOGO ENZI ZA MWALIMU JK. NYERERE

1. Idd Amini - Alipoivamia Tz. Mwalimu
alitamka tutampiga nduli. Na kweli Idd Amini alipigwa hadi akaikimbia nchi ya Uganda.

2. Kolimba - Alipotamka kuwa CCM imepoteza Dira na Mwelekeo, Mwalimu alimwita Dodoma
akamuuliza nani kakutuma useme hivyo? na huo Ndio ukawa mwisho wa Kolimba!

3. Samweli Sitta - Alipokuwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi UDSM aliongoza mgomo wa wanafunzi wenzake kudai siagi na maziwa!, Mwalimu aliibuka pale chuoni akamuuliza
Samweli Samweli kwenu mnakunywa maziwa
kweli?. Akamwambia lala chini, akamcharaza
bakora na mgomo ukaishia hapo hapo!.


4. Abdul Jumbe! - Alipotaka serikali tatu!,
Nyerere alimuuliza moja kujumlisha moja ni
ngapi?!. Jumbe akajibu ni mbili, Nyerere
akamwambia kama ni mbili mbona unataka
serikali tatu?! Huo ndio ukawa mwisho wa
Abdul Jumbe kuwa Rais wa Zanzibar!.

5. John Samwel Malecela - Ni baada ya taarifa
kuzagaa kuwa amebadili dini na jina ili apate
kuungwa mkono na nchi za kiislamu kugombea Urais mwaka 1995!. Nyerere alimwambia wee John wewe umeenda Arabuni mara moja umebadilisha jina sasa unaitwa Jumanne! Ukienda mara ya pili si utabadilisha kabila?! Huo ukawa mwisho wa ndoto zake kuwa Rais.

6. Edward Lowassa - Alipokodi ndege binafsi
ikampeleka hadi dodoma kwenye vikao vya
mchujo wa wagombea Urais kupitia CCM mwaka1995 alimpa lift Jakaya Kikwete, Nyerere alimuuliza mmekuja na Ndege dodoma pesa mmetoa wapi?! Jina la Lowassa likakatwa kabla ya vikao vya mchujo!.

Natamani Mwalimu Nyerere angekuwepo
Mpaka sasa kwenye uchaguzi wa mwaka 2015

HABARI NJEMA KWA WAZAZI NA WALIMU WA KINYEREZI TABATA SECONDARY SCHOOL

Mkuu wa taasisi ya Vodacom Foundation, Renatus Rwehikiza (kushoto) akishirikiana na wasimamizi wa mradi wa kompyuta mashuleni Meelis Kuuskler (katikati) pamoja na Julius Giabe kuunganisha kifaa cha kujifunzia masomo  kupitia kompyuta  katika shule ya sekondari Kinyerezi  ya Tabata jijini Dar es Salaam.  Mradi huo unaendeshwa na Learning In Sync  chini ya Vodacom Foundation.
Msimamizi wa mradi wa kompyuta mashuleni, Meelis Kuuskler (katikati)akiwafafanulia jambo Mkuu wa taasisi ya Vodacom Foundation, Renatus Rwehikiza (kushoto) na Julius Giabe kuhusu kifaa cha kujifunzia masomo  kupitia kompyuta  kilichokuwa kinaunganishwa katika shule ya sekondari Kinyerezi  ya Tabata jijini Dar es Salaam. Mradi huo unaendeshwa na Learning In Sync chini ya Vodacom Foundation.
Msimamizi wa mradi wa kompyuta mashuleni, Meelis Kuuskler akiunganisha kifaa maalum cha kuchajia kompyuta katika shule ya sekondari Kinyerezi  ya Tabata jijini Dar es Salaam.  Mradi huo unaendeshwa na Learning In Sync chini ya Vodacom Foundation utakabidhiwa hivi punde.

MTOTO WA KIKE AMUUA MAMA YAKE KISA KUFUA NGUO

Si jambo la kawaida kusikia mtoto kamuua mama yake ama mama kamuua mtoto wake, japo kwa miaka ya sasa matukio kama hayo yameshamiri kwa kiasi kikubwa sehemu mbalimbali duniani.

Tukio la mtoto kumuua mama yake leo limechukua headlines huko Zimbabwe baada ya kutokoea kutoelewana baina yao.

Kilichotokea ni kwamba binti wa miaka 17 alimuua mama yake kwa kumchoma moto baada kulazimishwa kufua nguo chafu, kitendo kilichomkasirisha na kufikia uamuzi huo.

Kabla ya kumuua mama yake kwa kumwagia mafuta kisha kumchoma moto, mama yake alimpiga kitendo kilichomuuzi binti huyo  na kufanya uamuzi huo mgumu.

Polisi wamemfungulia mtoto huyo mashtaka ya mauaji licha ya kupewa taarifa kuwa alikua akisumbuliwa na ugonjwa wa akili.

SHIRIKA LA ATCL LAONGEZA SAFARI MPAKA VISIWA VYA COMORO

Kwa sasa shirika hilo linatoa huduma zake kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Kigoma na Mtwara kila siku. Sambamba na kutoa huduma hizo hapa nchini, shirika hilo lina mpango mpya utakaoanza rasmi tarehe mosi ya mwezi Juni mwaka huu kwa kuongeza safari zake kuelekea visiwa vya Comoro hadi kufikia mara nane kwa wiki ikiwemo mara mbili siku za Alhamisi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Bw. Johnson Mfinanga alisema shirika hilo ndilo pekee linalotoa huduma ya safari za anga kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro huku akibainisha fursa za kibiashara zilizopo kati ya nchi hizi mbili jambo linalosababisha uwepo wa ongezeko la mahitaji ya huduma za ATCL.

Pia amewaasa watanzania hususan wakazi wa mtwara kuchangamkia fursa hizo kwa kuwa shirika hilo kwa sasa linatoa huduma zake kati ya Mtwara na visiwa vya Comoro kwa siku za Jumatano na Ijumaa kila wiki.
“Siku zote tumekuwa tukihakikisha kwamba tunabadilika kuendana na mahitaji ya wateja wetu.

Ni dhahiri kwamba katika kipindi hiki kuna hitaji kubwa la usafiri wa anga kuelekea visiwa vya Comoro kwa sababu za  kibiashara, mapumziko na sherehe mbalimbali, hivyo ATCL imejipanga kuchangamkia fursa hiyo,’’ alibainisha.


Akizungumzia ufanisi wa shirika hilo katika safari nyingine ikiwemo zile za Kigoma na Mtwara, Bw. Mfinanga alisema wamekuwa wakihudumia idadi kubwa ya abiria kutokana na ndege za shirika hilo kusafiri kwa mwendo kasi wa kuridhisha sambamba na huduma nzuri zinazotolewa kwa wateja wakati wa safari.

“Zaidi tunaamini kwamba huduma tunazozitoa kati ya Tanzania na Comoro zimekuwa zikichangia kuongeza ushirikiano baina ya nchi hizi mbili na tunaamini kuwa hata hili ongezeko la safari zetu kwenye mataifa haya mawili zitatoa fursa kwa wateja wetu kufaidi fursa zinazopatikana ndani ya nchi hizi,’’ aliongeza Bw. Mfinanga.

Kuhusu mpango wa shirika hilo kujipanua zaidi kihuduma, Bw. Mfinanga alisema:  “Ndege yetu aina ya De-Havilland Dash 8 Q300 kwa sasa inafanyiwa marekebisho makubwa kwenye karakana yetu iliyopo kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa  wa Julius Nyerere (JNIA) na itakapokamilika tutaendelea na huduma zetu katika mikoa ya Mwanza, Tabora, Kilimanjaro na Mbeya,’’

Bw. Mfinanga aliongeza kuwa kwa kufanya safari zake kuelekea visiwa hivyo shirika hilo limekuwa likiwezesha wateja wake kunufaika na fursa zilizopo kwenye visiwa hivyo huku pia akitoa wito kwa watanzania wengine kujitokeza kushiriki katika kuchangamkia fursa hizo.

BAADHI YA WABUNGE WAPINGA MASHINDANO YA MISS TANZANIA

Kwenye maswali na majibu ndani ya Kikao cha Bunge kibachoendelea Dodoma kuna vingi vinatokea, sasa hivi ni mijadala ya Bunge la Bajeti lakini ikifika wakati wa maswali na majibu kuna ishu nyingine huwa zinaibuliwa humohumo.

Leo niliinasa hii ya mashindano ya Miss Tanzania, kumbe kuna Wabunge hata hawayataki mashindano hayo kabisa !!
“Mimi sioni haja ya mashindano ya mamiss Tanzania.

Sisi tunaongozwa na maadili, unamuona mtoto wako anaenda kushindana mamiss, na ipo Kitaifa kabisa Mheshimiwa Fenela? Unamuona mtoto anavyodhalilishwa kwa sababu ya gari.. Jamani kama hamna gari bora mpande baiskeli au mpande pikipiki majumbani mwenu“>>>Mbunge Faida Mohamed Bakari.


“Sisi wazazi hasa wanawake hatutaki.. Serikali inashadadia umiss hasa mimi nasema huu umiss una faida gani katika nchi yetu? Mbona hawafanyi na wanaume?“>>> Faida Mohamed Bakari.

“Pamoja na yale mapungufu ambayo ameyagusia miss Tanzania ni suala la kisanii na yale mapungufu yalifanyiwa kazi na tukaruhusu Miss Tanzania ikaendelea“>>> Fenela Mukangala.

Ikafika time ya maswali kujibiwa >>> “Miss Tanzania inatengeneza ajira kwa warembo na pia inatangaza nchi na vivutio vya utalii ndani na nje ya nchi na pia inatoa burudani na elimu. Tunao warembo wenye akili nzuri wanaotumia nafasi ya Miss Tanzania kutengeneza ajira kwa vijana wengine“>>> Waziri Fenela Mukangala.

MASHINE ZA BVR ZASABABISHA WATU WENGI KUSHINDWA KUJIANDIKISHA

WATU wengi wameshindwa kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura kwa kutumia mashine za kisasa (BVR), licha ya kukaa vituoni muda mrefu.

SERIKALI YAKATAA BAJETI NA KUTAKA CAG ACHUNGUZWE

Serikali imekataa mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa shilingi bilioni 10, Raia Mwema limeambiwa.

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) ambayo CAG ndiyo Ofisa Mtendaji Mkuu wake ilikuwa imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 86 katika bajeti yake ya mwaka huu wa fedha (2015/2016) lakini sasa itapewa shilingi bilioni 76 tu.

Makato haya ni ya kihistoria kwa vile kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008, serikali haitakiwi kukata bajeti hiyo wakati ikiwa tayari imepitishwa kupitia utaratibu wake. Kwa maneno mengine, serikali imekiuka sheria katika suala hili.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya kibajeti ambayo gazeti hili limeyaona, ofisi hiyo ambayo bajeti yake inasomwa pamoja na ile ya Wizara ya Fedha, itakuwa na upungufu wa asilimia 12 ya kiwango kilichotakiwa.

Kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma, bajeti ya CAG hupangwa katika kikao maalumu baina ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Wizara ya Fedha na CAG.

Sheria hiyo inaeleza kwamba endapo bajeti itapitishwa kwenye kikao hicho, kwa kiwango chochote kile, inabidi serikali itoe kiasi hicho kama kilivyotakiwa bila kupunguza.

Kwa mujibu wa Mbunge wa Bariadi Mashariki na Mwenyekiti wa chama cha United Democratic (UDP), John Cheyo, utaratibu huo umewekwa ili kuhakikisha kwamba ofisi hiyo inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

“CAG anatakiwa aandae bajeti yake na kisha awasilishe mapendekezo yake. Baada ya mapendekezo hayo kujadiliwa katika kikao hicho, bajeti hupitishwa. Kiwango hicho hakitakiwi kupunguzwa kwa sababu kwenye kikao kuna Bunge na Serikali na ndiyo maana ya uwepo wao,” alisema Cheyo ambaye ni miongoni mwa wabunge wa Afrika wenye uelewa mkubwa wa masuala ya uwajibikaji.


Akizungumza na Raia Mwema kuhusu taarifa hizi za kupunguzwa kwa bajeti, Mwenyekiti mstaafu wa PAC, Zitto Kabwe, alisema katika kikao cha mwisho cha mapitio ya bajeti ya CAG, kiwango kilichopitishwa kilikuwa ni shilingi bilioni 86.

“Unasema wamepunguza zaidi kiwango? Basi watakuwa watu wa ajabu sana. Hii ni kwa sababu, mahitaji ya kibajeti ya CAG yalikuwa shilingi bilioni 94 lakini serikali ilijieleza kwamba ina hali ngumu na isingeweza kutoa kiasi hicho.

“Ndiyo tukakaa tena chini na kukubaliana kuhusu kiasi hicho cha shilingi bilioni 86. Sasa kama na hiyo wamepunguza tena basi hapo kuna tatizo. Hebu cheki ujue kama labda kuna kikao kimefanyika kati ya CAG, PAC na serikali kuhusu jambo hilo,” alisema Zitto ambaye sasa ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo.

Mmoja wa wajumbe wa PAC, Ismail Aden Rage, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini (CCM), alilithibitishia gazeti hili kwamba hakuna kikao kilichokaa kupunguza bajeti hiyo ya PAC. Juhudi za kumpata Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, kuzungumzia kuhusu suala hili hakifanikiwa kwa vile inaelezwa yuko nje ya nchi kikazi.

Gazeti hili limeambiwa kwamba hatua hii ya serikali inaweza kuwa na athari kubwa kwenye ofisi ya CAG kwa vile mwaka huu inatarajiwa kufanya kaguzi maalumu kwenye maeneo ya gesi na mafuta.

CAG imeamua kuingia katika eneo hilo la gesi na mafuta kwa lengo la kulisaidia taifa kubaini endapo mikataba ambayo nchi imeingia kwa sasa itakuwa na faida au la katika miaka ijayo.

CAG pia imeongeza mawanda yake ya ukaguzi kwa kukagua pia misamaha ya kodi na maeneo mengine kama vile bidhaa zinazodaiwa kusafirishwa kwenda nje ya nchi lakini zikipitia hapa nchini; mambo yote hayo yakihikitaji ongezeko la fedha. 

   Powerd by Raia Mwema. 

MY GREAT THUSDAY MESSAGE TO YOU IS HERE NOW

Our message to you is say that. Enjoy today and forget yesterday, also don't think about tomorrow because today is a gift, tomorrow is a secret and yesterday it will remain a history.

I wish you and your familly Nice day and God bless you. Every day visit Mutalemwa Blog for more news and other events in the world. 

TAARIFA KWA WASAFIRI WA MASAFA MAREFU

Kampeni ya zuia ajali sasa yazinduliwa, ambapo abiria watakiwa kutoa taarifa kwa kutumia namba maalum ili kuzuia mwendo kazi wa magari/mabasi yaendayo mikoani pamoja na kupunguza vifo vya abiria.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani  bwana Mohamed Mpinga ndiye alikuwa msemaji mkuu katika uzinduzi wa kampeni hii ya zuia ajali akishirikiana na Deogratius Rweyunga mkurugenzi wa radio one pamoja na  Bi. Rosalyin Mworia ambaye huyu ni mkuu wa Mawasiliano Vodacom Tanzania. 
Katika kampeni hii namba itakayotumiwa na abiria kutoa taarifa police juu ya gari ambalo linatembea kwa mwendokasi kinyume na matakwa ya abiria itakuwa ni 0800 757 575 Huduma hii ni kwa watumiaji wa simu mitandao yote, ambapo wewe abiria utatakiwa kutuma ujumbe mfupi kwa njia ya sms kwenda namba hiyo tajwa hapo juu. 

KONA YA SHERIA: RAIA KUKATAA KUKAMATWA NA ASKARI

Siku  zote  wananchi  wamekuwa    wakililalamikia jeshi  la polisi  kwa  namna  linavyoendesha  shughuli  zake hasa wakati  wa  ukamataji (arrest). Matumizi  ya  nguvu, ubabe    na  kutofuata  sheria    na  taratibu  maalum  limekuwa  ndio  tatizo  kubwa  kwa  wananchi  dhidi  ya  askari.
Sio  siri  askari wamekuwa  wakitumia  nguvu  na  ubabe  mno  katika  kuwakamata raia.  Hata  pale pasipo  na  haja  yoyote  ya  kutumia  nguvu    bado  wao  wamekuwa  wakilazimisha  nguvu  nyingi  hali  ambayo  hupelekea   vurugu , kuumizana  na  hata  mauaji. Mara  nyingi  unapochunguza  matukio   mbalimbali  ya  vurugu ambayo  huwahusisha raia  na polisi  utagundua  kwa haraka kuwa  ubabe    wa askari  ndio  uliopelekea  vurugu.  Basi  leo  nitaeleza nini  ufanye  askari  anapokiuka  taratibu   hasa  wakati  wa  kukamata/kuweka  chini ya ulinzi.
1.NINI  MAANA  YA  KUKAMATA ( ARREST ).

Sura  ya  20  Sheria  ya  Mwenendo  wa  Makosa  ya  Jinai  kama  ilivyofanyiwa  marekebisho  2002  ndiyo  sheria  inayotoa  mwongozo   wa  namna  na  jinsi  ya  kumkamata  mtu.  Pamoja  na  hayo sheria  hii  haikueleza   moja  kwa  moja  nini  maana  ya  kukamata.

Hata  hivyo  kutokana  na  miongozo mbalimbali  ya  kimahakama  ambayo  hutumika  kutafsiri  sheria  hii  tunaweza  kupata  tafsiri  ya  neno  kukamatwa  kwa  kusema  kuwa  ni  tendo  la  kumzuia  kwa  muda   raia  ambaye  inatuhumiwa  kwa  kosa  fulani,   ambalo  hufanywa  na  mamlaka  husika. Kwa tafsiri  hiyo  tendo la kuzuia  lazima  liwe    la  muda,  raia  anayekamatwa  lazima awe  ametuhumiwa, na pia  ukamataji  lazima  ufanywe  na  mamlaka.  Huo  ndio  utakuwa  ukamataji ( arrest).

2.  NANI  NA  NANI  WANARUHUSIWA  KUMKAMATA  RAIA ( ARREST ).

Kwanza  kifungu  cha  14  cha  Sheria  ya Mwenendo  wa  Makosa  ya  Jinai kinampa  mamlaka    askari  polisi kumkamata  au  kumweka  chini  ya  ulinzi   raia mtuhumiwa  . Hii ni  kusema  kuwa  mamlaka ya  kukamata aliyonayo  askari  yeyote  ameyapata  kutoka  kifungu  hiki.

Pili  kifungu  cha  18 cha  sheria  hiyohiyo   kinampa  hakimu  yeyote  mamlaka  ya  kumkamata  raia mtuhumiwa.  Mahakimu  wamegawanyika,   wapo  mahakimu  mahakama  za  mwanzo,  mahakimu mahakama  za  wilaya  na  mahakimu mahakama  za  hakimu  mkazi. Hawa wote  ni  mahakimu    na wanayo  mamlaka  ya  kumkamata  mtuhumiwa  kwa  mujibu  wa  kifungu  hiki.

Tatu  kifungu  cha  16 cha sheria  hiyohiyo  kinatoa  mamlaka  kwa raia yeyote  kumkamata mtu anayetenda  kosa. 

Hapa tofauti  ni  kuwa  mamlaka  ya  raia  kumkamata raia  mwenzake  ni  madogo  na huwezekana  pale tu ambapo  mtuhumiwa  ametenda  kosa  kubwa  na  pengine  kuna  wasiwasi  kuwa  anaweza  kutoroka  asipozuiliwa  haraka  na  kwa  muda  huo. 

Lakini  kama  mazingira  si  haya basi   raia    anatakiwa  kutoa  taarifa   polisi  ili  wao  wenyewe ndio  wafanye  kazi  hiyo.

3.  MATUMIZI   YA  NGUVU  HAYARUHUSIWI  WAKATI  WA  KUMKAMATA  RAIA.

Kifungu  cha 21 cha  sheria  hiyohiyo  kinakataza  kabisa  matumizi  ya nguvu  wakati  wa kumkamata  raia. Matumizi  ya  nguvu  ni  pamoja  na  kumpiga  raia, kumfunga  pingu, kumshika  suruali  kwa  kumningiza, kumtukana au  matumizi  yoyote  ya  lugha  chafu  na  kila  kitu  kinachofanana  na  hayo.

4. SHERIA  INAKURUHUSU  RAIA  KUKATAA KUKAMATWA   ASKARI  ANAPOKIUKA  TARATIBU.

Katika  kesi  ya  Nzige  Juma  vs R (1964) EA 107 uk 147  mahakama  ilisema  kuwa  ikiwa  mtu   atakamatwa   bila  kufuata  utaratibu  basi  mtu  huyo anaruhusiwa  kugomea  ukamataji  huo. Huu  ndio  uamuzi  wa  mahakama  na  kwa  mujibu  wa  sheria  uamuzi  wa  mahakama  ni sheria  na  hivyo  maamuzi  hayo  ni  sheria.

Kwa sheria  hii  nitoe  mwito  kwa  raia  kutowaonea  aibu  askari  polisi  wanaokiuka  taratibu  ikiwa  ni  pamoja  na  matumizi  ya  nguvu  katika  ukamataji  kwa  kuwagomea. Ieleweke  kuwa  kugoma  katika  hili  si  kuvunja  sheria  bali ni  kutekeleza sheria. Ni  haki    yako  kama  zilivyo  haki  zako  nyingine.

Na  kugoma  katika  hili  hakuwezi  kukuletea  shida  yoyote  na  hivyo  huna  haja  ya  kuwa  muoga.  Kumbuka  kama  wewe  mwenyewe  hautaweza  kulinda  haki  zako  hakuna  atakayelinda  haki  hizo  kwa  niaba  yako. 

Wewe   ndio  unatakiwa  kuwa  wa  kwanza  kulinda na  kusimamia  haki  zako  kwa  msimamo   usioyumba na  bila  woga  huku  ukiamini  kuwa  uko  salama  mbele ya  sheria. Chukua  hatua  sasa kwa  kukataa  na  kugomea  ukamataji  uliokiuka  taratibu.

NI HAKI YANGU KISHERIA KUPATA HABARI AU KUTOA HABARI

Mwaka juzi kulikuwa na sintofahamu kuhusu nani achinje iliyosababisha kifo cha mchungaji moja kanda ya ziwa. Wakati sarakasi hiyo ikiwachanganya watanzania, katibu wa Bunge Thomas Kashillah aliibuka na kusema, Bunge halitaoneshwa tena kwenye Runinga nchini.

Mjadala ukahama kutoka uchinjaji na kuwa Bunge kutooneshwa. Serikali ikafanikiwa, kombe likafunikwa na mwanaharamu akapita.
Mwaka 2013 mvua kubwa kuliko hii ya mwaka huu ilinyesha na kusababisha mamia ya watu kulala njiani na njaa wakiwa na watoto wao.

Njia nyingi za kuingia katikati ya mji wa Dar zilifungwa na maji na matokeo yake watu wakawa na hasira na serikali kutosimamia miundo mbinu vizuri jambo lililosababishia wao kupata madhara yale.

wakati hayo yakipamba kwenye vyombo vya habari ghafla tukaambiwa Makamu wa Rais, waziri magufuli na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam wameanguka na helikopta. kama kwaida Mjadala ukahama kwa walioanguka na helikopta.

Mwanaharamu akapita tena, Ikumbukwe kuwa hakuna kati ya wote walioanguka na helikopta aliyeenda hospitali wala picha ya helikopta iliyoanguka haikuonekana mpaka leo kama kaburi la Daudi Balali wa EPA iliyoibuliwa na Dr Slaa.

Wakati wa Bunge la katiba, Tundu Lissu na UKAWA waliibua madudu mengi kuhusu muungano hasa pale walipohoji lilipo kaburi la waasisi wa muungano amabao ni Hanga na wenzake.

Wakati mjadala huo ukishika kasi Dodoma, ghafla serikali ikaibuka na ugonjwa wa Dengue. Tukaambiwa wamekufa watu wawili mara watatu wakati malaria inaua zaidi ya watu watatu kila siku achilia mbali hao watatu hata kama ni zaidi ya watatu waliokufa mara moja na Dengue. Baada ya hoja ya Muungano kupita Dengue nayo ikayeyuka bila maelezo ya kutosha.

Je, watu wameshajiuliza kwanini magaidi feki wa amaboni walikuja wakati hoja ya ESCROW ikivuma? Tuliambiwa kuna askari wetu wamekufa. Je, akina nani kwa majina na walizikwa wapi na lini? Nani ameona picha hata moja ya askari wetu?

Mifano ya usanii huu wa serikali kuibua hoja ili kujilinda au kufunika udhaifu wake ni mingi sana.


Huko nyuma nilishaandika zaidi ya mifano kumi ya namna hii. Mifano hii michache inatosha kujenga hoja yangu. Kwa nini nimeyaeleza yote hayo?? Sababu ni moja tu ambayo ni kama ifuatavyo hapo chini.

Jana jioni nilimsikia kwenye ITV mwenyekiti wa MOAT ndugu Reginald Mengi akilalamikia serikali kutaka kupeleka mswada wa uhuru wa habari ambao moja ya kipengele chake kinavilazimisha vyombo vyote vya habari vikiwepo ITV, STAR TV, Chanel ten nk vijiunge na TBC saa mbili usiku kwa taarifa ya habari.

kwamba vyombo vingine (TV zingine/zote) havipaswi kuwa na taarifa yao ya habari wenyewe badala yake sheria itawalazimisha wajiunge na TBC. Je, hili linawezekana??

Mimi Nina wasi wasi nalo. Siamini kabisa nikirejea mifano tajwa hapo juu. Kwa maoni yangu taarifa hii imeletwa ili kubadilisha au kusahaulisha au kufunika mjadala wa ufisadi wa zaidi ya trilioni moja ulioibuliwa na Chadema baada ya kuchambua ripoti ya CAG. 

Kwa hiyo, taarifa hii imeletwa makusudi wakati bunge na vyombo vya habari vikijadili ufisadi huu wa serikali. Nijuavyo, Bungeni wakishamaliza taarifa hii ya TV zote kujiunga na TBC saa mbili jioni nayo itakuwa kama taarifa ya Dengue, hoja ya kashilillah ya Bunge kutooneshwa na TV au helikopta kuanguka bila majeruhi wala picha yake kuonekana.

Kama kicha cha habari hii kinavyosema "ni haki yangu kisheria kupata au kutoa habari" kwaiyo hoja hii ya kutunyima uhuru wa habari mimi siiungi mkono hata kidogo, maana iko kinyume na matakwa ya Watanzania na inakiuka haki za binadamu mpaka sasa. 

HII SI YA KUKOSA KUTOKA KWA MR.EDWARD LOWASSA

Waziri Mkuu aliejiuzulu Edward Lowassa amesafirisha wahariri wakuu wa vyombo vyote vya habari toka Dar es salaam na kufanya nao mkutano maalum leo nyumbani kwake mjini Dodoma. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema yafuatayo;

1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji. Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta. Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii.

2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo huku wengi wakiwa ni waliojeruhiwa katika serikali ya awamu ya nne akiwemo Aliekuwa DC Igunga Elibariki Kingu. 

Pia aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki ametangazwa rasmi kuwa Mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano katika timu ya kampeni ya Lowassa. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwani wao sio binadamu?

3. Lengo kuu atakaloanza nalo ni Elimu na sio Kilimo kwanza cha serikali ya JK. Amesema serikali ya JK ilikosea kuanza na kilimo na kuweka kando elimu. Ametangaza kuwa sera yake ni Elimu Kwanza.

4. Kuhusu pesa anasema anapata michango ya rafiki zake na ataendelea kupokea michango hii wakati wote wa harakati zake na haina madhara yotote.

5. Anasema hatahama CCM na asiyemtaka yeye CCM ndie aondoke ndani ya chama kwani yeye ana uhakika wa kupata nafasi kuwania urais.

6. Amesema hatalipa kisasi kwa lolote lililomtokea katika siasa. Amemwachia Mungu kwani yeye ni mcha Mungu.

7. Amesema Arusha itawaka moto tarehe 30 mwezi huu na kuwataka watanzania kutega sikio kwani ataanika kila jambo kuhusu mustakabali wa nchi hii na mipango yake ya kuiinua nchi kiuchumi katika miaka kumi ijayo.

Hayo ni kwa ufupi. Wahariri wakuu katika media zote kupitia Jukwaa la Wahariri walikuwepo, na Absalom Kibanda (New Habari) na Nevil Meena (Free Media) ndio walikuwa waratibu wakuu wa mkutano huu.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA

         Jamhuri ya muungano wa Tanzania
                 Tume ya taifa ya uchaguzi

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuviarifu vyama vyote vya siasa nchini pamoja na wananchi wote kwa ujumla kuwa kwa mamlaka iliyopewa kwa mujibu wa vifungu vya 35B(1), (3) (a), 37 (1) (a) na 46 (1) vya sheria ya taifa ya uchaguzi sura ya 343 ratiba ya uchaguzi mkuu itakuwa kama ifuatavyo:

Uteuzi wa wagombea uraisi, ubunge na madiwani itakuwa tarehe 21 August 2015

Kampeini za uchaguzi ni kuanzia tarehe 22 August mpaka tarehe 24 October 2015.

Siku ya kupiga kura ni tarehe 25 October 2015

Imetolewa leo tarehe 23 Mei 2015
Jaji wa rufaa (Mst) Damian Z. Lubuva
MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI.

WASHINDI WA TUZO ZA FILAM MWAKA 2015

Ijumaa ilikuwa siku ya fainali ya Tuzo za Watu kwa mwaka 2015, majina ya washindi yakaingia kwenye headlines mitandaoni na kwenye vyombo vya habari jana.. Jana hiyohiyo kingine kikubwa kwenye historia ya Filamu Tanzania nacho kikaingia kwenye headlines, ilikuwa usiku wa Tuzo za Filamu Tanzania 2015 kwa mara ya kwanza.

Shughuli yote ilikuwa pale Mwalimu Nyerere International Conference Center Dar es Salaam, na hapa naanza na list ya washindi waliopatikana:-

                 Habari kamili bofya hapa

Be actress in leading role- Irene Paul 
Best comedian- King Majuto 
Best supporting actress- Grace Mapunda
Best supporting actor (Male) – Tino Hisani Muya 

Best screenplay- Irene Sanga 
Tribute Award (Film Industry Support) – President Jakaya Kikwete 

Tribute Personality Award- Steven Kanumba 
Tribute Media- Zamaradi Mketema (Takeone Clouds TV) 

Life Time Achievement Award- Mzee Jangala 
Best Director- John Kalaghe.

MWIGULU NCHEMBA ATANGAZANIA YA KUGOMBEA URAIS

MWIGULU NCHEMBA ATANGAZANIA YA KUGOMBEA URAIS

May 22 Mwaka2015 kulikuwa na Headlines kubwa kuhusu ishu ya makada sita wa CCM kufunguliwa na Chama hicho baada ya kufungiwa kwa zaidi ya mwaka mmoja kutokana na ishu ya kuanza kampeni  za Urais mapema.
Leo kuna stori mpya kwenye siasa Tanzania  Mwigulu Nchemba ambaye ni Naibu Katibu Mkuu CCM Tanzania Bara katangaza kujivua cheo hicho na kuanza rasmi mchakato wa kugombea nafasi ya kuteuliwa kugombea Urais TZ kwa tiketi ya CCM.

ENEO LA 60 KWA 40 LINAUZWA MBAGALA CHAMAZI

Eneo la hatua 60 kwa 40 linauzwa, eneo hili liko Mbagala Chamanzi ni umbali wa dakika15 kutoka Mbagala rangi tatu stendi mpaka kulifikia eneo hilo.
Bei yake ni 3,500,000/= ukitoka chamazi magengeni unaenda chamazi kwa Marincha ndipo eneo lilipo wote mnakaribishwa sana.

Kwa yeyote mwenye kuhitaji eneo au shamba tuwasiliane kupitia namba 0659-919 292 au 0787-637 571 whats up pia napatikana. 
Mimi naitwa Mutalemwa .O. Juvenary.

ANGALIZO KWA MNAOTAKA KUGOMBEA OCTOBER 2015

Ndugu zangu leo napenda kutoa angalizo kwa watu wote wenyenia ya kugombea nafasi mbalimbali kwenye vyama mbalimbali vya siasa.

Uongozi nijambo jema, kwaiyo nivyema ukajiuliza maswali zaidi ya 70 kabla ya kugombea nafasi yeyote ile ndani ya chama chochote kile.

Ushauri wangu kwenu mnaotaka kugombea, watanzania wote tunataka kiongozi bora na sio bora kiongozi,  kwaiyo kama unatafuta nafasi ya uongozi kwa leongo la kujinufaisha wewe pamoja na familia yako ni vyema ukajiengue mapema kwenye list ya watakao gombea 2015

Wananchi tumechoka kuongea na viongozi wasio wasikivu tunachokitaka ndani ya uchaguzi wa mwaka huu ni utendajikazi nasio maneno meengi kuliko utekelezaji wa mipango.

Maendeleo chanya kwa nchi yeyote ile utokana na Serikali safi yenye mipango endelevu na Serikali yenye kusikiliza mawazo ya raia wake.

 Ndugu zangu tusilazimishe vitu pale isipowezekana,  kama wewe ukiona huwezi kufanya yale ambayo watanzania tunataka  nivyema ukafanye mambo yako mengine kuliko kulazimisha nafasi kwakutoa rushwa na mwisho wa siku unatufanyia madudu tu.

KURA ZAPIGWA JUU YA NDOA ZA JINSIA MOJA

Mwaka 1993 nchi ya Ireland ilikuwa moja ya mwisho mwisho kabisa katika nchi za Ulaya kuhalalisha ishu ya uhusiano wa jinsia moja.

mpaka leo ni miaka 22 imepita, wakati wowote huenda kukatokea headline nyingine kuhusu suala hilo, Bunge liliamua hii ishu washirikishwe watu wao pia na mpaka leo Jumamosi May 23 2015 tutasikia nini kimepitishwa.

Watu wa Ireland wanaendelea kupiga kura leo, kama kura nyingi zikisema YES, basi Katiba ya nchi hiyo itafanyiwa mabadiliko na ishu ya ndoa za watu wenye uhusiano wa jinsia moja zitakuwa zimeruhusiwa rasmi kwenye nchi hiyo!!

Kuna vitu vingi vinaendelea Ulaya, Marekani na nchi nyingine ikiwemo hii ya kuhalalisha ndoa na uhusiano wa jinsia moja, kwa Afrika ni nchi chache zimetoa msimamo.. Uganda ni moja ya nchi ambazo zilikataa kuhalalisha ndoa za aina hiyo.

Ireland VITEKampeni zimeendelea mtaani, migahawani kuna mabango yaliyoandikwa “YES EQUALITY” kuonesha watu kwamba wapo watu ambao wako tayari kuyakubali mabadiliko hayo.

IRELAND-master675
Mpaka sasa hivi ni nchi 19 duniani ambazo zimehalalisha ndoa za jinsia moja, kama majibu ya kura hizo za Ireland yataonesha watu wengi wamekubali basi jumla ya nchi  zitakuwa 20.

WATU WATANO WAKAMATWA NA VIUNGO VYA BINADAMU

Watu wapatao watano kutoka mkoani Shinyanga wametiwa mbaroni kwa kosa la kujihusisha na biashara haramu ya viungo vya binadamu.

Bwana Justus Kamugisha ambaye ni kamanda wa police mkoani Shinyanga amesema mnamo tarehe 21st May 2015 majira ya saa saba mchana huko kahama mjini katika hotel maarufu kama Maji hotel walifanikiwa kuwakamata watu watano ambao majina yao nikama ifuatavyo.

1. Bahati kirungu umri wake ni miaka 56 kabila msukuma pia ni mwalimu wa shule ya msingi Katunguru iliyopo tarafa ya msalala wilaya ya kahama.

 2. Muoja John umri wake ni miaka 24 kabila msukuma yeye ni mkulima nanimkazi wa isagei wilayani nzega.

3. Bilia Busana umri wake ni miaka 39 kabila msukuma yeye ni mkazi wa moga Nzega

4. Shija Makandi (mwanamke) umri wake ni miaka 60 kabila msukuma na mkazi wa lusagerwa wilayani nzega Tabora

5. Regina Kashinje umri wake ni miaka 40 kabila msukuma huyu ni mkulima pia ni mkazi wa insagee wilayani nzega mkoani tabora.

Watu hawa walikamatwa wakiwa kwenye harakati za kuuza viungo hivi vya binadamu kwa mtu mmoja kwa thamani ya Tsh 600 millions. Endelea kutembelea Mutalemwa Blog. 

KITUO CHA POLICE KENYA CHASHINDA TUZO YA USAFI

Kituo cha Voi kimeibuka mshindi bora kwa kupata tuzo ya usafi kati ya vituo vyote vilivyoko nchini humo.

Kamanda Richard Bitonga ambaye ni mkuu wa kaunti, Taita Taveta amesema wamekuwa wakitaidi sana kuimalisha usafi kwenye maeneo ya kituo chao cha kazi kwa mwaka mmoja uliopita.

Jambo la kushangaza kwenye kituo hicho ni pale tulipoona wahalifu wakiwa wameketi huku wakisoma gazeti huku vyoo vyao vikiwa katika hali ya usafi wa hali yajuu sana na vinavutia.

Kiujumla muonekano pamoja na mpangilio wa kituoni hapo ukovizuri sana maana mpaka kuna viti vya watu kuketi waliokuja kuwaona ndugu zao kituoni hapo walioletwa kama wahalifu pamoja na mpangilio mzuri wa files.
Joshua Lukayi ambaye ni Mkuu wa police Voi yeye anasisitiza sana juu ya usafi kwenye maeneo yate ya police stations maana bila ya usafi wahalifu watakuwa katika hali mbaya amabayo inaweza kuwasababishia magonjwa pamoja na wao kama police wanao hudumia maali hapo. 

TAIFA STARS MMETUDHALILISHA SANA JAMANI

Soka ya Tanzania imeanza safari ya kasi kwa kudidimia, baada ya Taifa Stars kuonesha vituko ugenini kwa kufungwa na timu ndogo.

Japokuwa kocha Mart Nooij alichagua sura ‘zile zile’ pengine kwa kigezo cha uzoefu kwenye michuano ya kimataifa, Stars waliambuliwa kipigo cha pili na kutupwa nje ya michuano hiyo waliyokuwa waalikwa.

Stars walioanza Jumatatu kwa kupigwa 1-0 kutoka kwa Swaziland, moja ya mataifa madogo Afrika, Jumatano waliongezewa dozi kama mgonjwa anayezidiwa homa, kwa kufungwa 2-0 na Madagascar.

Wachezaji wazuri na chipukizi waliong’ara kwenye Ligi Kuu ya Tanzania iliyomalizika hivi karibuni hawakupewa nafasi kwenye michuano hiyo, badala yake waliitwa walizoeleka pamoja na sura chache mpya.

Kocha wa zamani wa Stars, ambaye amekuwa mwajiriwa katika Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk Mshindo Msolla amenukuliwa akisema kiwango cha soka cha timu hiyo kinasikitisha na kuonesha kwamba hatua zinatakiwa kumhusisha pia kocha Nooij.

Ijumaa hii, Stars watashuka dimbani kucheza dhidi ya Lesotho katika mechi ya kukamilisha ratiba, ambapo hata wakishinda watajiandaa kurudi.

Maelezo ya kocha kabla ya kuondoka ni kwamba wachezaji hao na waliobaki kwa matatizo mbalimbali wataanza kambi kujiandaa na mechi za kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (CHAN), lakini wadau wanaona iwapo busara ingetumika timu ingevunjwa na kuundwa upya.

Wakati Tanzania ikiwa na idadi ya watu milioni 49.25, Swaziland walioanza kuchafua nyota ya Stars wana watu milioni 1,106,000 (milioni moja na laki moja na elfu sita).

Swaziland washika nafasi ya 176 katika ubora wa kiwango cha soka kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), hawajapata kufuzu kwa Kombe la Dunia wala CHAN na wanafundishwa na kocha Harris ‘Madze’ Bulunga, raia wa Swaziland.

Madagascar wanashika nafasi ya 150 kwa kiwango cha soka duniani na wanafundishwa na Franck Rajaonarisamba wa huko huko Madagascar. Hii ni nchi yenye watu 22,005,222, pungufu kabisa ya nusu ya Watanzania.

Tanzania kwa mujibu wa takwimu za Fifa, kwa sasa inashika nafasi ya 107. Ilipata kupanda hadi ya 65 Februari 1995 na kushuka hadi ya 175 Oktoba 2005.

Maneno ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi ya Tanzania kuwa sawa na kichwa cha mwendawazimu ambacho kila mmoja hujaribu kunyoa, yanatakiwa sasa kujirudia rudia vichwani mwa viongozi wa soka wa ngazi mbalimbali.

Kwa namna ya pekee Shirikisho la Soka (TFF), benchi la ufundi la timu na wachezaji wenyewe, ili wabadili mwelekeo kabla hali haijawa mbaya. Katika makundi ya CHAN Tanzania wamepangwa na Nigeria, Misri na Chad. Kwa hali ilivyo, hata Chad wangeweza kuwafunga Tanzania. Ni wakati wa mabadiliko sasa.

VIFO VYA WAKIMBIZI KUTOKA BURUNDI KUFIKIA 40

Baada ya vifo vya wakimbizi kutoka Burundi kufikia 40, Serikali imelazimika kuongeza idadi ya kambi za wakimbizi ili kupunguza msongamano Nyarugusu.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga alisema jana kuwa hali iliyopo kwenye Kambi ya Nyarugusu siyo ya kuridhisha, maana mpaka sasa wagonjwa wa kipindupindu wanafikia 7429 na watoto wenye utapiamro idadi yao ikizidi kuongezeka.

Alisema wakimbizi waliopo kambini ni 29,145 na ambao hawajaingia wakiwa katika uwanja wa Lake Tanganyika ni 4,729

Nantanga alisema Serikali imelazimika kuongeza kambi moja katika eneo hilo litakaloitwa Nyarugusu 2.

Alisema wameshaanza kuwahamisha wakimbizi kutoka kwenye uwanja huo chini ya uangalizi mkali.

“Tumebaini wakimbizi wanabanana sana kwenye kambi moja, kuna wengine wajawazito, wagonjwa wa kipindupindu, hivyo tumelazimika kuongeza kambi ya pili,” alisema Nantanga.

Alisema Serikali inashirikiana na Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR) kuhakikisha huduma za chakula na matibabu zinapatikana.

Nantanga alisema kuhusu suala la ulinzi, Serikali imejipanga kuhakikisha hakuna uhalifu wowote utakaotokea kambini hapo.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Steven Kebwe alisema wanashirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhakikisha wanapeleka timu ya wataalamu maeneo ya Kagunga na Nyarugusu kufanya tathmini na kutoa elimu ya afya.

KERO MPYA YAJITOKEZA KWA ABILIA WA MBAGALA

Na Happyness L. Michael, ikiwa leo ni siku ya ijumaa ya tarehe 22/5/2015 maudhi mapya yamejitokeza kwa abilia waishio maeneo ya Mbagala rangi tatu,  mtoni mtongani, kwa Azizi Ally, Mission, Kipati, zakhiem, kizuiani nk.

Kero yenyewe inamuhusu kondakta na dreva wa gari lenye usajiri wa namba T447 CTL linalotoa huduma kati ya mbagala to posta via Kilwa road, ambapo inadaiwa kondakta wa gari hilo amejijengea tabia ya kutorudisha nauri kwa baadhi ya abilia huku dreva akiwa kimya.

Pia abilia hao waishio mbagala wamesema gari hilo linautaratibu wake tofauti na magari yote yanayotoa huduma ya kusafirisha abilia kutoka mbagala rangi tatu to Posta, maana magari mengine hutoza bei ya Tsh450 hadi 700, wakati gari tajwa hapo juu hutoza bei ya Tsh 450 hadi 800 pindi uzungukapo na gari hilo

Leo katika tukio lililowafanya abilia mpaka wakaamua kupaza sauti zao nipale ambapo moja ya abilia alipotaka kushuka katika kituo cha bandari ya kwanza huku akidai Tsh 100 kama change yake, ndipo kondakta alianza kusema hana change na kumpeleka mwanadada huyo mpaka kituo cha bandari yapili, tukio hili limetokea leo mda wa asubuhi.

Kiukweli vitendokama hivi vinaumiza sana maana mtu anapokuwa ameshapiga hesabu zake kisha anakuja kuvurugiwa inamuweka katika wakati mgumu muhusika, kwaiyo kama mmiriki wa gari tajwa hapo juu umepata habari hii 

Tafadhali tunakuomba ufanye mabadiriko kwenye gari lako maana bila ya kufanya hivyo kuna mawili, 1.waweza kulipoteza gari lako au 2.kusabisha vifo visivyotarajiwa kati ya abilia na kondakta/dreva kutokana na ugonvi.

WAFAHAMU WASHINDI WA KTMA 2015 KUPITIA HAPA

washindi wa vipengele mbalimbali katika tuzo za Kili Tanzania Music Awards 2015 (KTMA) wakitarajiwa kujulikana Juni 13 katika hafla ya ugawaji wa tuzo hizo, hakuna msanii atakayevunja rekodi ya Abdul Nassib (Diamond) kwa kuwa hakuna aliyeko katika vipengele saba.

Tuzo hizo zilizoanza mwaka 2000 hadi leo zina rekodi iliyowekwa na Diamond ya kunyakua tuzo saba mwaka jana, mwaka huu amekutana na mchuano mkali baada ya kuingia katika vipengele sita akichuana na Ali Kiba na Juma Jux ambao nao wanataka kuweka rekodi ya kihistoria ya kunyakua tuzo nyingi katika shindano hilo.

Mbali na Diamond kuvunja rekodi msimu uliopita, Bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa pia iliwahi kunyakua tuzo tano mwaka 2013, huku wasanii, Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz wakinyakua tuzo tatu kila mmoja.

Kwa mwaka huu katika shindano hilo lililopo chini ya udhamini wa Kampuni ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro, yanaonyesha kuvutia hiyo rekodi mpya itakayoshindanisha wasanii hao wa Bongo Fleva ambao wanatamba kuwa na mashabiki wengi kwa sasa.

Pia wasanii wa muziki wa aina nyingine ukiwemo taarabu na nyimbo za asili huwa zikinyakua tuzo nyingi kutokana na muziki wao kuwa na mvuto mkubwa kwa ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa mkuu wa matukio wa Baraza la Sanaa Tanzania (Basata), Kurwijira Maregesi, zoezi rasmi la upigwaji wa kura litafungwa Juni 5 baada ya kufunguliwa Mei 4 na mwaka huu hivyo kila msanii aliyepo katika kipengele chochote awashawishi mashabiki wake wampigie kura zaidi wawezavyo ili aibuke mshindi.

Basata mwaka huu wameendelea kusimamia vema uchaguzi wa nyimbo kwa kufuata maudhui ya wimbo huku wakiachana na nyimbo zenye maneno yasiyo na mafunzo zaidi ya kutumia tafsida kuhalalisha lugha chafu. 

Mwaka jana ilizuia wimbo wa Jux na Snura Majanga kutokana na kutokuwa na kukiuka maadili katika video za nyimbo zao na mwaka huu wamefanya hivyo kwa nyimbo zisizostahili ubaya uko wapi?

Jux aliyezuiwa wimbo wake mwaka jana, mwaka huu ameingia katika vipengele sita, hayo ni mabadiliko inaonyesha amekubali makosa yake na ameyafanyia kazi na sasa wananchi wanapiga kura kwa kutumia mfumo wa website ya www.ktma.co.tz, WhatsApp na njia ya SMS.

Tuzo hizi zinazosimamiwa na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa muziki, kwa kiasi kikubwa zimefanikiwa kuleta mageuzi katika fani ya muziki lakini pia zinatakiwa kufanyiwa marekebisho katika vipengele hivi;

kwanza zitoe elimu zaidi ili ziondoe dhana potofu ya kuitwa mradi wa wachache ili baadhi ya wanaozisusia wasisuse ili ziongeze mvuto.

UKARABATI WA JENGO LA WETE KUGALIMU TSH 370 MILLIONS

Jumla ya Shl. Milioni 370 za kitanzania, zinahitajika kwa ajili ya Ukarabati wa Jengo la Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi ulipo Wete Kisiwani Pemba.


Kupatikana kwa Pesa hizo kutaiwezesha Serikali kuweka Samani na Vifaa vya kisasa kwa ajili ya kuendeleza Shughuli za Baraza la Wawakilishi Kisiwani Pemba kama ilivyokuwa mwanzoni.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud wakati akijibu Swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Saleh Nassor Juma katika Kikao cha Bajeti kinachoendelea Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Amesema miaka ya nyuma kulikuwa na utaratibu wa kufanyika Vikao vya Baraza la Wawakilishi kwa mpangilio maalum baina ya Kisiwa cha Unguja na Pemba lakini kwa sasa utaratibu huo umeondoka.
Amesema kukosekana kwa Vikao vya Baraza la Wawakilishi Pemba kumetokana na Ukumbi wa Baraza hilo uliopo Pemba kukosa Viwango vinavyohitajika.

Hata hivyo Waziri Aboud amesema nchi nyingi Duniani Vikao vya Baraza au Bunge huwa vinafanyika pahala pamoja tu jambo ambalo ni tofauti na Zanzibar.

Amesema licha ya tofauti hiyo bado Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaona ni vyema kuendeleza utamaduni wa kufanya Vikao vyake Unguja na Pemba hasa pale Ukumbi huo Utakapomaliza matengenezo yake.

HOFU YA MABOMU YATANDA KWA WAKAZI WA NJOMBE

Wakazi wa Mji wa Njombe, juzi walikumbwa na taharuki kutokana na mabomu ya machozi yaliyopigwa na Polisi

kwa lengo la kutawanya waandamanaji waliokuwa wanapinga mauaji ya mkazi mmoja anayedaiwa kupigwa risasi na askari na mwingine kujeruhiwa.

LEO NI KUMBUKUMBU YA KUZAMA KWA MV BUKOBA

Itakumbukwa kuwa siku kama ya leo MAY 21 mwaka 1996 ilikuwa ni siku ya majonzi makubwa sana kwa wana bukoba pamoja na watanzania wote kwa ujumla wake.

Stori kubwa ni kuhusu ishu ya kumbukumbu ya kuzama kwa meli ya MV Bukoba ambayo ilipata ajali mwaka 1996. Ndugu zangu, naomba kuchukua nafasi hii kuwapapole wale wote mliopoteza ndugu/jamaa au marafiki zenu. Tuzidi kuwaombea kwa Mungu napia sara zetu zitawafikia huko walipo mbinguni.

Wote tuseme Amen

MADA JUU YA NISHATI ENDELEVU KWA WOTE

Kutoka New York Marekani. Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Charles Kitwanga ( Mb), ni miongoni mwa mawaziri kutoka mataifa mbalimbali duniani wanaohudhuria mkutano wa kila mwaka kuhusu Nishati Endelevu kwa Wote (SE4All)

Mkutano huu unafanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, ambao siku ya jumatano mawaziri wameanza kujadili na kubadilisha uzefu kuhusu eneo hilo la nishati ambalo linaelezwa kuwa ni muhimu kwa maendeleo endelevu kijamii, kiuchumi na mazingira.

Mhe. Kitwanga ambaye anatarajiwa kuelezea msimamo wa Tanzania katika eneo hili la nishati endelevu siku ya alhamisi ( leo). Ameambatana na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Ngosi Mwihava pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati na Madini.

Akifungua mkutano wa Mawaziri, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson, amesema mkutano huo wa mawaziri na ambao ulitanguliwa na mijadala mbalimbali iliyofanyika nje na Makao Makuu, kuwa Mawaziri hao wanakutana katika wakati muafaka na hasa kwa kuzingatia kwamba mwaka huu wa 2015 ni muhimu sana kwa Umoja wa Mataifa na Nchi wanachama.

Akasema , viongozi wa dunia wametambua kwamba, njia sahihi ya kufikia mafanikio ya pamoja sasa na baadaye ni kuwa na uwiano uliosawa kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Naibu Katibu Mkuu, ameongeza kuwa kwa muda mrefu, jumuiya ya kimataifa imekuwa ikifuata njia za ukuaji wa pamoja pasipo kuheshimu mipaka baina ya mazingira ya dunia na haja ya kuishi kwa kuzingatia uwiano bora na viumbe wengine. 
Na kwa sababu hiyo, Bw. Jan Eliasson amewaeleza Mawaziri hao na wadau wengine wanaoshiriki mkutano huu kuwa, mwaka huu Jumuiya ya Kimataifa itakuwa na mikutano mitatu muhimu na ambayo itatoa mwelekeo mpya na ajenda mpya kuhusu maendeleo endelevu kwa wote.

Ameitaja mkutano hiyo mitatu na muhimu kuwa ni  Mkutano utakaofanyika mwezi Julai Addis Ababa, Ethiopia, mkutano ambao dhumuni lake kuu litakuwa ni kujadili na kukubaliana kuhusu mfumo wa fedha kwaajili ya utekelezaji wa maendeleo endelevu. 

Mkutano wa pili ambao ameutaja ni ule utakofanyika mwezi Septemba hapa New York, mkutano ambao Wakuu wa Nchi na Serikali watapitisha ajenda na malengo ya Maendeleo Endelevu baada ya 2015.

Aidha mkutano wa tatu ni ule utakaofanyika Jijini Paris, Ufaransa mwezi Desemba, ambapo makubaliano yanatarajiwa kufikia kuhusu mabadiliko ya Tabia Nchi.

Akizungumzia kuhusu nishati endelevu, Naibu Katibu Mkuu, ameeleza kwamba Nishati endelevu ndio msingi mkuu wa maendeleo na mageuzi katika sekta zote ziwe za viwanda, kilimo au ustawi wa jamiii na kuongeza kuwa katika dunia ya sasa ambayo inakabiliwa na changamoto nyingi, ufumbuzi wa changamoto hizo unahitaji ushirikiano wa pamoja baina ya serikali, sekta binfasi na makundi mengine ya kijamii 

Akasisitiza kuwa mpango kuhusu nishati endelevu kwa wote, umeonyesha kwamba ushirikiano miongoni wa wadau mbalimbali umeweza kusaidia kusukuma mbele ajenda hiyo ya nishati endelevu kwa wote.

Ameongeza kuwa kizazi kijacho kitakichangaa kizazi cha sasa kwa kutoweka mipango madhubuti kwaajili yao.

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Taifa akabainisha pia kwamba, Nchi zaidi ya 80 zinazoendelea zimejiunga mpango huo wa nishati endelevu kwa wote.

Na kwamba Ahadi zenye thamani ya mabilioni ya dola tayari zimepatikana. Ripoti kuhusu kuhusu mchakato wa kuelekea nishati endelevu ambayo ilitolewa kwa washiriki wa mkutano huo Mei 18, inaonyesha kwamba watu 1.1 bilioni duniani kote wanaishi bila nishati ya umeme.

Huku karibu wengine 3 bilioni wakiendelea kupika kwa kutumia nishati ambazo si salama kwao na mazingira, nishati hizo ni pamoja na mkaa, kuni, mafuta ya taa na samadi.

TAARIFA JUU YA VIONGOZI WA CUF WALIOZALILISHWA

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu Mhe. Bahame Nyanduga akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya uchunguzi wa tuhuma dhidi ya Jeshi la Polisi za kuwapiga na kuwazalilisha Viongozi na Wafuasi wa CUF huko Mtoni Mtongani Temeke, Dar es sa Salaam.

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imelaani vitendo vya uzalilishaji vilivyofanywa kwa Viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Januari 27 mwaka huu (2015) wakati wa maandamano ya Chama hicho Mtoni Mtongani Wilaya ya Temeke.


Akizungumza na waandishi wa habari jana (Mei 20, 2015) Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Bahame Nanduga, alisema uchunguzi wa tukio hilo umekamilika kwa kuzingatia kifungu cha 130[1][c],[f] na [g] cha katiba ya jamhuri ya Tanzania.

Aidha aliongeza kuwa sheria nyingine zilizotumika kuchunguza tukio hilo ni pamoja na kifungu cha 6[1][c]na [g] vifungu 15[1][a] na 28[1][a],[b] na f vya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Na.7 ya mwaka 2001, sheria ya polisi na polisi wasaidizi, sura 322, na sheria ya vyama vya siasa, sura 258

Nyanduga alisema Tume yake imebaini ukikwaji mkubwa wa haki za binadamu waliofanyiwa viongozi na wanachama chama cha wananchi CUF katika maandamano yao ya shughuli za kichama, hivyo Tume ilibaini kuwa jeshi la polisi lilitumia nguvu kupita kiasi, ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na udhalilishaji wa wanachama wawili wa kike wa CUF.

“Tume imetoa mapendekezo kwa jeshi la polisi  kuzingatia kanuni, sheria, haki za binadamu na misingi ya utawala bora katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku na kuhakikisha maafisa wake wanajipanga vyema katika kuratibu na kusimamia utekelezaji wa operesheni zake” alisema Nyanduga

Kwa mujibu wa Nyanduga tume hiyo pia imewataka Viongozi na wanachama wa CUF kutafuta namna ya kuboresha mahusiano na jeshi la polisi, ili kuondoa mivutano isiyo na tija.

Tume imepanga kuitisha mafunzo na mikutano mbalimbali kwa kushirikiana na vyama vya siasa,Tume ya Taifa ya Uchaguzi [NEC], pamoja na vyombo vya Ulinzi na Usalama ikiwemo Jeshi la Polisi na Magereza, msajili wa vyama vya siasa, na asasi za kiraia ili kupanga taratibu zote katika kujua haki za binadamu na utawala bora.

HABARI NJEMA KWA WATUMIAJI WA MTANDAO WA VODACOM

Watumiaji milioni 13 wa mtandao wa simu za mkononi kuanzia leo wataweza kuperuzi internet inayofikia MB100 kwa masaa mawili bure kuanzia saa 12 alfajiri hadi saa 2 asubuhi kutokana na ofa inayojulikana kama”Good Morning Tanzania” inayotolewa na Vodacom Tanzania.

Promosheni hii imeanzishwa kutokana na kuonenakana kuwepo kwa mahitaji makubwa ya matumizi ya data katika kupata  taarifa kupitia mtandao wa intaneti.

Vodacom Tanzania siku zote imekuwa mstari wa mbele kubuni huduma zinazoendana na matakwa ya wateja wake na kuwarahisishia maisha katika nyanja ya elimu,afya,Kilimo,burudani,huduma za kibenki na huduma nyinginezo  za kurahisisha biashara mbalimbali.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hii leo,Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Kampuni hiyo Kelvin Twissa amesema “Kupitia promosheni hii ya ”Good Morning Tanzania” Vodacom tutawaunganisha wateja wetu na sehemu nyingine za dunia bure kila siku.

Ofa hii  inawawezesha wateja wetu kufanya shughuli zao mapema bure kupitia mtandao wa intaneti ikiwemo kuwasiliana na marafiki,kupata habari mbalimbali za kitaifa na kimataifa na matumizi mengineyo mengi yanayoweza kufanyika kupitia kwenye mtandao wa internet.

Promosheni ya ”Good Morning Tanzania”imeadaliwa mahususi kukidhi matakwa ya wateja wa Vodacom ili kuwarahisishia maisha na watanzania wametakiwa kujiunga na familia ya Vodacom  waweze kutumia  fursa hii kupata wakipendacho kupitia teknolojia ya simu  za mkononi.

Ili kupata huduma hii mteja anachotakiwa kufanya ni kupiga namba *149*01# ambapo atapata maelekezo zaidi na kuanza kupakua na kuperuzi intaneti na kuweza kupata kwa urahisi anachohitaji akiwa ametulia nyumbani kwake.

MAREKANI YABAINI KASORO KWENYE MAGARI

Takriban magari milioni thelathini na nne 34,000,000 yanatarajiwa kurejeshwa viwandani nchini Marekani kufuatia hitilafu ya kiufundi kwenye mifuko ya hewa ya usalama.

Kampuni inayotengeneza mifuko ya hewa ya usalama ya magari inachukua hatua hiyo baada ya malalamiko kuwa hitilafu ya muundo wake imesababisha vifo vya watu wapatao watano.

Tukio hili la urejeshwaji wa magari viwandani kutokana na kasoro za kiufundi ni kubwa zaidi kuwahi kutokea nchini Marekani. Kampuni ya kutengeneza vifaa vya magari ya Japan, Takata, imekiri mifuko ya hewa kulinda usalama wa watumiaji wa magari kuwa na kasoro.

Baadhi ya mifuko hiyo ya hewa imepasuka kwa nguvu kupita kiasi na kusababisha kurusha vipande vya chuma kwa madereva na abiria wanaokaa viti vya mbele.

Waziri wa Usafirishaji wa Marekani, Anthony Foxx, ametangaza kurejeshwa kwa magari yenye hitilafu ya mfumo huo kote nchini humo.
Bwana Foxx amesema urejeshwaji wa magari hayo ni kazi kubwa.

Tangazo hilo limetolewa na Utawala wa usalama wa taifa nchini Marekani katika barabara Kuu baada ya mazungumzo marefu na kampuni ya Takata.

Magari yanayorejeshwa yanahusu kampuni kumi na moja za kutengeneza magari zikiwemo za Honda, Toyota na Nissan.

Urejeshwaji viwandani kwa magari mapya hufanyika baada ya kugundulika hitilafu lolote la kiufundi linaloweza kuhatarisha usalama wa watumiaji wa magari hayo.
Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top