Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

VIFO VYA WAKIMBIZI KUTOKA BURUNDI KUFIKIA 40

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Baada ya vifo vya wakimbizi kutoka Burundi kufikia 40, Serikali imelazimika kuongeza idadi ya kambi za wakimbizi ili kupunguza msongamano Nyarugusu.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga alisema jana kuwa hali iliyopo kwenye Kambi ya Nyarugusu siyo ya kuridhisha, maana mpaka sasa wagonjwa wa kipindupindu wanafikia 7429 na watoto wenye utapiamro idadi yao ikizidi kuongezeka.

Alisema wakimbizi waliopo kambini ni 29,145 na ambao hawajaingia wakiwa katika uwanja wa Lake Tanganyika ni 4,729

Nantanga alisema Serikali imelazimika kuongeza kambi moja katika eneo hilo litakaloitwa Nyarugusu 2.

Alisema wameshaanza kuwahamisha wakimbizi kutoka kwenye uwanja huo chini ya uangalizi mkali.

“Tumebaini wakimbizi wanabanana sana kwenye kambi moja, kuna wengine wajawazito, wagonjwa wa kipindupindu, hivyo tumelazimika kuongeza kambi ya pili,” alisema Nantanga.

Alisema Serikali inashirikiana na Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR) kuhakikisha huduma za chakula na matibabu zinapatikana.

Nantanga alisema kuhusu suala la ulinzi, Serikali imejipanga kuhakikisha hakuna uhalifu wowote utakaotokea kambini hapo.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Steven Kebwe alisema wanashirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhakikisha wanapeleka timu ya wataalamu maeneo ya Kagunga na Nyarugusu kufanya tathmini na kutoa elimu ya afya.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top