Takriban watu 100 wameuawa baada ya ndege ya uchukuzi wa kijeshi ya Indonesia kuanguka mapema leo katika maeneo yenye makazi ya watu huko Medan Sumatra.
Maafisa wa kijeshi wanasema kuwa tayari miili 49 imepatikana katika eneo la ajali.
Habari Mchanganyiko
Takriban watu 100 wameuawa baada ya ndege ya uchukuzi wa kijeshi ya Indonesia kuanguka mapema leo katika maeneo yenye makazi ya watu huko Medan Sumatra.
Maafisa wa kijeshi wanasema kuwa tayari miili 49 imepatikana katika eneo la ajali.
Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Brandon Cohen, mkazi wa mji wa Los Angeles huko Marekani ametoa kali ya mwaka baada ya kuamua kuvaa viatu vya kike ili kupima ni kiasi gani Wanawake wanapata maumivu wavaapo aina ya viatu hivyo.
Brandon Cohen aliamua kutenga siku maalumu kuvaa viatu hivyo vijulikanavyo kama High heels, baada ya kusikia malalamiko kwa wanawake wengi kwamba viatu hivyo vinawaumiza.
“Nilitaka kufahamu ni kwa nini Wanawake wengi wanalalamika kwamba viatu hivi vinawaumiza, na kwa nini sasa wanavivaa?”, alisema na kuhoji Brandon Cohen.
Bhuku akiwa amevaa viatu vya kike Brandon Cohen, siku hiyo aliavaa viatu hivyo na kuendelea na ratiba yake kama kawaida, ambapo alitoka kwenda kazini, kutembea mitaani, kuendesha gari na kwenda kwenye maduka mbalimbali ya shooping ambapo alipata changamoto ya watu wengi kumuangalia kwani ilionekana ni kitu cha ajabu kwa mwanaume kuvaa viatu vya kike.






Wakati kukiwa na sintofahamu kuhusu hatma ya uchaguzi mkuu wa Burundi unaotarajia kufanyika mwezi ujao kutokana na vurugu za kisiasa zinazoendelea kupinga kugombea tena kwa Rais Pierre Nkurunziza..headlines zimerudi tena nchini humo.
Makamu wa Rais wa nchini hiyo Gervais Rufyikiri ametoroka nchini humo na kudaiwa kimbilia Ubelgiji baada ya kupinga hatua ya Rais wa nchi hiyo kuwania muhula wa tatu akiungana na makamishna wa tume huru ya uchaguzi na jaji mmoja wa mahakama ya kikatiba.
Benki ya NMB Tawi la Mkuranga Limevamiwa na majambazi na kupora fedha nyingi ambazo zilikuwa zimefikishwa kwenye benki hiyo na gari maalum.
Marupu adhaminiwa na wanafunzi
Katika hatua nyingine, mgombea mwingine, Maliki Marupu amesema amelazimika kutumia mkoa maalumu wa vyuo vikuu kupata wadhamini ili kukwepa changamoto ya fedha za kuzunguka katika mikoa mbalimbali.
Marupu ambaye ni mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu Mzumbe alilieleza Mwananchi jana kuwa anatarajia kukamilisha idadi ya wadhamini 450 kwenye Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Morogoro.
Alipoulizwa kama haoni kuwa kwa kutumia mkoa huo wa vyuo vikuu pekee atakuwa amekosa sifa kwa kushindwa kutembelea mikoa mingine 14 zaidi inayotakiwa, Marupu alisema hata hao wanafunzi wanaunda mkoa wa vyuo vikuu kuna mikoa yanayotoka, hivyo haoni shida kumdhamini.
Lowassa avunja rekodi
Mkoani Arusha, Edward Lowasa ameendelea kuvunja rekodi ya idadi ya watu wanaojitokeza kumdhamnini baada ya kupata wadhamini 120,392 jana.
Rekodi hiyo ya Arusha imezipiku ile iliyowekwa na mkoa ya Iringa alikodhaminiwa na wanachama 58,562.
Mbunge huyo wa Monduli aliwasili jijini Arusha saa 9:00 alasiri na kupokelewa kwa mbwembwe zilizoambatana na nyimbo mbalimbali za wasanii kadhaa nchini. Lowassa aliongozana na mkewe Regina na viongozi kadhaa wa CCM.
Mara baada ya kuwasili uwanjani hapo, Lowassa alifanyiwa maombi rasmi na wazee wa kimila wa jamii ya Wamaasai, maarufu kama Malwaigwana.
Minara 292 ya mawasiliano iliyojengwa na Kampuni ya Simu ya Excellentcom Tanzania mwaka 2008, imetelekezwa bila kutoa huduma yoyote, JAMHURI linaripoti.
Baada ya kuitelekeza kwenye viwanja ambavyo baadhi vina makazi ya wamiliki wa ardhi hiyo, kumefanya kampuni hiyo sasa kudaiwa mamilioni ya shilingi ya kodi za pango la eneo.
Kampuni ya Excellentcom Tanzania Limited ilisajiliwa kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Septemba 13, 2006 ikiwa na wanahisa wawili — Jitco Limited ikiwa na hisa 3,500 na Excellentcom Systems hisa 6,500.
Mara baada ya kusajiliwa, kampuni hiyo ilianza mchakato wa kusimika minara yake ya mawasiliano mwaka 2008 kwa kuingia mikataba ya pango na wananchi wanaomiliki maeneo ambayo minara hiyo imejengwa, lakini imeshindwa kutimiza masharti ya mikataba hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika ambazo JAMHURI imezipata, Excellentcom kwa sasa imeshindwa kuiendeleza sambamba na kulipa kodi za pango kulingana na mikataba hiyo na kufunguliwa kesi za madai na wananchi hao.
Helena Mafita, mkazi wa Mtaa wa Litapwasi, Chang’ombe Uwanja wa Taifa, Temeke jijini Dar es Salaam anasema kwamba kwa sasa hakuna walinzi wanaolinda minara hiyo iliyojengewa mitambo pamoja na jenereta kubwa.
Nyumbani kwa Helena mitambo hiyo imefungwa kwenye pointi ya longitudo nyuzi 039.26935 latitudo nyuzi 06.85363 kiwanja namba 28 ambako aliingia mkataba wa kampuni hiyo kwa miaka 20 kuanzia Agosti 15, mwaka 2008.
Katika mkataba huo ambao Helena alikuwa analipwa Sh 300,000 kwa mwezi ungefika ukomo Agosti 14, 2028. Helena anadai kuwa hajalipwa na kampuni hiyo tangu mwaka 2010 na kila anapofuatilia ofisi za Excellentcom, Mikocheni, hafanikiwi kuwaona wahusika baada ya kuelezwa kuwa “ofisi hiyo haipo kwa sasa hapo.”
Hali hiyo ilimfanya Helena aende kwa wanasheria ili kufuatilia haki (pango) yake kwa njia ya mkondo wa sheria ambako sasa amewakodi mawakili wa Kampuni ya CERW. Katika barua hiyo ya Novemba 18, 2013 yenye Kumb. Na. CERW-ADV/HELENA/2013/01, mawakili hao waliandika,
Matumizi ya mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter, Instagram ni kitu ambacho kimeshika chati sana kwa sasa duniani, vijana wameonekana kuwa waathirika wakubwa wa matumizi ya mitandao hii.
Kijana Little Wang ambaye umri wake ni miaka 19 huko China aliona njia pekee ya kukomesha tabia yake ya kupenda kutumia laptop na simu kuingia mtandaoni ni kujikata mkono wake, alipoona hali haimwendei sawa aliita taxi impeleke Hospitali ambapo hakuna aliyejua kinachoendelea nyumbani kwao, aliacha ujumbe kwamba ametoka kwenda Hospitali na angerudi muda mfupi baadaye.
Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya dola Bilioni 30 kwa ajili ya Kulinda mazingira, Kukuza uhifadhi na Utalii nchini.
Hafla ya kutiliana saini ilifanyika jana, Seronela mkoani Arusha ambapo waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress walisaini makubaliano ya dola 2milioni kwa ajili ya kuendeleza mapambano ya ujangili n anyingine milioni 14.5 kwa ajili ya uhifadhi.
Balozi huyo wa Marekani Mark Childress, alimwelezea Nyalandu, kuwa ni mwanasiasa jasiri na makini asiyeogopa kusema ukweli hata kama unaumiza.
Baraza la Ushauri la Wazee wa CCM linaundwa na wajumbe sita ambao ni wenyeviti na makamu wenyeviti wastaafu Taifa wa chama hicho.
Nao ni Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi (Mwenyekiti), Makamu Mwenyekiti mstaafu (Tanzania Bara), Pius Msekwa (Katibu); Benjamin Mkapa (Mjumbe); Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume; Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour; na Waziri Mkuu mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), John Malecela.
Habari kutoka vyanzo vya kuaminika zinasema Katibu wa Baraza hilo, Pius Msekwa, tayari ameshaandika barua kwenda kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania Bara), Rajab Luhwavi, akimtaka aitishe kikao cha Baraza hilo.
Kwa maelekezo hayo, Baraza la Ushauri la Wazee linatarajiwa kuketi wiki hii, Juni 25. Kwa maelekezo ya Msekwa, waalikwa kwenye kikao hicho, ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Dk. Edward Hoseah, na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman.
Wananchi wa Kenya sasa wataweza kununua maji safi na salama kwa kutumia kadi maalum kupitia mitambo kama ya ATM.
Hii ni nafasi nzuri ya kuleta mabadiliko, kuhamasisha vijana na kuwasaidia kujijenga kibiashara endelevu na ninapenda kuwapongeza Airtel kwa ajili ya mpango huu," alisema Mulamula.
Bwana Mulamula aliahidi kufanya kazi kwa karibu na Airtel pamoja na jopo la washauri katika kuhakikisha wanachagua na kuwapa mafunzo walengwa wa Airtel Fursa ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kuweza kutumia techonologia ya habari yaani ICT kama nyenzo muhimu itakayowawezesha kuleta ufanisi katika shughuli zao za uzalishaji na kiuchumi.
Akiamini kuwa vijana watakaofaidiaka na Airtel fulsa watahamasisha na kuongoza katika kuleta mabadiiko kwenye jamii zao huku akihakikisha mpango huu unakuwa na mafanikio makubwa kwa walengwa na kuwa na mvuto kwa vijana wengine .
Mhandisi Mulamula ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dar Teknohama (ICT) Business Incubator (DTBi) kwa ajili ya ujasiriamali katika Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), analeta uzoefu wa kutosha katika mpango huu wa Airtel fursa kwenye nyanja ya ujasiriamali na kukuza biashara zinazoanza.
Yeye ni mshauri na mwalimu kwa wajasiriamali. Amekuwa akisaidia kuinua vipaji vya watu mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na katika mkutano wa kimataifa wa ujasiriamali nchini Moscow, Durban na Nairobi kwa ajili ya maonyesho ya Afrika.
Pia ni Mjumbe wa Bodi ya Demeter nchini Boston USA na pia Mjumbe wa Bodi ya XPrize nje ya California, Marekani.
“Mpango huu unatafuta vijana wenye kiu, nguvu na utayari wakupata wanachokiamini na kukihitaji, wenye uwezo wa kuzipitia changamoto na kufikia matarajio waliojiwekea na wakati huohuo kubadilisha maisha yao” aliongeza.
Mwananmke mwingine ambaye ni kada wa CCM, Ritta Ngowi amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama kuwania urais katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu jana makao makuu ya CCM mkoani Dodoma Ngowi alisema akifanikiwa kuwa rais ataanzisha kituo kikubwa cha kuwahudumia wastaafu, walemavu, wasiojiweza na vijana.
Kingine atakachofanya ni kuendeleza mazuri yaliyofanywa na marais waliopita, lakini zaidi akiweka mkazo kwenye masuala ya elimu na kukuza uchumi.
Aidha Ritha anafanya , idadi ya wanawake waliojitosa mbio za urais kufikia watano kati ya 39 waliochukua fomu hadi sasa.
Hiki ndicho alichokisema waziri Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa
amesema hana shaka na swala la kukatwa
jina lake katika vikao vya Chama cha
Mapinduzi(CCM), kwani anaamini Chama
chao kitatenda haki kwa kurudisha jina lake
kuwa mgombea urais wa Tanzania.
Lowassa aliyasema hayo jana wakati
akizungumza na wanachama wa CCM na
wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika ofisi
kuu za CCM Mkoani humo, wakati akitoa
shukrani baada ya kudhaminini na wanaCCM
zaidi ya elfu 52.
Barcelona Star Neyamr ambae hivi karibuni amepigwa panga la kukosa mechi nne kwenye Copa America baada ya kitendo cha utovu wa nidhamu alichofanya kwenye mechi.
Staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu ambaye ametangaza nia ya kugombea nafasi ya ubunge wa viti maalumu Singida,amesema anafurahishwa na kitendo cha mashabiki wake kumwigiza sauti akiwa bungeni kwa kuwa wameonyesha kumkubali kabla hajafika ‘Mjengoni’.
Alisema sauti hiyo inayomuigiza alitumiwa kupitia simu yake na haikumkwaza zaidi ya kufurahia kwamba watu wengi wanakubali awe bungeni.
Wagombea wetu ama watangaza nia tunawapima kwa kipimo gani? Na Je kipimo hicho kina usawa? Tukiacha ushabiki ulio wa wazi ni vigezo gani hasa tunatumia kuwapina?
Tunaposhurutisha Taifa na mgombea tunayemtaka kwa kuaminisha uwezo wa mgombea huku kiukweli tunajua uwezo una walakini je hiyo ni busara?? Na Je rekodi yake kiutumishi ni njema na inaridhisha??
Sizungumzi kwa siasa na vipimo vya majitaka, au hisia na uzushi usio na vithibitisho bali uwazi wa uwezo wa mgombea na uimara wake
Uimara wa mgombea uanze na uwezo wake na wapambe wake kujihoji kwa dhati na si ushabiki kama kweli mgombea ana uwezo wa kweli kuwa Rais. Kazi hii ya urais ni ya dhamana na majukumu makubwa ambayo inahitaji akili na maarifa ya rais yawe na uwiano wa kufanya mambo kwa usahihi.
Vita Saa chache tu baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar akitokea nchini Marekani kwa shughuli za kimuziki, staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ametangaza kile kinachotafsirika kuwa ni vita dhidi ya hasimu wake kwenye anga la muziki huo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz.
Ali Kiba alitema cheche Alhamisi ya wiki iliyopita ndani ya Hoteli ya Sea Cliff, Masaki jijini Dar, kulikokuwa na uzinduzi wa kampeni ya kupinga vita ujangili, iliyoratibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, huku akiwa ni mmoja wa mabalozi sanjari na mlimbwende wa zamani, Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi ‘K-Lyin’.
Baada ya shamrashamra za ‘event’ hiyo, haraka sana kama mshale wa Mmakonde, mwandishi wetu alimfuata Ali Kiba, lengo kuu likiwa ni kusikia chochote juu ya ushindi wa Tuzo za Kili ambapo alizoa tano binafsi na moja ya kushirikishwa.
Kiba alisema anaamini alistahili kushinda tuzo zote kwani vigezo na sifa anazo na amejiandaa kikamilifu kupambana na yeyote anayedhani kuwa ni mfalme wa muziki huo.
Mbunge wa Mbeya Mjini kwa ‘leseni’ ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’ amemfikisha kotini aliyekuwa mkewe, Faiza Ally akitaka apewe mtoto wao, Shaa (2) ili amlee kwa vile mama yake huyo si mwadilifu.
Aliyekuwa mkewe na mbunge wa mbeya mjini Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally akiwa katika pozi.