Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

AMEAMUA KUVAA VIATU VYA KIKE LENGO NI KUTEST MAUMIVU YAO

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Brandon Cohen, mkazi wa mji wa Los Angeles huko Marekani ametoa kali ya mwaka baada ya kuamua kuvaa viatu vya kike ili kupima ni kiasi gani Wanawake wanapata maumivu wavaapo aina ya viatu hivyo.

Brandon Cohen aliamua kutenga siku maalumu kuvaa viatu hivyo vijulikanavyo kama High heels, baada ya kusikia malalamiko kwa wanawake wengi kwamba viatu hivyo vinawaumiza.

“Nilitaka kufahamu ni kwa nini Wanawake wengi wanalalamika kwamba viatu hivi vinawaumiza, na kwa nini sasa wanavivaa?”, alisema na kuhoji Brandon Cohen.

Bhuku akiwa amevaa viatu vya kike Brandon Cohen, siku hiyo aliavaa viatu hivyo na kuendelea na ratiba yake kama kawaida, ambapo alitoka kwenda kazini, kutembea mitaani, kuendesha gari na kwenda kwenye maduka mbalimbali ya shooping ambapo alipata changamoto ya watu wengi kumuangalia kwani ilionekana ni kitu cha ajabu kwa mwanaume kuvaa viatu vya kike.

“Changamoto nyingine niliyoipata ni kwamba kila nilipopita nilisikia minong’ono watu wakisema kwamba mimi ni shoga, kuna wakati nililazimika kuegesha gari mbali kidogo na maeneo ya maegesho ili kukwepa watu”, alisema Brandon Cohen.

Brandon Cohen alisema pamoja na yote hayo lakini aligundua kwamba wanawake wanapata maumivu makali sana wavaapo mavazi hayo, lakini wanapenda kuvaa viatu hivyo sababu wanapendeza na watu watu hupenda kuona wanawake wakiwa kwenye vazi la viatu hivyo.

“Siwezi kurudia kuvaa viatu hivyo tena kwani nimeumia sana, haya maumivu ni makali sana”, alimalizia Brandon Cohen ambaye alivaa viatu hivyo kwa saa 12 tu kwani maumivu yalimzidi.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top