Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MALIKI MARUPU ADHAMINIWA NA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Marupu adhaminiwa na wanafunzi
Katika hatua nyingine, mgombea mwingine, Maliki Marupu amesema amelazimika kutumia mkoa maalumu wa vyuo vikuu kupata wadhamini ili kukwepa changamoto ya fedha za kuzunguka katika mikoa mbalimbali.

Marupu ambaye ni mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu Mzumbe alilieleza Mwananchi jana kuwa anatarajia kukamilisha idadi ya wadhamini 450 kwenye Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Morogoro.

Alipoulizwa kama haoni kuwa kwa kutumia mkoa huo wa vyuo vikuu pekee atakuwa amekosa sifa kwa kushindwa kutembelea mikoa mingine 14 zaidi inayotakiwa, Marupu alisema hata hao wanafunzi wanaunda mkoa wa vyuo vikuu kuna mikoa yanayotoka, hivyo haoni shida kumdhamini.

Marupu, mwenye umri wa miaka 34, alisema endapo angefuata mikoa ya kijiografia ingekuwa shida kwake kutokana na kukosa fedha.

Alisema katika mzunguko wake alipata changamoto za watu walioko katika ofisi za wilaya wakisubiri kudhamini wagombea kwa malipo ya Sh20,000 au 30,000, hivyo akaamua kuwakwepa na kudhaminiwa na wanafunzi wenzake.

Mwanafunzi huyo alisema licha ya kukamilisha idadi ya wadhamini, atakwenda nyumbani kwao Ukerewe kutafuta baraka za wazee kabla ya kuwasilisha fomu zake Dodoma.

Makada nane warejesha fomu
Jumla ya makada wanane wamerudisha fomu za kuomba kuteuliwa na CCM kuwania urais, huku Boniface Ndengo akisema amekumbana na tatizo la kuombwa fedha na wanachama kwa ajili ya wamdhamini.

Wengine waliorejesha fomu jana ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani.

Akizungumza mjini hapa mara baada ya kurejesha fomu hizo, Ndonge alisema katika mchakato wa kukusanya wadhamini amebaini wananchi wa kawaida nao ni zao la rushwa.

“Unafika mahali wananchi wanakataa kukudhamini kwa sababu hauna pesa ya kuwapa. Mimi niliwaambia sina fedha ila ninataka kuwatumikia. Waliniambia mbona fulani katoa kiasi fulani wewe hutoi,”alisema.

Alilalamikia makada wenzie waliochukua fomu kuandikwa mara nyingi katika vyombo vya habari na wengine kutopewa nafasi. Ndonge alisema alifanikiwa kupata wadhamini 602 katika mikoa 20 aliyoenda.

Katika hatua nyingine, Waziri Chikawe aliwaomba msamaha waandishi wa habari kuwa hataweza kuzungumza nao kutokana na kukimbilia majukumu mengine.

Kwa mujibu wa ratiba ya chama hicho mwisho wa kuchukua fomu na kurudisha ni Julai 2 saa 10:00 jioni. Kazi hiyo ilianza Juni 3.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top