Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

HAYA NDIYO MAPENZI YA KWELI YA KUFA NA KUZIKANA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
SEHEMU YA KWANZA.

Mungu ameujaalia mkoa huu kwa kuwa na milima kila sehemu na miti yenye majani ya rangi ya kijani kibichi. Ameupa ardhi yenye rutuba iliyoweza kuzalisha mazao mbali mbali, pia amewapa mito japokuwa kasoro yao ni moja kubwa na ndio jina livumalo hususani ukiitaja kasoro hiyo.


Nauzungumzia mji kasoro bahari. Si mwengine na mji wa Morogoro. Huko aliishi mzee kambi na mtoto wake wa pekee Aisha. Hiyo ni kutokana na kumpoteza mke wake na kuamua kuishi hivyo huku akiridhika kumlea mtoto wake huyo wa kike aliyeachwa na mama yake akiwa na umri wa miaka sita tu.

Maisha sio mazuri kwa upande wa kipato, ila furaha ya familia hiyo ilizika mapengo yote ya umasikini walionao. Aisha alikua kwa kasi na kupelekwa shule na baba yake alipofikisha umri wa miaka saba. 

Kichwa cha msichana huyo kiliwafurahisha sana walimu wake kutokana na uwezo wa darasani aliokuwa nao. Alishika nafasi ya kwanza kuanzia darasa la kwanza hadi darasa la sita ambapo aliachishwa shule na baba yake mkubwa baada ya baba yake mzazi kupooza viungo kuanzia kiunoni kushuka chini.

Walimu na wanafunzi wenzake walisikitishwa na hatua hiyo, lakini hawakuwa na la kuamua japokuwa waliamini kuwa angemaliza darasa la saba, basi lazima angefaulu tena kwa kiwango kikubwa.

Kazi ya kumuhudumuia baba yake aliachiwa peke yake. Hadi kuna vitu vingine kama kumsafisha pindi baba yake alipojisaidia aliifanya yeye mtoto wa kike huku ndugu zake wakiwa wanakuja kwa nadra sana kuwatembelea.

Mzee kambi alikua analia kila siku na kumuomba mungu amchukue ili mtoto wake asipate yale mateso aliyokuwa anayapata juu yake. Siku moja Shani alitumwa na baba yake aende akamtafutie ndulele kwa kua alikuwa anashida nazo.

Kwakua walikua wanaishi mbali kidogo na shamba lao, ilimchukua dakika ishirini kwenda na kurudi baadae baada ya dakika zipatazo arobaini na tano toka alipotoka pale.

“baba…babaaaaaaaaaaaaa’ Alilia kwa uchungu Aisha baada ya kumuona baba yake amekata roho baada ya kujichoma na kisu alichokua anakitumia kummenyea baba yake machungwa.

Kilio kilikua zaidi na majirani walikisikia kilio kile na kukusanyika eneo la tukio. Waliungana na yule mtoto na wengine wakimpooza mazito yaliyo mkuta. Baada ya mazishi ya mzee Kambi, baba mkubwa wa Aisha alichukua jukumu la kumlea mtoto huyo.

Ukurasa mpya wa mateso kutoka kwa mama yake mkubwa na baba yake huyo ulifunguliwa baada tu ya arobaini ya mzee kambi. Aligeuzwa mfanyakazi wa ndani kwenye nyumba ya marehemu wazazi wake, alichota maji, kufua nguo za watu wote mule ndani na kila kazi zenye uhusiano na ile familia, basi alizifanya yeye.

Maisha ya tabu,dhiki,mateso na msoto ndio uliomkuza Aisha. Ugumu wa maisha na kutafutiwa wanaume kwa ajili ya kuolewa kinguvu ndio vitu vilivyomchosha Aisha na kuamua kutoroka nyumbani kwao na kukimbilia kijiji cha pili.

Huko alipata hifadhi na mama mmoja baada ya kumuhadithia kila kitu kilichohusu maisha yake. Kwa imani ya yule mama, alimkaribisha na kuanza kuishi naye kama mtoto wake. Uzuri uliofunikwa na shida miaka mingi iliyopita, ulianza kuonekana taratibu kama kijua cha asubuhi kichomozapo. 

Hali iliyofanya vidume vya kijiji hicho kumtolea macho. Alinawiri vizuri kutokana na matunzo ya yule mama ambaye alifaidika naye kutokana na yeye alivyokuwa anajituma. Aisha alipotimiza miaka ishirini na moja, alifanikiwa kumpata ampendaye pale kijijini. 

Alianzisha uhusiano na mvulana huyo wa kwanza katika maisha yake kwa makubaliano ya kutofanya mapenzi mpaka ndoa. Kutokana na uelewa na mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo ZAKARIA, alikubaliana na Aisha na mapenzi yao yalinoga bila kushiriki kitendo hicho. Kila mahali walikuwa wote na walipendezana kwa hali yao.

Hakika walikuwa wakivutia kwa kila mahali wapitapo. Baada ya mwaka mmoja toka waanzishe uhusiano wa kimapenzi, Zakaria aliitwa na kaka yake Dar- es-salaam kwa ajili ya kufanya kazi kutokana na kupata nafasi aliyokuwa anamuahidi kila siku.

Kwa majonzi makubwa, Zakaria alimuambia kua anaenda kutafuta maisha na yakikaa sawa basi atakuja kumchukua. Wote walilia sana na kupeana ahadi ya kuishi pamoja tena kivyovyote vile. Zakaria aliondoka na kumuacha Aisha peke yake.

Baada ya miezi sita kupita, mama mlezi wa Aisha aligongwa na nyoka alipokuwa Shambani na kupoteza maisha. Lilikua ni zaidi ya pigo kwa Aisha ambaye hakuwa na mtegemezi mwingine pale kijijini zaidi ya yule mama peke yake.

Alilia sana na baadae uamuzi wa kwenda kumtafuta mpenzi wake mjini Dar-es-salaam ulimjia. Hela za pole alizozipata ndizo alizozitumia kwenda nazo Dar, bila kujua ni wapi afikiapo, atakapolala wala chakula atakachokula kwa siku zote atakazokuwa mjini. Yote hayo hakuyawaza zaidi ya kuamini kuwa akifika huko ataonana na mwanaume wa ndoto zake. ZAKARIA.

ITAENDELEA SEHEMU YA PILI.....……..

Jiunge na mi kwa kubonyeza kwenye link zifuatazo chini ili kupata habari mpya zaidi. 

        FACEBOOK >>> TWITTER  >>> MATUKIO KWA NJIA YA SAUTI
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top