Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MGOGORO WA ARDHI KWA WAKAZI WA CHASIMBA, CHA TEMBO NA CHA CHUI WAPATIWA DAWA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Hatimaye mgogoro wa ardhi wa wakazi wa chasimba,cha hui na cha tembo uliodumu kwa muda mrefu umetatuliwa rasmi na waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi mh.wilium lukuvi baada ya kufanya mazungumzo na mwekezaji wa kiwanda cha cement na kukubali kuwapa hekta 224 watakazo gawiwa na kupewa hati miliki.

Mh.lukuvi akizungumza katika mkutano na wananchi wa cha simba cha chui na cha tembo akisindikizwa na viongozi wengine wa majimbo na mitaa amesema licha ya mwekezaji kushinda keshi ya kumiliki eneo lote la ardhi yao amekubali kuwapa hekta 224 ikiwa ni jitihada za waziri na kufanya nae mazingumzo ambapo amewataka wananchi hao sasa kutambua kuwa maeneo watakayopangiwa wataishi kwa amani.

Mh mbunge saidi kubenea akimwakilisha mbunge wa jimbo la kawe mh halima mdee alikasirishwa na hatua ya wananchi hao kugoma kutoa shiling elfu kumi kama fedha ya kusaidia zoezi la kupima viwanja hivyo na kuwatahadharisha endepo zoezi hilo likikwama basi itakuwa wamejitakiwa wenyewe kuendelea kuwa wakimbizi.

Nao baadhi ya wakazi wa maeneo hayo licha ya kumshukuru mh waziri wa ardhi wamesema sasa wanaweza kufanya shughuli za kimaendeleo na kujikwamua kiuchumi.


Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top