Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

AMREF YAZINDUA MRADI WA KUPAMBANA NA UKEKETAJI WA WANAWAKE, ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

AMREF yazindua mradi wa kupambana na ukeketaji watoto wa kike mkoani Mara.

Wilaya ya Serengeti mkoani Mara imetajwa kuongoza kwa kiasi kikubwa kwa vitendo vya ukeketaji watoto wa kike hatua ambayo imeelezwa kuwa mbali na kusababisha idadi kubwa ya watoto wa kike   kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu kutokana na kuolewa muda mfupi tu baada ya kukeketwa lakini pia vitendo hivyo vimetajwa pia kuchangia ukatili mkubwa kwa watoto wa kike.

Kufuatia ongezeko kubwa la kiwango cha ukeketaji kwa watoto wa kikemkoani Mara hasa katika wilaya ya Serengeti, shirika la afya barani Afrika AMREF kwa kushirikiana na kituo cha sheria na haki za binadam LHRC wamezindua mradi wa tokomeza ukeketaji ambao unalenga kupambana na vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike katika wilayani ya Serengeti mkoani Mara.

Meneja wa mradi huo wa tokomeza ukeketaji wilayani Serengeti, Bw Phinias Johnstone, akizungumza wakati wa uzinduzi huo ambao umefanyika katika viwanja vya mbuzi mjini mugumu wilayani Serengeti, amesema mradi huo unalenga kupunguza vitendo vya ukeketaji katika wilaya hiyo hasa kwa mwaka huu ambapo tayari baadhi ya jamii imeanza kufanya maandalizi makubwa ya kukeketa watoto wa kike.

Akisoma hotuba ya mkuu wa wilaya ya Serengeti wakati wa uzinduzi     wa mradi huo tokomeza ukeketaji wilayani Serengeti, katibu tawala wilaya wa wilaya hiyo Bw Qamara Cosmas, amesema mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na vitendo vya ukeketaji ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya serikali katika kupambana na vitendo hivyo vya ukatili.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top