Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUANZA UCHUNGUZI

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Wizara ya Maliasili na Utalii imeanza kufanya uchunguzi kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali, ikiwemo Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) na vyombo vya ulinzi na usalama ili kubaini waliohusika na upitishwaji wa nyara za serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) hivi karibuni.

Wizara hiyo pia imeeleza kupokea kwa masikitiko makubwa taarifa hizo za kukamatwa kwa nyara za serikali katika Uwanja wa Ndege wa Zurich nchini Uswisi zikiwa njiani kwenda China kutokea Uwanja huo wa Ndege wa Kimataifa wa JNIA wa jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya wizara hiyo kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Waziri Lazaro Nyalandu ilisema wizara hiyo inaupongeza uongozi wa Uwanja wa Ndege wa Zurich na Serikali ya Uswisi na watu wote walioshiriki kubaini na kukamata nyara hizo.


Waziri Nyalandu alisema, nyara hizo zinajumuisha meno ya tembo yenye uzito wa kilo 262, kucha na meno ya simba vyenye uzito wa kilo moja.

Alisema tukio la kukamatwa kwa nyara hizo lilitokea kwenye uwanja huo Julai 6, mwaka huu zikiwa ndani ya masanduku manane zikiwa njiani kwenda Beijing China kutokea uwanja wa ndege wa Dar es Salaam kupitia Zurich.

“Wizara imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hizi na kwamba nyara hizo zimesafirishwa kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere. Tukio hili linadhihirisha kuwa tatizo la ujangili bado linaendelea ndani na nje ya nchi yetu” alisema.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top