Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UANDIKISHAJI VITAMBURISHO BVR DAR WAVUKA LENGO

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Licha ya kuanza kwa kusuasua, kazi ya uandikishaji wapigakura katika mfumo wa kielektroniki wa BVR katika Jiji la Dar es Salaam, imepata mafanikio na kuvuka lengo la uandikishaji lililokuwa limewekwa.

Awali, ilikadiriwa watu 2,810, 423 sawa na asilimia 98, lakini baada ya kumalizika kwa siku za uandikishaji juzi, waliojiandikisha wamefikia 2,845,256 sawa na asilimia 101.2 Hayo yamethibitishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana, kuhusu kukamilika kwa kazi hiyo jijini Dar es Salaam.

Alisema hadi Agosti 4 mwaka huu mkoa wa Dar es Salaam, wananchi waliojiandikisha katika wilaya ya Kinondoni walikuwa 1, 157,617 sawa na asilimia 105, ambapo lengo lilikuwa 1,102,565. Wilaya ya Temeke imeandikisha wapigakura 886,564 sawa na asilimia 98.9 lengo lilikuwa 896,142.

Wilaya ya Ilala imeandikisha wapigakura 886,564 sawa na asilimia 98.9 lengo likiwa ni 811,716. Kutokana na kukamilika kwa uandikishwaji huo, NEC ilitangaza rasmi kukamilika kwa uandikishaji katika mkoa wa Dar es Salaam Agosti 4, hivyo kuhitimisha rasmi uandikishaji wa wapiga kura kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa BVR kwa nchi nzima.

Alisema NEC inasisitiza kuwa hakutakuwa tena na muda wa nyongeza wa kuandikisha wapiga kura. Kazi inayoendelea hivi sasa ni kuweka wazi daftari la awali la wapiga kura pamoja na kutoa fomu za kugombea urais, waliopitishwa na vyama vyao vya siasa.


Alisisitiza kuwa NEC inaendelea kuliweka wazi daftari la kudumu la wapiga kura, ambapo hadi sasa tayari mikoa 19 imekwishapelekewa daftari la awali la wapiga kura. Alisema Dar es Salaam na Zanzibar, mchakato wa kuandaa daftari la awali unaendelea na unatarajiwa kukamilika muda si mrefu kuanzia sasa baada ya uandikishaji kukamilika.

Alisema kazi ya kuweka wazi daftari hilo, linafanyika ili kutoa fursa kwa wale wote waliojiandikisha, kusahihisha taarifa zao, kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au jimbo moja kwenda kata au jimbo lingine, kutoa kadi kwa wapiga kura waliopoteza kadi zao na kuangalia iwapo taarifa za mpiga kura aliyejiandikisha zipo kwenye daftari.

Pia, kuweka pingamizi kwa jina au taarifa za mpiga kura asiye na sifa ya kuwemo katika daftari la kudumu la wapiga kura. Alisema kazi ya uandikishwaji katika mkoa wa Dar es Salaam na nchi nzima imefanyika na kukamilika kwa mafanikio makubwa, licha ya changamoto za zilizojitokeza hasa katika hatua za mwanzo za uandikishaji.

Uandikishaji huo kwa mkoa wa Dar es Salaam ulianza rasmi Julai 22 na kufanyika kwa siku 10, muda ambao haukutosheleza kutokana na idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza hali ambayo tume ililazimika kuongeza siku nne zaidi.

“Hii inatafsiriwa kuwa imetokana na mwamko mkubwa wa wananchi waliojitokeza kujiandikisha katika daftri la kudumu la wapiga kura ikilinganishwa na miaka mingine iliyopita,” alisema.

Sambamba na hilo, tume inaendelea na kazi ya utoaji fomu za urais kwa wagombea urais na wenza wao, ambapo hadi kufikia jana jumla ya vyama vya siasa vitano tayari wagombea wake wameshachukua fomu.

Hivyo ni United People Democratic Party (UPDP), Tanzania Labour Party (TLP), Democratic Party (DP), Chama cha Umma (CHAUMMA) na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top