Tume ya Uchaguzi (NEC),
imesema imeandikisha zaidi ya watu milioni 21 nchini tangu uandikishaji
uanze Februari 23, mwaka huu na kwamba, Dar es Salaam pekee,
wameandikishwa watu zaidi ya milioni mbili.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Damian Lubuva
alisema juzi Dar es Salaam kuwa, uandikishaji wa wapiga kura katika
Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo wa Biometric Voters
Registration (BVR) unaendelea jijini humo hadi Agosti 8.
Kwa mujibu wa Jaji Lubuva, baada ya siku hizo zilizoongezwa, hakutakuwa na muda mwingine utakaoongezwa.
“Tumieni
muda ulioongezwa kujiandikisha, vinginevyo mtaikosa haki yenu ya kupiga
kura kwa sababu ya kutoandikishwa katika Daftari la Wapigakura,” Jaji Lubuva alisema.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies