Ni mbunge wa Nzega Dr. Hamisi Kigwangalla ambaye alikua miongoni mwa waliojitokeza kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya CCM kuwania Urais wa Tanzania 2015.
Leo August 5 2015 alitumia page
yake ya twitter kuyatoa yake ya moyoni kwa kuandika sentensi kadhaa
kuhusu CHADEMA na Edward Lowassa kwa kuandika >>> ‘Baada ya safari ya matumaini kufa nimeambiwa Edward Lowassa ameiba jina la safari ya mabadiliko toka kwa Kigwangalla‘
‘CHADEMA ilipata
umaarufu kwa kupinga ufisadi na kumchafua Lowassa, leo wana kazi ya
kumsafisha na kujieleza kuwa wao si wa aina yake, uchaguzi2015 CCM itaheshimika zaidi, upinzani utapotezwa vibaya sana na utakufa kifo cha aibu #MagufuliMtendaji ‘