Mbunge wa Viti Maalumu Chadema, Chiku Abwao
ndiye atakayepeperusha bendera ya ACT kuwania ubunge wa Jimbo la Iringa
mjini katika uchaguzi mkuu ujao, huku akitamba kwamba atambwaga mbunge
anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema).
Mbali na Abwao aliyejiunga na ACT Wazalendo hivi karibuni, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chadema, Abuu Changawa naye ameiacha Chadema na kujiunga ACT Wazalendo, huku akitangaza kuwania udiwani katika Kata ya Mivinjeni, mjini hapa.
Abwao aliyewahi kuwa mbunge wa NCCRMageuzi, alisema; “Nimeondoka
Chadema baada ya kubanwa kila kona na Mchungaji Msigwa akidhani kwamba
mimi nilikuwa Chadema kwa sababu ya kutaka cheo.”
Alisema pamoja na kunusurika maisha yake
wakati akipigania ushindi wa Mchungaji Msigwa 2010, mahusiano yao
kisiasa yamekuwa mabaya kwa kipindi chote kwani kila alilokuwa akijaribu
kulifanya kwa niaba ya chama hicho alitafsiriwa analenga kugombea
ubunge jimbo la Iringa Mjini.
Alisema ili kumuonesha nguvu yake
kisiasa na kwamba yeye sio mwanasiasa anayetaka tu uongozi lakini mwenye
dhamira na maono ya dhati ya kusaidia kuleta mabadiliko nchini
atagombea ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini kupitia ACT Wazalendo.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies