Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Ujambazi Mkoa wa Morogoro, Elibariki Pallangyo , amepigwa risasi na kufa papo hapo nyumbani kwake eneo la Yombo jiji Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Andrew Satta
alisema kuwa usiku wa kuamkia jana majira ya saa tisa usiku, kundi la
watu zaidi ya kumi lilivamia nyumbani kwa Pallagyo eneo la Yombo kwa
kuruka ukuta, kisha kuvunja mlango na kuingia ndani walikopora fedha na
simu za mabinti wanne waliokuwa ndani kabla ya kufanya mauaji.
“Hili
tukio ni la kusikitisha kwani watu hawa wanaonesha walikuwa na lengo la
kumuua tu na si kupora mali, kwani wamechukua fedha Sh 130,000 pamoja
na simu za mkononi 4 ambazo walikuwa nazo hawa wasichana waliowakuta
sebuleni,” Satta.
Alisema baada ya watu hao kupora simu na
fedha kutoka kwa mabinti, waliekea kwenye chumba cha Pallangyo,
wakampiga risasi moja kifuani na kumuua.
Wauaji hao walitokomea kusikojulikana
huku wakisahau kifaa kinachotumika katika milipuko. Mwili wa marehemu
umehifadhiwa Hospitali ya Temeke na utapelekwa Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi kabla ya maziko.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies