Magazeti ya Agosti 4 2015
yako mtaani na vichwa vyake vikubwa vya habari, nimefanya jitihada ya
kukusogezea zile zote kubwakubwa zilizoweka vichwa vya habari magazetini
leo
Kuna stori kubwa zenye headlines zake mtaani leo, iko inayohusu Prof. Ibrahim Lipumba kuachia ngazi na mgogoro mzito unaotikisa, chanzo Lowassa?.. Zanzibar imesema haitotambua umoja wa UKAWA na maamuzi ya kutambua umoja huo ni ya Tanzania Bara na sio yao.
Dk. John Magufuli kuliteka jiji kwa kuchukua fomu ya Urais leo ataongozana na mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan kwenye ofisi za NEC.
CHADEMA yamuweka pembeni Dk. Wilbroad Slaa, wameamua kumpumzisha kwa muda baada ya kutoafikiana na maamuzi ya Chama kumkaribisha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
ADC yaanza mchakato wa
kumpata mgombea Urais wa mwaka 2015, leo ikiwa ni siku ya mwisho ya watu
kujiandikisha idadi wapiga kura Mil 2.6 waandikishwa kupiga kura na BVR Dar, hii ni aslimia 94%.
Rushwa yamtia kichefuchefu Rais Jakaya Kikwete, Mzee Peter Kisumo afariki dunia jana saa moja usiku kwenye Hospitali ya Muhimbili, kifo chake kimesababishwa na maradhi ya figo.