Stori ilianza kusambaa kuanzia
July 28 2015 kwamba Naibu spika wa bunge la jamuhuri ya muungano wa
Tanzania Job Ndugai amempiga mtu mpaka akazimia na kisha baadae
kufariki.
Hili tukio limefanya mpaka
millardayo.com imtafute kamanda wa Polisi Dodoma Kamishna msaidizi
mwandamiz wa Polisi David Misime ambaye ameyathibitisha haya >>> ‘Ukweli
nilionao mimi ni kwamba tarehe 28 2015 jioni Joseph Elieza Chilongale
alifika kwenye kituo cha Polisi Kongwa Dodoma akilalamika kuwa wakiwa
kwenye mkutano wa kujinadi kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Ubunge
jimbo la Kongwa kupitia CCM, alipigwa kwa kutumia fimbo kichwani na
tumboni na Job Ndugai‘
‘Baada ya kutoa taarifa hiyo
alipewa PF3 na akapelekwa Hospitali ambako amelazwa, tunachofanya ni
kuendelea na uchunguzi kwa kupata maelezo kutoka kwenye eneo la tukio
kutoka kwa watu waliokuwepo pale na baada ya kukamilisha upelelezi
tutafikisha jalada kwa Mwanasheria wa serikali aelekeze hatua za
kuchukua‘ – Kamanda Misime.
Kuhusu taarifa kwamba Joseph amefariki, Kamanda Misime amesema ‘hizo
taarifa sio za kweli sababu mkuu wa Upelelezi wilaya ya Kongwa muda
mfupi uliopita alikua pale Hospitali kuchukua maelezo yake kwa ajili ya
kukamilisha upelelezi‘
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies