Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KAMPENI ZA URAIS ZAZIDI TSH.5BILLIONS SOMA ZAIDI HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
MTANZANIA
Shirika la Umeme Tanzania TANESCO,  limesema haliwezi kutaja bei rasmi ya gharama za umeme wa gesi hadi mtambo utakapoanza kufanya kazi ili kubaini halisi.

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO  Felchesmi Mramba alisema Tanzania ni nchi ambayo inatumia kiwango cha chini cha gharama za umeme ikilinganishwa nan chi jirani za Afrika Mashariki.

Alisema mitambo ya umeme wa mafuta inatarajia kuzima ifikapo Septemba ndio maana wamesaini mkataba wa miezi mitatu kwa vile mwezi huo ndio mradi wa umeme wa gesi unakamilika.

Alisema mitambo ambayo haitakatishwa mikataba ni ule wa IPTL na Nyakato.
“Mkataba wa shirika la umeme IPTL  ni wa muda mrefu hivyo hatuwezi kukatisha mkataba isipokuwa  tutaiomba ibadilishe mfumo na kutumia gesi  lakini wa Nyakato ni kwa kwetu” Mramba.

Alisema Serikali pia inafanya juhudi za kupunguza utegemezi wa mitambo ya kufua umeme wa  na kutumia mafuta ambayo ni ghali zaidi na kuamua kutekeleza mradi wa Kinyerezi wenye uwezo wa kuzalisha MW 150 ambao utagharimu zaidi ya bilioni 293 na utakamilika Agosti mwaka huu.

NIPASHE
Mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) umeendelea kuibua mapya na kuleta mvutano baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Mark Mwandosya, kunukuliwa akisema kuwa majina matano yaliyopelekwa kwenye Kamati Kuu ya CCM (CC) kutoka kwenye Kamati ya Maadili yalijulikana hata kabla ya kikao cha Kamati ya Maadili hakijaketi.

Prof. Mwandosya ambaye ni Mbunge wa Rungwe Mashariki amenukuliwa akisema hayo kwenye sauti yenye maelezo yake iliyorekodiwa na kusambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Prof. Mwandosya alisema amepata taarifa za kusambazwa kwa sauti hiyo lakini hafahamu kama yanayozungumzwa humo ni ya kwake.
Prof. Mwandosya alisema anachokumbuka akiwa kijijini kwao Lufilio wilayani Rungwe aliitwa na wazee na kufanya nao mkutano wa ndani wakitaka kujua nini kilichojiri wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais CCM.

“Niliitwa na wazee kwenye mkutano wa ndani wakitaka kujua nini kimetokea na inawezekana yaliyomo ndani ya hiyo clip yana ukweli, lakini wewe unadhani nilichokisema ni uongo?, Si kinalingana na hali halisi ilivyokuwa Dodoma,” alisema.

Hata hivyo, alisema taarifa zilizosambazwa kwamba anataka kuhamia Chadema siyo za kweli. Katika sauti iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Prof. Mwandosya amenukuliwa akisema kuwa majina ya makada walioingia tano bora katika kinyang’anyiro cha urais yaliyopelekwa Kamati Kuu yalijulikana hata kabla ya kikao cha Kamati ya Maadili hakijaketi.

Alisema Mwenyekiti wa Kamati Kuu, Rais Jakaya Kikwete, alikuwa na majina yake matano mfukoni na kamati yenyewe pia ilikuwa na majina yake.
Akizungumzia madai hayo, Prof. Mwandosya alithibitisha kuwa madai hayo ni ya kweli na kwamba wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa CCM waliokuwapo Dodoma wanalijua hilo.

“Hapo mimi sioni kwamba kuna jambo ambalo limepotoshwa, kwani yote yanayosemwa ni ya kweli na hata wajumbe wote waliokuwa Dodoma kwenye Mkutano Mkuu wanayajua vizuri mambo hayo,” Prof. Mwandosya.

Alisema ingawa hajaisikia sauti inayodaiwa kuwa ni yake, lakini  kama ni suala la kusema kuwa mgombea urais mteule wa CCM, Dk. John Magufuli hajawahi kuwa hata mwenyekiti wa tawi la CCM ni kweli.

Alizidi kueleza kuwa, anaona ni sahihi kwa sababu katika kumbukumbu zake hajawahi kusikia wala kumwona Dk. Magufuli akiwa Mwenyekiti wa Chama katika ngazi yoyote.

Nina kazi nyingi sijafungua mitandao ya kijamii kwa muda mrefu kidogo, lakini kama mambo yanayosemwa ni hayo, sioni kama kuna uongo ndani yake, ningepata shida sana kama mambo yanayozungumziwa yangekuwa siyo ya kweli, katika kumbukumbu zangu sijawahi kusikia Dk. Magufuli amekuwa Mwenyekiti wa Chama au Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama, lakini sasa ndiye atakayekuwa mwenyekiti wa Chama chetu nadhani hilo liko wazi,” alisema.
 top
Akizungumzia uamuzi wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Prof. Mwandosya alisema kuwa Lowassa ametumia haki yake ya kidemokrasia na yeye haoni kama kwa uamuzi huo amefanya kosa lolote.

Alisema vyama vya siasa ni sawa na madhehebu ya dini, ambapo waumini wanayo haki ya kwenda kuabudu katika kanisa wanalolitaka au ambalo imani yao inawatuma na hakuna mtu wa kuwapokonya haki hiyo.

“Alichokiamua Lowassa sidhani kama ana kosa, kwani anayo haki na uhuru wa kufanya alichokifanya, siku hizi kuna makanisa mengi, mtu anapoamua kwenda kuabudu katika kanisa analoona linamfaa huwezi kusema kuwa amekosea, labda ninachoweza kushauri ni CCM kujiuliza sababu za Lowassa kuondoka na ikiwezekana ijisahihishe ili watu wengi zaidi wasiondoke,” alisema.

NIPASHE
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai amehojiwa na Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kumshambulia kwa fimbo na kumjeruhi mgombea mwenzake katika mbio za kuwania ubunge wa Jimbo la Kongwa kwa tiketi ya CCM, Dk. Joseph Chilongani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, David Misime, alisema kuwa walilazimika kumhoji Ndugai baada ya kupokea malalamiko kuhusiana na tukio hilo lililotokea wilayani Kongwa juzi.

Inadaiwa kuwa Ndugai alimpiga fimbo na kumjeruhi vibaya Chilongani wakati wagombea hao na wenzao watano wanaowania kuteuliwa kuwa wagombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM walipokuwa wakijinadi ili wapitishwe na wanachama wenzao jimboni humo.

“Tulipokea malalamiko, tumemhoji Ndugai na kisha tukamuachia kwa dhamana… hivi sasa tunaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo,” alisema Kamanda Misime na kuongeza kuwa watatoa taarifa zaidi pindi uchunguzi ukikamilika.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Ezekiel Mpuya, alithibitisha vilevile kuwa Dk. Chilongani alipokewa kwao juzi jioni kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kongwa na kwamba hadi kufikia jana alikuwa bado akiendelea na matibatu.
“Anaendelea na matibabu lakini hali yake inaendelea vizuri,” Dk. Mpuya.

 Dk. Chilongani, alisema kuwa juzi, wagombea wote saba walifanya kampeni katika kata tatu na kabla hawajamalizia ngwe hiyo, ndipo sakata hilo lilipozuka.

Aliongeza kuwa wakati wakimalizia kujinadi kwenye kata ya Ugogoni, yeye alipanda jukwaani kujinadi kabla ya kufuatiwa na Ndugai, kwa mujibu wa ratiba waliyopangiwa na kiongozi wa msafara huo.

Alisema Ndugai baada ya kupanda jukwaani, licha ya kunadi sera, alianza kumshambulia (Ngatunga), kwa maneno makali akimtuhumu kuwa amekuwa akishirikiana na watendaji wa halmashauri ya wilaya kufanya ubadhirifu.

Aliposhuka jukwaani, akaendelea kunishambulia kwa maneno, nikamwambia kwa hadhi yako haustahili kufanya siasa za namna hii; akatishia kunipiga,Ngatunga.

Alisema Ndugai kwa kutumia fimbo kubwa aliyokuwa nayo mkononi muda wote, alimpiga Ngatunga kwenye paji la uso na sehemu nyingine za mwili hadi akazimia.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top