Hatimae
Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini, kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Mh. Joseph Mbilinyi almaarufu Sugu amepata mpinzani
aliyetangaza nia leo ya kuwania kiti hicho ndani ya Chama hicho.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari mara baada ya kuchukuwa fomu ya
Ubunge katika Ofisi za chama hicho Wilaya ya Mbeya mjini,Mwandishi wa
habari Mkongwe na mwakilishi wa kampuni ya magazeti ya Free Media mkoani
mbeya,Christopher Nyenyembe amesema endapo atapata ridhaa ya
kupeperusha bendera ya Chadema atakuwa jirani na wananchi kusikiliza
vipaumbele na kuahidi kuvitekeleza kwa asilimia 100.
Bw.
Nyenyembe ambaye amewahi kuwania nafasi ya Ubunge jimbo la Mbeya mjini
katika uchaguzi mkuu mwaka 2010 na kushika nafasi ya tatu kwa tiketi ya
Chadema akitanguliwa na Mh.Sugu na kufuatiwa na Mponzi ametaja
kipaumbele cha pili ni kuwasemea wanahabari wote mkoani Mbeya.