Imeelezwa
kuwa panya ndiye aliyekuwa chanzo cha tukio la waumini wanawake
kukanyagana kwenye msikiti mmoja katika mji wa Casablanca nchini Morocco
na kusababisha watu 80 kujeruhiwa.
Maafisa
wa nchi hiyo wamesema waumini waliokua msikitini walizimia baada ya
panya kukatiza kwenye mguu wa mwanamke mmoja aliyekuwa anaswali, na
kulazimika kukimbia nje na kusababisha hofu kwa wengine.
Tukio
hilo la kukimbia na kukanyagana katika msikiti wa Hassan II, lilitokea
jumatatu usiku wakati waumini wakiendelea na swala katika kipindi hiki
cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies