Lowassa akoleza joto Urais UKAWA, asubiriwa kujiunga CHADEMA, ACT Wazalendo watamba kusimama kivyaovyao Uchaguzi 2015, CUF yabariki mgombea Urais UKAWA na Obama amaliza ziara yake ya siku 3 nchini Kenya.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC yadai kuwa Mgombea Urais kupitia CCM Dk. John Magufuli anakiuka sheria na kanuni za Uchaguzi Mkuu kwa kuanza kampeni kabla ya wakati.
Changamoto za BVR bado zinaendelea kuibuka Dar, lengo la kusajili watu Mil.2 linazidi kutia mashaka baada ya kasoro kadhaa zinazoendelea kujitokeza.
Zitto Kabwe asema kuwa Chama cha ACT Wazalendo kitasimama chenyewe kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na hakitaungana na UKAWA.
Rais Barack Obama amaliza ziara yake ya Siku 3 nchini Kenya, akumbushia changamoto alizozipata kabla ya kuwa Rais ikiwemo kuibiwa begi Airport ya Jomo Kenyatta.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies