Headlines zimeendelea kwenye mwaka huu wa Uchaguzi 2015 ambapo UKAWA sio
jina geni kwa Watanzania, vyama mbalimbali vya upinzani vikiwemo
CHADEMA na C.U.F vilijiunga na vinataka kumtangaza mgombea mmoja
atakaewawakilisha.
Zitto Kabwe ambaye aliondolewa kwenye chama cha CHADEMA, alijiunga na chama cha A.C.T Wazalendo March 2015 ambapo siku kadhaa baadae chama hicho kilitaka kujiunga na UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI (UKAWA) lakini imeshindikana, haya hapa chini ndio maneno ya Zitto Kabwe July 26 2015.
‘Leo
siku nzima nilikua nina kikao cha mashauriano na viongozi wa chama wa
kata zote za mkoa wa Dar es salaam ( mikutano mikuu ya majimbo 10 ya
Dar) jumla ya wajumbe 1023 walihudhuriam, tumesisitiza kuwa hatutajiunga UKAWA… ikumbukwe kuwa tuliomba utaratibu wa kujiunga UKAWA mwezi Aprili mwaka 2015 na hatujajibiwa rasmi lakini moja ya chama ndani ya UKAWA kilitangaza kuwa hawatutaki‘ – Zitto Kabwe
‘Hata juzi kwenye gazeti la Mawio waliandika kuwa tumefukuzwa UKAWA, sisi
tumeamua kuingia kwenye uchaguzi wenyewe.. tarehe 10 Agosti 2015
tutatangaza mgombea Urais tutakayemuunga mkono baada ya mkutano mkuu wa
kidemokrasia wa ACT Wazalendo.Tutanadi #AzimioLaTabora kama zana ya kuleta mapinduzi katika nchi yetu‘- Zitto
Kwenye sentensi nyingine ya Facebook aliyoandika Zitto Kabwe saa kadhaa kabla ya hiyo ya juu aliandika >>> #ACTWazalendo Tutaingia
kwenye uchaguzi wenyewe. We will go it alone as a party to defend our
principles. Mkutano Mkuu wa Chama wa Kidemokrasia ( National Convention)
utafanyika tarehe 10 Agosti 2015′
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies