Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

SHULE 250 ZAFUNGIWA HUDUMA YA INTERNET NA VIJIJI 480 KUPATA HUDUMA YA SIMU

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Shule 250 kufungiwa huduma ya intanetiVijiji 480 kuunganishwa huduma ya simuSerikali kuzibana kampuni za simu nchini.

MIKAKATI ya serikali ya kutoa wataalamu wengi wa sayansi imeendelea kutetekelezwa kwa kasi, ambapo imetia saini mikataba kusambaza huduma za mtandao kwenye shule mbalimbali nchini.

Mikataba hiyo iliyotiwa saini jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, iko miwili ya kupeleka huduma za mawasiliano vijijini na kuunganisha mtandao wa intaneti katika shule utakaogharimu sh. bilioni 26.28.

Katika mikataba hiyo, serikali imeonya kuwa itazifuta kampuni ambazo zitashindwa kutekeleza makubaliano ya kufikisha mawasiliano kwa wakati katika vijiji 480 vilivyoainishwa.

Onyo hilo la serikali linatokana na kampuni hizo kushindwa kutekeleza makubaliano ya mkataba wa kupeleka huduma za mawasiliano vijijini, ambapo nyingi zimetekeleza kwa asilimia 50 tu.

Akizungumza wakati wa kutia saini mikataba hiyo, Profesa Mbarawa alisema awamu ya tatu ya kupeleka mawasiliano vijijini utahusisha kata 102 ambapo vijiji 480 vitanufaika nayo.
Alisema awamu ya kwanza ya mradi huo ulihusisha kata 52, ambao ulitekelezwa mwaka 2013 na umekamilika kwa asilimia 99.05 na awamu ya pili ilihusisha kata 86 na ulitakiwa kukamilika mwaka jana na hadi sasa umetekelezwa kwa asilimia 50.

“Awamu ya kwanza kuna kata nne kati ya 52 ambazo bado hazijamazilizika, jambo ambalo halikubaliki na kama mtu ameshindwa kutekeleza mkataba wake afungiwe na katika hili sitakubali,” alisema.

Mkataba wa mradi huo ambao utahusisha kata 102 na kugharimu sh. bilioni 14.02 umesainiwa kati ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCAF) na kampuni za utoaji huduma za mawasiliano.

Kampuni zilizotia saini mkataba wa utoaji huduma ya mawasiliano kwa awamu ya tatu na idadi ya kata katika mabano ni Tigo (42), Vodacom (36), TTCL (19) na Airtel (5).

Alisema bado kuna changamoto kubwa ya mawasiliano katika maeneo ya vijijini, hivyo kuzitaka kampuni hizo kuhakikisha zinatekeleza mikataba ili kila mwananchi apate huduma popote alipo.

Waziri huyo alisema katika kuhakikisha huduma ya mawasiliano inawafikia wananchi wote, serikali ilianzisha utoaji wa ruzuku kwa kampuni zinazotoa husika ili kupeleka mawasiliano kwenye maeneo yenye uchumi hafifu.

Alisema serikali kupitia UCAF itatoa ruzuku ya asilimia 100 ambayo inatolewa kulingana na eneo yakiwemo maeneo ya mipakani ambayo ni lazima yawe na mawasiliano wakati wote ili kuimarisha ulinzi na usalama.

Alisema UCAF ilianzishwa mwaka 2006 ambapo hadi mwaka 2010 anaingia katika wizara hiyo hakukuwa na kazi yoyote iliyotekelezwa ambapo alilazimika kubadilisha uongozi jambo ambalo limeleta mafanikio na sasa mawasiliano yanaendelea kufika kwa wananchi.

“Ni mafanikio makubwa yaliyopatikana itakuwa kichekesho kwa waziri atakayekuja ashindwe kufanya vizuri zaidi, na akishindwa kuna tatizo kwa sababu sasa teknolojia imebadilika,” alisema.

Awali, Mtendaji Mkuu wa UCAF, Mhandisi Peter Ulanga, alisema mbali na kutia saini mkataba na kamapuni za mawasiliano, pia waliingia mkataba na kamapuni ya Avanti inayotoa huduma za mtandao wa intaneti kwa ajili ya kuziunganishia shule 250 za serikali.

Pia alisema wataanzisha vituo 25 vya kufundishia walimu wa masomo ya teknolojia ya habari na mawasiliano, mradi unaotarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya UCAF, Profesa John Nkoma, aliwaomba wananchi wabadilike na kutumia huduma ya intaneti kwa faida na si vinginevyo.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dk. John Mngodo, alisema huduma ya kuunganisha intaneti katika shule za serikali itasaidia kuboresha elimu.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top