Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

HAYA NDIYO MAPENZI YA KWELI YA KUFA NA KUZIKANA.

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
SEHEMU YA TANO
Baada ya kukumbatiana kwa muda wa dakika mbili hivi, waliachiana na kuangaliana kwa chati. Kila mmoja alikua haamini macho yake kwa kile alichokiona. “karibu ndani.” Aliongea Zakaria na kumuangalia Aisha ambaye hakuwa na usemi zaidi ya kumfuata Zakaria aingiapo.


Waliingia mpaka ndani na kwa bahati mbaya umeme haukuwepo pale nyumbani. “tutafute sehemu nyingine tulivu, hapa hapafai tena.” Aliongea Zakaria na kumuangalia Aisha ambaye alikuwa hana usemi wowote kwa wakati huo.

Walitoka na kwenda sehemu tulivu kwa ajili ya kuongea mawili matatu. “unajua mpaka muda huu siamini macho yangu kuwa ni wewe ndiye ninayeongea nawe!” aliongea Zakaria baada ya kutulia kwa muda mahali hapo walipoweka kambi ya muda mfupi. “kwanini?” aliuliza Aisha huku uso wake ukiwa umejawa tabasamu.

“unajua nilienda mpaka Morogoro kukutafuta lakini nikakukosa. Nikaambiwa kuwa toka mama yako wa hiyari afariki tu na wewe ukatoweka pale” aliongea Zakaria na kumuangalia Aisha ambaye alikua makini kumsikiliza. “ni kweli zakaria, niliamua kuja huku mjini kukutafuta wewe mpenzi wangu.” 

Alifunguka Aisha bila kujali kuwa kwa sasa alikua na mtu mwingine ambaye siku za ndoa yao zilikua zinahesabika. “kusema ukweli mpaka hivi sasa bado sijachukua uamuzi wa kuwa na mwanamke mwingine japokuwa nilishakata tamaa ya kukutana na wewe tena.

Sijui wewe mwenzangu umeshanitoa moyoni?” aliuliza Zakaria huku akijaribu kuonyesha hisia zake juu ya mpenzi wake huyo waliyepotezana muda mrefu sana. Aisha alipatwa na kitu cha ajabu kilichosoma ubongoni haraka na kumpa maamuzi ya kuivua pete ya uchumba aliyovalishwa na Jack kwa siri hali iliyofanya tukio hilo lisionekane na Zakaria ambaye hakuwa makini sana kumchunguza.

“hata mimi, nimekutafuta bila mafanikio kwa muda mrefu. Japokuwa nilikata tamaa kukutana na wewe tena, ila moyo wangu umekuwa mgumu sana kumkubali mwanaume yeyeto zaidi yako wewe Zakaria” Alijikuta Aisha anaongea maneno hayo bila kujali kuwa anatengeneza tukio litakalomuumiza mtu asiyekuwa na hatia katika tasnia ya mapenzi.

Aliongea maneno hayo na kumtazama Zakaria ambaye muda huo alikuwa ametabasamu huku akoionyesha wazi kuyafurahia maneno yake. “woooooh… ahsante Mungu.” Aliongea maneno hayo Zakaria na kunyanyuka. Akamfuata Aisha alipokaa na kumyanyua.

Bila kuchelewa akamkumbatia na kuanza kumpa mabusu yasiyokuwa na idadi. Masaa yalisogea kwa kasi hadi kufikia saa tatu usiku bila ya Aisha kuonekana katika macho ya Jack. Hali ya wasi wasi iliwatanda Mack na kaka yake kwa kuhofia usalama wa Aisha. Kwa mara kadhaa walipiga simu ya Aisha na haikupokelewa.

Na baadae haikupatikana kabisa. Hali hiyo ilizidi kuwachanganya sana. Hawakuwa na raha muda wote walipokuwa wamejipanga sebuleni kumsubiri Aisha. “kwani alivyokuaga kuwa anaenda saloon, hakusema kuwa atapitia sehemu yoyote?” aliuliza Jack huku akionyesha ishara zote za kuchanganyikiwa kutokana na tukio hilo ambalo ni mara ya kwanza kutokea. 

“hakuniambia kua atapitia mahali popote, zaidi ya kuniambia kuwa anaenda saluni kuseti nywele zake.” Alijibu Mack “wewe unapajua huko saloon?” aliuliza Jack huku akiwa hatulii sehemu moja. Alikuwa anatembea tembea huku akikizunguka kile kiti alichokalia Mack na kutafuta kitu cha maana alichokuwa anakifuatilia.

Kila dakika alitupa macho yake kwenye saa ya ukutani ambayo ilikuwa inajitahidi kumuhesabia sekunde na dakika ambazo zilimsomea kuwa mpaka wakati huo saa nne juu ya alama ilikuwa imeshagota. “mambo ya wanawake brother mi nitayajulia wapi?

sijui ni wapi atakuwa ameenda.” Aliongea mdogo wake Jack na kumfanya kaka yake akae kwenye ngazi ya kuelekea chumbani badala ya kwenye sofa. Tai aliiona inamkaba, aliilegeza kidogo na kuamua kusubiri muda atakaorudi Aisha. 

Honi za gari zilizokuwa zikilia muda huo getini ndizo zilizomshtua na kumuamsha Jack pale alipokaa na kwenda nje na kufungua geti. Aliiona gari ya Aisha ikiwa nje, alifungua geti na Aisha aliingiza gari ndani na kwenda kupaki mahala pake. 

Baada ya hapo, alishuka na kuingia ndani, alimsalimia shemeji yake na kupitiliza chumbani kwake. Jack alimfuata Aisha chumbani na kumkuta anasaula nguo kwa ajili ya kulala. “kimekupata nini mke wangu mpaka unarudi muda huu?” aliuliza Jack baada ya kuingia tu ndani. 

“kuna sehemu nilienda, so foleni na ukijumlisha sikuenda muda mrefu ndio maana nimechelewa kurudi.” Alijibu Aisha kwa kujiamini na kuonyesha wazi kuwa haoni kama alikua ana kosa. “ndio hata kupiga simu angalau kutujulisha basi kwamba utachelewa?” aliongea Jack baada ya kutoridhishwa na jibu la Aisha. 

“simu yangu ilikata chaji.” Alijibu Aisha huku akiendelea kuvua nguo zake. “mbona nilipokupigia simu kwa mara kadhaa ilikua inaita bila ya wewe kuipokea?” bado Jack aliendelea kumbana Aisha kwa maswali yalimgusa Aisha kwa wakati huo. “naomba tulale Jack, maana fikira zako zinafikiria mbali sana.
Kwani huniamini?” Aisha alikwepa kujibu lile swali na kumgeuzia kibao Jack na kumuuliza yeye. “kukuamini nakuamini, tena sana tu. Ila kitendo ulichokifanya leo sijakifurahia.” Aliongea Jack kwa sauti ya upole kama yeye mwenyewe na muonekano wake ulivyo. “basi, nisamehe mume wangu.

Njoo tulale basi.” Aliongea Aisha na kumfuata Jack alipo na kuanza kumvua shati na tai. Siku ya pili yake, Jack alienda kazini kama kawaida, huko alipata kazi ambayo ita mlazimu kuchelewa kurudi nyumbani. Alichukua simu yake na kumpa Taarifa hiyo Aisha. Mishale ya saa mbili usiku, mlio wa simu ya Aisha ulimshtua alipokuwa jikoni anapika na kwenda kuipokea ile simu.

“niambie mpenzi wangu.” Iliongea sauti upande wapili baada ya simu yake kupokelewa. “safi tu. Mzima wewe?” aliongea Aisha huku akiangaza huku na huko ili ahakikishe usalama kwa kua mdogo wake Jack aliokua nyumbani. “njoo basi jamani, maana nahisi kitanda kimekuwa kikubwa sana usiku huu.” 

Aliongea mtu huyo maneno yaliyomshtua kidogo Aisha. “mpenzi wangu Zakaria, unanipa mtihani mwenzako. Sijawahi hata siku moja kulala nje ya nyumba hii. Unafikiri watanifikiriaje?” aliongea Aisha kwa sauti ndogo lakini iliyosikika vizuri kwenye masikio ya Zakaria. “we waambie tu ndugu zako kuwa leo unaenda kwa mumeo.

Na wakitaka kuniona hata kesho nikiwa nakurudisha wataniona. Kwani kuna tatizo hapo. Njoo bwana.” Aliongea Zakaria na kumfanya Aisha ashushe pumzi. “ngoja nijaribu.. sijui lakini.” Aliongea Aisha huku akionyesha kutokuwa na jibu sahihi. “nakuaminia, kama kweli unanipenda na nguvu yetu ya mapenzi bado ipo, basi utakuja kwakua tumefanya mengi makubwa na ya kushangaza kuliko hili.

”Aliongea Zakaria. “sawa, nikukute kituoni basi, maana leo sichukui gari.” Aliongea Aisha na kuonyesha kuwa alikua tayari kufanya hivyo. “poa, nakuja muda huu. Nipe dakika ishirini tu.” Aliongea zakaria na kukata simu. Aisha aliipua chakula ambacho kilikuwa tayari kimeshaiva. 

Akaingia bafuni na kuoga. Kwa haraka alichagua nguo zilizomkaa vizuri na kutinga. Wakati anajipamba kwenye dressing table, simu yake ikaita tena. “nimeshafika tayari.” Aliongea Zakaria baada ya simu yake kupokelewa. “nakuja, nipe dakika tano tu.” 

Alijibu Aisha na kuongeza spidi katika kujipamba kwake. Alitoka sebuleni kwa kunyata. Alifurahi kutomuona shemeji yake sebuleni. Huku akiwa ameshika viatu vyake, aliufikia mlango kwa style hiyo ya kunyata na kuanza kuufungua mlango huo taratibu. Hamadi! Alichokiona mbele yake hakuamini, alikua Jack yupo mlangoni kama vile alikua anamsubiria yeye amfungulie mlango.

 “UNAENDA WAPI USIKU HUU??” Aisha alikutana na swali hilo ambalo alishindwa kulijibu zaidi ya kutumbua tu macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.

ITAENDELEA SEHEMU YA SITA....……….


Jiunge na mi kwa kubonyeza kwenye link zifuatazo chini ili kupata habari mpya zaidi. 

        FACEBOOK >>> TWITTER  >>> MATUKIO KWA NJIA YA SAUTI
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top