Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

NINI MAANA YA HISA?? BOFYA HAPA KUJUA MAANA YAKE NA JINSI INAVYOWAPATIA WATU VIPATO

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Unapomiliki   au kuwa  na  wazo  la  kumiliki  kampuni  ni  vema  pia kujitahidi  kujua  mambo  kadhaa  yanayohusu  kampuni.  Kampuni  kama kampuni  inayo  mambo  mengi  sana. Katika  hayo mengi  si  lazima  ujue yote  isipokuwa yafaa ujue japo   machache   ya  msingi   ili upate ufanisi  wa kuendesha  kampuni.  Wengi  waliofungua  makampuni  hawajui   hata  mambo  madogo  yanayohusu   kampuni  na  uendeshaji  wake . Unamkuta  mtu  anamiliki  kampuni  kwa  mwaka  wa  tano  lakini  hajui  nini maana  ya hata  neno  Limited( LTD) ambalo  limeandikwa  kwenye  kampuni  yake.

Hii  ni  tofauti na  wenzetu    wazungu  ambao   hujishughulisha  na  kujua  mambo  ya  msingi   katika  shughuli  zao  mbalimbali  wanazoziendesha.  Kutokana  na hili  nimekuwa  nikieleza  mara  kwa  mara  baadhi  ya mambo  ya  msingi kuhusu kampuni.  Nakumbuka   nimewahi  kueleza namna  ya kuunda kampuni,  maana ya neno  limited,  namna  ya  kuandaa  mahesabu  ya  kampuni, jinsi  ya  kununua  na  kuuza hisa,   na  mengine  mengi. Kwa  anayetaka kuyaona  haya  atembelee  SHERIA  YAKUB  BLOG. Leo  tena  naeleza   kitu  kingine  ambacho  ni, Maana  ya  hisa  na  aina  zake ( shares) .

1.NINI  MAANA  YA  HISA.

Hisa ni  maslahi  ya  kila  mwanahisa  aliyonayo katika  kampuni  fulani. Yaani  wewe  kama ni  mwanahisa  katika  kampuni fulani  basi   yale  maslahi  yako au  kiwango chako  cha  uwekezaji  ulichowekeza  katika  ile  kampuni   ndio  hisa zako. Kama  mko  watu  kumi  katika  kampuni  basi  kila  mtu  ana  maslahi  au  kiwango kadhaa cha uwekezaji ambapo ukikusanya uwekezaji  huo  kwa  pamoja  ndio  utaitwa  hisa  za  kampuni.  Uwekezaji  au  maslahi  katika  kampuni  hutofautiana kutokana na  uwezo  wa  kila  mwanahisa.

Tofauti  hutokana  na kiwango  cha  kila  mtu  alichowekeza. Kuna  mwenye hisa  kumi, kuna  mwenye   ishirini,  kuna  mwenye  hisa mia n.k.  Hisa  siku  zote  hupimwa  kwa kiwango  cha  pesa.  Yawezekana  uwekezaji  wa  mtu kwenye  kampuni  ni magari  yaani  amepata hisa  kwa  kuchangia  magari.  Mwingine  amepata  hisa  kwa  kuchangia   ofisi.  Na mwingine   amepata  hisa  kwa  kuchangia  vifaa   vyote  vya  ofisi.  Katika  kuhesabu  hisa  michango  hii   yote  itawekwa  katika   viwango  vya  pesa  na  itasemwa  kuwa  fulani  ana  hisa  za  shilingi  kadhaa  na  sio  ana hisa  za  magari au vifaa  kadhaa.  Kwa  hiyo  hisa  huhesabiwa  kwa  mtindo/viwango   vya  fedha.

 2.   AINA  ZA  HISA.

Hisa  sio  hisa   kama  wengi  tunavyojua  isipokuwa  hisa  zina  aina  zake. Sio  kila  mwenye  hisa  ana  hisa  isipokuwa  ana  hisa  gani  au  za  aina  gani. Aina  za hisa  za mtu katika  kampuni  ndio  humwezesha  kujua  ana  haki  gani  katika  kampuni, ana  wajibu  gani   na anawajibikaje  likitokea  tatizo. Kwa  hiyo  haki,  wajibu(duty)   na  uwajibikaji(liability)  katika  kampuni  hutofautiana  kutoka  mwanahisa  mmoja  hadi  mwingine  kutokana  na  aina  za  hisa anazomiliki.  Wanahisa  wote  hawana  haki  sawa,  hawana  wajibu  sawa  na  hawawajibika  sawa  pamoja  na kuwa  katika  kampuni  moja. Hapa chini tutaona   aina  za  hisa.

( a  )  HISA  ZA  WAMILIKI  ( EQUITY  SHARES).

Hizi  ni  aina  za  hisa  ambazo  huwa  ndio  nyingi  katika  kampuni. Wale  wanaomiliki  hisa  nyingi   katika  kampuni  hisa  zao  huitwa  hisa  za  wamiliki.  Huitwa  hisa  za  wamiliki  kwakuwa   hawa  huhesabika  kama  ndio   kampuni  yenyewe  na  hivyo  wenye  hisa  hizo  ndio  wamiliki  wa kampuni.  Nimesema  hapo  juu  kuwa  wanahisa  hawana haki  sawa, wajibu  pamoja  na  uwajibikaji.  Wenye  hisa  hizi  wana  haki  kubwa  ya  kimaamuzi  katika  shughuli  zote  za  uendeshaji  wa kampuni   kwakuwa  wao  kila  hisa  moja  huwa  ni  kura  moja  na  kwahiyo  kila  kitu  hupitishwa  kwa  kura  zao.  Pia  wana  haki ya  kupata  mgao  mkubwa  kuliko  wengine. Hata  hivyo  wanawajibika  zaidi  linapotokea  tatizo  kwa  mfano   inapotokea  hasara  wao  ndio  hupoteza  zaidi. Kwa  jina  jingine  hisa  za  hawa  huitwa   HISA  ZA    SIMBA( LIONS  SHARE). Hii  ni  kwasababu  huko  mwituni  simba  hupata  mgao  mkubwa wa  nyama kati  ya  wanyama  wote.

( b ) HISA  ZA  KAWAIDA.

Hizi  ni  zile  hisa  ambazo  humilikiwa  na  watu  wengine   wa  kawaida  katika  kampuni. Mara  nyingi  hawa  ndio  huwa  wengi  japo  kila  mtu  huwa  na hisa  kidogo kidogo. Mgao  wao  wa  faida  hutokana  na asilimia  ya  kile  mtu  anachomiliki. Maamuzi  yao  katika  kampuni  huwa  ni   madogo ukilinganisha  na  wenye  zile hisa  za  umiliki( equity shares). Hata  hivyo  uwajibikaji  wao  nao ni  mdogo pia kwani hupata  hasara  kidogo  pale  kampuni  inapopata  hasara.  Pamoja  na  hayo  sheria  imewapa  kipaumbele  cha  kupewa  mgao  wa faida kabla  ya  kundi  jingine  lolote.

( c ) HISA  ZA  WAANZILISHI ( DEFERRED  SHARES).

Hizi ni  hisa  ambazo  hutolewa  kama  zawadi kwa  waanzilishi  wa kampuni. Mgao  wa  faida  wa hisa hizi  huwa  sio wa  moja  kwa  moja isipokuwa  hutegemea   na  faida  inayozidi. Kawaida mgao  wa  faida   kwa  wanahisa  wengine  hutoka  katika   faida   ya  kawaida lakini  hawa  hawapewi  mgao  kutoka  faida  ya  kawaida  isipokuwa   hupata  pale  faida  inapozidi  au  kuvuka  kiwango ilichotegemewa.

 ( d ) HISA  ZA  KAMPUNI( CORPORATE  SHARES).

Zote  nilizotaja  juu ni  hisa  za  kampuni  lakini  bado  jina  hili hupewa  hisa  hizi  kutokana  na  kuwa  ni  hisa  maalum  ambazo  hutolewa  kwa  waajiriwa/wafanyakazi  katika  kampuni  husika. Waajiriwa  hutengewa hisa  zao  na  mwenye  uwezo  huweza  kuchukua  hisa  hizo  kwa  kiwango  cha  uwezo  wake.  Mwajiriwa huendelea  kuwa  na  hisa   hizo hata  baada  ya  utumishi  wake  kukoma .  Kwa  ufupi  sana  niseme  tu  kuwa  hisa  sio  hisa  ila  hisa  ni  una  hisa  za  aina  gani Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top