Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

Mvua kubwa ambayo imeambatana na upepo mkali, yasababisha maafa makubwa mkoani Mara

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Mvua kubwa ambayo imeambatana na upepo mkali, imesababisha maafa makubwa katika vijiji vitatu vya wilaya ya Butiama mkoani Mara na kusababisha nyumba za kaya zaidi ya mia moja zikiwemo nyumba za ibada kubomolewa vibaya na mvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali, huku idadi kubwa ya ekari za mashamba yenye mazao mbalimbali pia yakiathiriwa na mawe yaliambatana na mvua hiyo.

Akizungumza baada ya kukagua athari ambayo imesababishwa na mvua hiyo, mwenyekiti wa kamati ya maafa ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama Bi Annarose Nyamubi, akiwa ameambatana na mwenyekiti wa halmashauri ya Butiama Bw Magina Magesa, wamesema mvua hiyo imesababisha madhara makubwa na kwamba watendaji wa serikali wameanza kufanya tathimini ya kina ili kujua ukubwa wa maafa hayo

Naye diwani wa kata ya Butuguri Bw. Paul Warati, akizungumzia maafa hayo, amesema tathimini ya awali inaonyesha kuwa zaidi ya kaya mia moja,majengo ya taasisi, chakula na mazao mashambani zimeathirika na mvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top