Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WATOZWA FAINI YA MILLIONS 7 KISA KUTOFANYA USAFI KILA JUMA MOSI

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Wakazi wa manispaa ya Sumbawanga ikiwa ni pamoja na wamiliki wa Hoteli, Migahawa, Bar na nyumba za kulala wageni, wamejikuta wakikumbwa na mzigo wa kulipa faini ya zaidi ya shilingi milioni saba, baada ya kupatikana na makosa ya uvunjaji wa sheria ya usafi wa mazingira, na kukaidi agizo la Rais la kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.

Mkurugenzi wa manispaa ya Sumbawanga Bw Hamid Njovu, akiongea mjini Sumbawanga amesema manispaa hiyo inatarajia kuwafikisha mahakamani wakazi wanne ambao wameshindwa kulipa faini ya shilingi elfu 50 kila mmoja, na kwamba zoezi hilo la usafi wa mazingira ni endelevu na la kudumu, na kwamba wakazi wote wanatakiwa kushiriki usafi siku hiyo ya jumamosi kuanzia saa moja hadi saa nne asubuhi na shughuli zote zikiwa zimefungwa.

Akiongelea kuhusu suala la usafi kwenye manispaa hiyo ya Sumbawanga, afisa usafi na mazingira Bw. Hamidu Masare amesema mji huo unaweza kuzalisha kati ya tani 80 hadi 90 za taka ngumu kwa siku, na kwamba halmashauri hiyo ina uwezo wa kuzoa zaidi ya tani 100 kama magari yote matatu yakiwa katika hali nzuri, hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi zima la usafi wa mazingira.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top