Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WATAKAO KIUKA MATUMIZI YA NJIA YA MABASI YA MWENDO KASI WACHUKULIWE HATUA KALI ZA KISHERIA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.


Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kutembelea barabara ya mabasi ya mwendo kasi Jijini Dar es Salaam  huku  akiagiza  kuchukuliwa hatua kali  za kisheria kwa wale watakaokiuka  kwa kufanya matumizi  ya barabara za magari hayo kinyume na utaratibu.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa Kimara mwisho mara baada ya kumaliza ziara hiyo ya kutembelea mradi wa mabasi yaendayo haraka Waziri Mkuu amesema aliamua kufanya ziara hiyo ya ghafla ili kuangalia matumizi ya njia za mabasi yakoje na pia kuona abiria wanaelewa vizuri namna ya kuitumia huduma hiyo.

Kwa nyakati tofauti wahudumu wa mradi huo pamoja na Mkurugenzi wa UDART wamemweleza Waziri Mkuu kuwa zipo changamoto mbalimbali ikiwemo matumizi ya tiketi zilizoisha muda wake pamoja na baadhi ya wananchi kutokuwa na uelewa wa mfumo unaotumika katika utoaji tiketi hizo pamoja na utekelezaji wa mradi huo.

Waziri Mkuu Mh Majaliwa ametoa onyo hilo kwa  waendesha pikipiki, magari na watembea kwa miguu kuacha kukatiza hovyo na kusababisha ajali ambazo zinaweza kuzuilika huku akitaka kikosi cha usalama barabarani  kusimamia zoezi lautekelezaji agizo hilo hasa kwa wale wanaokuwa wakilala katika vivuko vya mabasi hayo hasa nyakati za usiku.

Katika hatua nyingine Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani amewataka wananchi kutii sheria bila shuruti ikiwa pamoja na kufuata taratibu zinazotakiwa katika matumizi ya barabara hizo pamoja na vivuko ili kuondoa usumbufu kwa watumiaji wengine, huku baadhi ya mashuhuda wa ziara hiyo wakipongeza hatua hiyo.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top