Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UCHIMBAJI WA MAFUTA NA GESI WAANZA VISIWANI ZANZIBAR, KUJUA ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeanza harakati za kutafuta utaalamu wa uchimbaji wa mafuta na gesi ambapo wataalamu mbalimbali wa serikali wameanza kupatiwa taaluma hiyo kimataifa.

Akifungua mkutano maalum wa wadau wa sekta ya nishati ambao umeandaliwa kwa pamoja kati ya mamlaka ya usafiri baharini na serikali ya Norway kupitia taasisi yake ya uchimbaji wa mafuta baharini naibu katibu mkuu wa wizara ya ujenzi, mawasialino na usafirishaji wa Zanzibar Shomari Omar Shomari amesema sasa ni wakati muafaka kwa Zanzibar kujipanga kwa sekta hiyo kwa vile matarajio ya kupata nishati  hizo zipo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa mamlaka ya usafiri baharini  Abdi Omar Maalim amesema mkutano huo utawawezesha wadau kupata mbinu za kujiandaa na athari za mafuta baharini huku baadhi ya washiriki wakiwemo wa sekta ya ulinzi wa bahari na uchimbani wa mafuta wamesema wameanza kupata mwelekeo wa hali ya nchi inapokabiliwa na ajali zozote za bahari zianzotokana na mafuta na gesi.

Wataalamu hao watatu wa Norway kwa siku mbili wanatarajiwa kutoa mwelekeo na mbinu za kupambana na uharibifu wa mazingira baharini unaotokana na uchimbaji wa mafuta na gesi na mikakati ya kupambana nayo.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top