Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KUWASHINDANISHA WAWEKEZAJI NDIO NJIA BORA , ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Serikali imesema ushindani kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika sekta ya nishati, ndiyo njia bora zaidi itakayowezesha kuwapata wawekezaji wenye vigezo vinavyotakiwa.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliyasema hayo jana, Mei 10, alipokutana na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KOYO kutoka Japan, Norio Shoji na Ujumbe wake, ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika uzalishaji na usafirishaji wa umeme nchini, kwa kutumia vyanzo mbalimbali ikiwemo gesi asilia na jua.

“Kampuni nyingi zimeonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya nishati. Serikali inao uhitaji mkubwa wa wawekezaji walio makini, hivyo tunahitaji kuwapata wawekezaji wenye vigezo kwa kutumia ushindani unaozingatia uwazi,” alisisitiza Profesa Muhongo.

Aliongeza kuwa, ili kuwarahisishia wawekezaji wenye nia ya kuwekeza katika sekta ya nishati nchini, Wizara inaandaa taarifa maalum itakayobainisha maeneo yanayohitaji uwekezaji pamoja na vipaumbele vyake.

Alisema, taarifa hiyo itakuwa tayari na kutolewa mwishoni mwa mwezi huu (Mei 31, 2016) na kwamba itasambazwa kwa wadau wote wa ndani na nje ya nchi kupitia njia mbalimbali za mawasiliano, ikiwamo tovuti ya wizara.

Profesa Muhongo alieleza kuwa, taarifa hiyo pamoja na mambo mengine, itawapa fursa wawekezaji wenye nia, kuchagua aina ya uwekezaji wanaohitaji kufanya na katika maeneo ambayo wanadhani watakuwa na uwezo wa kumudu ushindani kutoka kwa wawekezaji wenzao kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Akifafanua zaidi, Profesa Muhongo alisema kuwa, zoezi la kuwashindanisha wawekezaji walioonesha nia, litakuwa ni endelevu na litakuwa likifanyika kila baada ya muda fulani, ambao utabainishwa katika taarifa husika inayotarajiwa kutolewa.

Akitoa mfano, alisema kuwa, siyo lazima kumpata mwekezaji katika zoezi la ushindanishaji, hivyo ni muhimu zoezi liwe endelevu ili kuweza kutoa fursa kwa wawekezaji wengi zaidi kushiriki na hivyo kumpata mwekezaji mwenye vigezo vyote ambavyo Serikali inavihitaji.

“Endapo tutaendesha zoezi la ushindanishaji wawekezaji na wote walioshindanishwa wasipotimiza vigezo vinavyotakiwa, hatulazimiki kumchukua yeyote tu. Tutakachofanya ni kutokumchukua yeyote kati yao na hivyo kuendelea na zoezi hilo baada ya muda tutakaoubainisha, hadi pale tutakapowapata wawekezaji wenye vigezo tunavyovitaka.”

Profesa Muhongo alibainisha kuwa, mchanganyiko wa nishati ambao Serikali imekusudia kuutumia kama vyanzo vya kuzalisha umeme nchini kwa sasa ni pamoja na gesi asilia, maji, upepo, jua, makaa ya mawe, mvuke (maji moto) na tungamotaka.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top