Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

BOFYA HAPA=> KAMA HUKUMSIKILIZA RAIS ALIPO ONGEA NA WAZEE

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Napenda niwahakikishie wazee na watanzania kwa ujumla, hatutawaangusha. Kwa niaba ya viongozi wenzangu, nawaahidi tutawanyia kazi, ninachowaomba wzee na watanzania kwa ujumla, mtuamini.

Katika shughuli zozote za kufanya mabadiliko huwa kuna changamoto zake, watakaoguswa ni wachache sana kwa ajili ya watanzania wote hasa maskini.

Haipaswi kuwa maskini, Tanzania hii ina utajiri wa kila aina, haipaswi kuwa na wanafunzi wanaokaa chini, watu wanaolala chini mahospitalini.

Lakini ni lazima tujue wapo watu wachache waliotufikisha hapa, mlituchagua kwa mioyo yenu wote, ndio maana nasema kwa dhati naomba mtuamini kwa sababu tunaamini tukiyatekeleza haya, nchi hii itakuwa ya mfano Afrika kama si duniani kwa ujumla.

Mimi na serikali yangu tumejitoa sadaka kwa ajili ya watanzania, tunaomba muendelee kutupa nguvu ili haya matamanio yetu kwa ajili ya Tanzania yoyote tena kwa hara.

Yoyote atakaejaribu kutukwamisha serikalini tutambomoa kwa ajili ya watanzania.

Wapo watu kwao pesa si tatizo na angalau wangezipata kihalali, lakini ni za wananchi wenye hali mbaya sana Kilometa moja imejengwa kwa bilioni mbili tena ni barabara ya halmashauri, nimekaa serikalini miaka 20 na sijawahi kutengeneza barabara kuu, kilometa moja kwa bilioni mbili lakini barabara ya halmashauri tena ya Bariadi inatengenezwa kwa mabilioni ya shilingi zilizokuwa zinatoisha kutengeneza zaidi ya kilomita 20

Waziri alienda kuangalia mafuta, PUMA na ORLX serikali ina share ya asilimia 50. Flow meter ambayo ndio inapima mafuta kiasi gani yanaingia nchini hakifanyi kazi miaka mitano na Dar es Salaam kila kona sheli.

Nilikutana na wakina mama wakaniambia twende ukaone, nilishaenda lakini ilikuwa upande mwingine, wasaidizi wangu wakaniambia usiende lakini nikaenda.

Nikakuta maji ya kutoka chooni yanaingia, wakina mama wamelala chini wakati kuna jengo linajengwa tangu awamu ya mzee Mwinyi halijaisha mpaka leo.

Wazee tunapochukua hatua, sisi si wakatili sana, tunawawakisha nyinyi uchungu wenu. Ninafahamu mawaziri wangu wanafanya kazi nzuri. Ninawapa muda na nyinyi muwape muda na mimi mnipe muda.

Lile jengo linalotumika kama ofisi ya uzazi wa mpango wahame na waziri atajua atawapeleka wapi tena ofisi kama ya waziri, anaweza kwenda kukaa nao ofosini kwake, wale kina mama waliokuwa wanalala chini wahamie hapo.
Ninawaomba katika kipindi hiki cha mpito mtuvumilie, majipu tutayambua kweli kweli.

Tanzania haiwezi kwenda mbele bila kuwa na fedha zake, wafanyabiashara wanakwepa sana kodi. Tunataka fedha tunazozikusanya ziende kuwasaidia watanzania wa hali ya chini.

Zipo kejeli nyingi kuwa ni nguvu ya soda, hata kama ni soda ukiweka gongo utalewa, kwa hio hii ni soda special.

Tumeweka bilioni 200 kwa ajili ya daraja la Coco beach hadi Agha Khan, barabara ya kutoka Rangi tatu pia tumeitengea fedha na interchange ya ghorofa tatu pale Ubungo.

Shirika la ndege tunataka kulifufua ndio maana tunachukua hatua mbalimbali. Yuko mmoja ameshikwa pale alikuwa anataka kubadilisha fedha kwenye akaunti tukamkamata, hatutaki kusema mengi kwa sababu hatua zinachukuliwa ikiwemo za kimahakama.

Watanzania tujifunze kulipa kodi, chochote unachoenda kununua omba risiti. Kuna sehemu inatakiwa kubaki kwa ajili ya kuhudumia watu.

Nimemuona Makonda akihamasisha, limekujengea heshima kubwa kwa hio ukipanda hata cheo, watu wasikuonee kwa sababu you deserve it.

Kwa sababu na sisi tunakaa Dar, nilikuwa nazungumza na makamu na waziri mkuu. Tunaokaa Dar ikiwemo mawaziri na makati wakuu, nikasema kwa sababu wakati nafanya uteuzi na hawakuniomba, nikiwaambia leo watoe milioni moja moja ni vibaya? Tunakusanya milioni 80 bado kuna mimi, kisha tutatenga bilioni mbili tuzigawe hizo fedha Dar ili zikajengwe hizo shule.

Michango ni hiari, pasitokee watu kupitia hii hotuba wakaanza kulazimisha watu, watakaoguswa kuchangia wachangie.

Najua sijateua wakuu wa mikoa, ma-DC na wakurugenzi, nimefanya makusudi ili niendelee kuchangia nani anatosha na nani hatoshi, kutosha kwao ni kutatua kero za wananchi.

Yapo magazeti mengine wanaandika mpaka unashangaa, unajiuliza yakitokea machafuko wana mahali pa kwenda kukaa. Nayapongeza magazeti mengi mfano gazeti la Jamhuri lilivoenda kufufua uozo wa Flow meter.

Kuhusu Zanzibar, kama tume za uchaguzi nyingi duniani, haiwezi kuingiliwa na Rais yeyote ndiyo maana tume za uchaguzi huwa huru.

Napenda kuheshimu sheria lwa hio ZEC ina uhuru wa kuamua mambo yake lakini kama kuna tafsiri mbaya, waende mahakamani, mahakama ziko pale halafu unamwambia Magufuli ingilia.

Jukumu langu kama amiri jeshi mkuu ni kuhakikisha amani ya Zanzibar inaimarika, yeyote atakaeleta fyoko fyko ajue vyombo vya usalama vipo.

Kwa niaba ya serikali ninayoiongoza, sisi tuko makini, niwahakikishie tutaweza na Tanzania tutaivusha, itaenda mbele kwa ajili ya maendeleo ya watanzania wote.

Naomba wazee wangu na watanzania kwa ujumla mtuombee, wanaolalamika wachache muwapuuze kwa sababu ni miongoni ya waliofaidi matunda ya wanyonge kwa miaka ya nyuma.

Niwahakikishie wafanyabiashara tuko pamoja nao katika biashara zao zote halali, na wafanyabiashara watanzania huu ni wakati wao, taifa haliwezi kujengwa na watu kutoka nje.

Tunataka Tanzania iende mbele kwa ajili ya watanzania wote.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top