Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WATUHUMIWA 3 WA TRA KUPEWA DHAMANA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
MTANZANIA. Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imeridhia kutoa dhamana kwa watuhumiwa watatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuwataka kila mmoja kutoa fedha taslimu Sh bilioni 2.6.

Akisoma uamuzi huo jana, Jaji Winfrida Koroso, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Tiagi Masamaki (56) ambaye ni Kamishna wa Forodha wa mamlaka hiyo, Burton Mponezya na Habibu Mponezya ambaye ni Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja.

Alisema kabla ya kutoa dhamana hiyo, mahakama hiyo imepitia maelezo ya pande zote mbili ambazo ni upande wa washtakiwa na wa Serikali ili kuangalia kama watuhumiwa hao wana vigezo vya kupewa dhamana.

Jaji Koroso alisema baada ya kupitia maelezo hayo, mahakama iliridhia kuwapatia dhamana hiyo, huku ikiwataka kutimiza masharti sita ili waweze kukidhi vigezo.

Aliyataja masharti hayo kuwa ni kila mwombaji kulipa fedha taslimu Sh bilioni 2.6 au mali yenye thamani ya fedha hizo na kudhaminiwa na wadhamini wawili ambao ni wafanyakazi wa Serikali wenye bondi ya Sh 20 kila mmoja.

Alisema, kila mwombaji hatakiwi kusafiri bila ya kibali cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambako kesi hiyo inaendeshwa, kuwasilisha vibali vya usafiri ikiwamo paspoti katika mahakama hiyo na kuripoti mahakamani hapo kila baada ya wiki mbili siku ya Jumatatu.


Alisema masharti mengine ni kila mwombaji ahakikishe taarifa zote alizowasilisha mahakamani hapo ziwe zimesainiwa kisheria na kukamilisha taratibu za dhamana ndani ya saa 24 ili waweze kukidhi vigezo vya dhamana hiyo.

Awali, Masamaki na wenzake walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakituhumiwa kufanya makosa mawili ya uhujumu uchumi ambapo shtaka la kwanza ni kutoa makontena 329 katika Bandari ya Dar es Salaam bila ya kulipiwa kodi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh bilioni 12.7.

Katika shtaka la kwanza, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa tarehe tofauti kati ya Juni mosi na Novemba 17 mwaka huu, sehemu isiyojulikana ndani ya Jiji la Dar es Salaam, watuhumiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kuidanganya Serikali kuwa Sh bilioni 12.7 zimetolewa kwa kutoa makontena 329 katika bandari kavu ya Azam baada ya kodi zote kutolewa.

Shtaka la pili, inadaiwa kuwa Juni mosi na Novemba 17, mwaka huu ndani ya Jiji la Dar es Salaam, walishindwa kutimiza majukumu yao kwa namna inavyotakiwa na kusababisha Serikali kupata hasara ya Sh bilioni 12.7.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top