Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

RAIS KIKWETE NA KENYATTA WAZINDUA MRADI WA UJENZI WA BARABARA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na mwenzake wa Tanzania Jakaya Kikwete wamezindua mradi wa ujenzi wa barabara ya Taveta-Mwatate ambayo inatarajiwa kurahisisha uchukuzi kati ya kataifa hayo mawili.

Barabara ya Arusha-Holili upande wa Tanzania pia inakarabatiwa.
Rais Kikwete yumo nchini Kenya kwa ziara rasmi ya siku tatu na Jumanne anatarajiwa kuhutubia kikao cha pamoja cha mabunge mawili ya Kenya.

Mradi wa ujenzi wa barabara hizo mbili umefadhiliwa kwa pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika na serikali za Kenya na Tanzania.

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa kanda hii wa AfDB Gabriel Negatu benki hiyo imetoa $218 milioni za kutumiwa kwenye mradi huo, Kenya ikipokea $116 milioni na Tanzania $102 milioni.

Huo ndio mradi wa pili wa barabara wa kuunganisha Kenya na Tanzania uliofadhiliwa na benki hiyo, wa kwanza ukiwa barabara za Arusha-Namanga/Namanga-Athi River.

Rais Kikwete alisema barabara hiyo ya Taveta-Mwatate hutumiwa na wakazi wa kaskazini na kaskazini-magharibi mwa Tanzania kusafirisha bidhaa hadi Mombasa.

“Huchukua saa 14 kutoka Arusha hadi Voi. Lakini ujenzi huu ukikamilika, itachukua saa mbili na nusu pekee, hivyo kuwa nafuu sana kwa wasafiri na wenye magari,” alisema.

Kiongozi huyo, anayetarajiwa kuondoka mamlakani karibuni baada ya uchaguzi mkuu Oktoba 25, alisema barabara hiyo ina uwezo wa kuimarisha biashara kati ya Kenya na Tanzania kwa asilimia 10.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top