Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

PICHA ZA MATUKIO YA MKUTANO WA UKAWA ARUSHA JANA ZOTE ZIKO HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Rais mtarajiwa Edward Ngoyai Lowassa akiwa na Timu nzima ya UKAWA watakuwa viwanjani hapa kuanzia majira ya Saa10 Jioni.

    Endelea kufuatilia huu Uzi Kwa Updates zaidi...

    
Updates

    Mkutano ameshaanza. Mbatia anazungumza.

    Anasema Arusha imepewa heshima ya kuhutubiwa na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru.

    Anasema Ccm wameuza hisa za TBI zenye thamani ya shilingi177Bil ili zisaidie kampeni zao

    Wiki ijayo watauza tena 50% za NBC zenye dhamani ya 412bil

    Jk katumia 4trilion kwa safari za nje fedha ambazo zingetosha kujenga vyuo vya ufundi 200 kwa thamani ya bil 20 kila kimoja

    Ccm badala ya kufanya kampeni inabebwa na dola kwa kufanya haramu.

    Kikwete amefanya ccm haramu kwa kutumia fedha za watanzania kwenye kampeni

    Lowassa amesema kipaumbele chake cha kwanza hadi tatu ni elimu.

    Elimu ya Lowassa itasaidia kwa kuanzisha vyuo vya ufundi ili ziweze kumsaidia.

    Mkamate sana elimu usimwache aende zake maana ndiyo uzima wako. Maneno ya mithali

    Tarehe 25/10 tuhakikishe rais wetu ni Lowassa.. Magufuli asipate kura hata moja

 
    Mbowe:
    Naomba nimlete kwenu mgeni wenu wa siku ya leo ambaye ana kadi namba 8 ya ccm. Anataka kuzungumza na watu wa Arusha

    Watu wanashangilia babu babu babu babu babu

    Tangu ccm imeanza kampeni imefanya vituko,kampeni zao zimetawaliwa na matusi,kimepoteza dira

    Ccm haisemi sera tena bali kusema watu kwenye mikutano yao

    Lazima mtu anayesemwa sana awe ni mtu mzito sana,ndio maana watu wazima wanamsema sana

    Mimi ni mtu wa mabadiliko

 
    Ninaamini kwa dhati ya moyo wangu kuwa mabadiliko Tanzania ni sasa

    Wakati tunaanzisha TANU tulikuwa tunatafuta chombo cha kumkomboa Mtanganyika

    ASP na TANU vimefanya jitihada kubwa kuboresha maisha ya watanzania,na kwa kuwa viliamini katika mabadiliko viliungana

    Tunaendelea na mabadiliko hadi sasa,lakini katika awamu hii ya nne,kuna dalili kuwa baada ya ccm kukaa madarakani kwa nusu karne imeishiwa pumzi

    Ccm ilirithi pumzi ya asp na Tanu ila sasa pumzi imekwisha

    Mkapa alichukua kutoka kwa Mwinyi wakati uchumi ukikuwa kwa 4%

    Kikwete karithi unaokuwa kwa 7asilimia,miaka 10 baadae na kwa taarifa za serikali yenyewe uchumi unakuwa chini ya 7%

    Maana yake ni kwa miaka 10 hii tumeganda!

 
    Ili kuondoa umasikini lazima uchumi ukue kwa 10%kitaalam
    Kwa miaka kumi ccm uchumi umekuwa kwa single digit

    Uchaguzi ni kura,sio maneno

    Tarehe 25 kazi ni moja tu,unachukua kichinjio unaweka Lowasa

    Naomba marafiki zangu wa ccm,wengine tangu wakati wa kupigania uhuru,wasibabaike,sijawaacha kwa sababu nawachukia,nimeondoka kwa sababu sikubaliani na uongozi unaovunja katiba ya chama,taratibu,na kanuni.

    Uongozi unaodhalilisha wagombea Urais wa chama chao,na wanaendelea kana kwanba hakuna lililotokea

    Anaaga wanachi kwa kumtia moyo.

    Nawatakieni mafanikio katika harakati za kuleta mabadiliko

    Uwanja unalipuka Kwa kushangilia. babu babu babu babu.


    Sumaye
    Watanzania wameamua kuwa sasa ni mwaka wa mabadiliko

    Wameamua hivyo kwa kuwa ccm imeshindwa kuleta maisha bora

    Watoto hawatibiwi bure

    Ccm imeahidi vijana ajira,na kikwete aliahidi vijana kuwa tatizo la ajira litakuwa ajira,Je tatizo hilo limeisha?

    Elimu imeharibiwa na ccm

    Wananchi wanajibu kuwa hakuna haja ya kuchagua ccm tena

    Rais lazima awe mwadilifu,awe mtumishi mwema,na awe kimbilio la watu

    Kwenye mizani kuna rushwa kubwa,wizara ya magufuli imenunua bot ya miaka 30 kwa gharama ya boti mpya

 
    Wizara ya ujenzi inaongoza kwa ufisadi,Je ni Magufuli ni mwadilifu?

    Ameshindwa kupambana na ufisadi wizarani kwake ataweza kwa nchi?

    Lazima rais awe msikivu,je Magufuli ni msikivu?

    Kigamboni aliwaambia watu wapige mbizi Maana yake wafe.

    Hatutaki Rais mbambe

    Sumaye anamaliza Kwa kushangiliwa vilivyo.

    Sasa Lowassa anataka kuzungumza na Watanzania.

    Wimbo unapigwa anacheza

   
 Lowassa
    Namshukuru sana mzee Ngombale ndie aliyekuwa nguzo ya ccm,kuondoka kwake ni pigo kwa ccm

    Nimekuja kuomba kura

    Wananchi wanaitikia Kwa shangwe. Umepataaaaaaa. Uwanja mzima kelele na vifijo

 
    Wananchi wanaimba Rais Rais Rais Rais Lowassa

    Kwa huu umati ikulu nimefika

    Kwanini nagombea urais

    Nimechoshwa na umaskini

    Naomba kura nyingi ili niweze kushinda.

    Nimeomba kuwa rais kwasababu nimechoka na umaskini.

 
    Nitaanza na elimu ili kuondoa hali ya umaskini. Vipaumbele vyangu vya kwanza elimu pili elimu tatu elimu. Ukimpa mtoto wako elimu umemsaidia kimaisha. Nimesema elimu kuanzia nursery hadi chuo kikuu bure.
 
    Wanasema haiwezekani mimi nasema inawezekana kabisa tuna fedha nyingi sana nchi hii kuanzia gesi mpaka madini na utalii. Hakuna mwanafunzi kulipa mchango wa aina yoyote. Nitazingatia maslahi ya mwalimu ili awe na moyo na kazi yake.
 
    Eneo la pili ni eneo la kilimo nitaiboresha na mkulima akitaka kuuza mazao yake popote auze. Tuwape wananchi uhuru wafurahie matunda ya nchi yao wakale raha.

    Eneo la tatu ndugu zangu wa bodaboda, mama ntilie na machinga watakuwa rafiki wa serikali yangu. Naahidi nikiingia ikulu baada ya wiki moja atakayewasumbua nakula nao sahani moa. Nitaanzisha benki kwa ajili wa wamama kupata mikopo.

    Nikichaguliwa kuwa rais kila wilaya kutakuwa na hospitali za rufaa zenye vifaa vya kisasa kuwasaidia wagonjwa.

    Nimekusudia kuongoza Tanzania kwakuwa nia ninayo sababu ninayo na uwezo ninao. Serikali yangu itakuwa ya mchakamchaka

    Lema
    Kamanda Lema, Kiboko ya CCM Arusha anazungumza sasa.

    Wananchi wanamshangilia Lema Lema Jembe Jembe.

    Lema anazungumza

 
    Mh rais hawa watu ni watu wangu wananipenda nami nawapenda sana. Nimekamatwa na kuteswa kwa ajili a watu hawa, nimeenda jela kwa ajili ya watu hawa, nimejenga hospitali bado tunawapigania watu wangu.

    Nakuhakikishia tayari tuna kura laki mbili na sitini na tayari hao walikusainia wakati wa udhamini. Mh rais una kura nyingi sana.

    Nakuomba uwasiliane na Lubuva umwambie mpango wa kuchelewesha vifaa ukome tunahitaji kura za haki.


    Wakuu mkutano imeisha na watu wanaanza kuondoka viwanjani hapa.

    Ni dhahiri shahiri CCM wana kazi nzito kuanzia ngazi ya Udiwani mpaka Urais ndani na nje ya Arusha.

 
    WanaArusha wameionyesha Arusha na Tanzania kwamba Mabadiliko hayakwepeki na CCM lazima itoke.



    Shukrani za dhati ziwafikie makamanda Kwa kuwezesha Updates za Leo.

    chakii Mungi Molemo Emma sweetlady Filipo Crashwise na wengine wote walioshiriki.


    Tukutane Oktoba 25.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top