Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

JANUARY MAKAMBA AMEINGIA UKUMBINI SOMA ZAIDI

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Januari Makamba ameingia ukumbini anatoa tathmini fupi ya kampeni, anasema watanznaia waliomuona wanadadiriwa kufikia asilimi 70 na wanamuelewa na kuielewa ilani ya Chama.

Tathmini yao fupi inaonyesha kuwa atashinda kwa asilimia 66.3, anasema upande wa kampeni za Ubunge wanaendelea vizuri na Sekterieti ya CCM itaandaa utaratibu wa kutatua changamoto zilizojitokeza.

Amesema mwendendo wa kampeni hizo, umeenda sambamba na midahao, anasema John Mgufuli aliombwa kushiriki mdahao huo na amekubali na misingi hiyo kuna kauli iliyotolewa na UKAWA kupitia kwa James Mbatia ni kauli ambayo inashabiana na kile kinachojadiliwa na vyama vya siasa.

Makamba: CCM midahalo inatakiwa kuwa kati ya wagombea, wagombea wote washiriki na akikosekana yoyote katika vyama vikuu utapoteza maana.

Wote tunafahamu kura zinapigwa vituoni na zoezi la kuhesabu linafanyika mbele ya macho mengi na kwa uwazi na mawakala kwenye vituo wanatia sahihi na kuondoka na fomu zao, kila mtanzania ana fursa ya kujumlisha matokeo nchi nzima, kwenye tume pia wanajumlisha na kuna mawakala na sio sehemu ya siri.

Kauli kwamba kura zitaibiwa ni recless, tunapenda kuwasihi watanzania wasikubali vishawishi vya kufanya vurugu, wahamasishaji wa vurugu huwa wana ulinzi ama sehemu ya kukimbilia, huu ni uchaguzi wa tano na zote za kabla ziliisha kwa amani.

Baada ya uchaguzi kuna maisha, kuna taifa na lazima wote tuendelee kubaki wamoja. Tusitoe kauli zilizopitiliza, tunaendelea kuasa wagombea wa kujinadi kwa ukabila, udini na ukanda, CCM haina mpango wa kuendeleza mjadala wa kauli aliyotoa mgombea Rais Tabora. Tulitegemea UKAWA jana wangeomba radhi kwa kauli ile, CCM tunasema tunafunga mjadala

Mayage(Swali): Nahitaji tu ufafanuzi, unaongea kama nani ndani ya chama

Makamba: Nazungumza kama mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM vilevile mjumbe wa kamati ya taifa ya kampeni ya CCM, nazungumza kwa niaba ya CCM na ninayo mamlaka ya kuzungumzia mwenendo wa kampeni na mambo yote niliyoyazungumzia hapa. Kuhusu kumzungumzia mgombea Urais na si mgombea mwenza, kama mnavyofahamu kampeni inabeba mgombea Urais na kura anapigiwa mgombea Urais

Matutu(Matanzania): Mnafikiria mtapata asilimia 69.3, mnatumia vigezo gani?

Balile: UVCCM walisema watashinda kwa asilimia 80 leo asilimia 69 na UKAWA walisema 80 lakini sasa 70

Makamba: Tumewapa taasisi huru watufanyie badala ya sisi wenyewe, kuna metholodojia ya takwimu imetumika, margin of error kwetu ni asilimia tatu. Sina hakika UVCCM walitumia vigezo gani na siwezi kuwasemea UKAWA. Tunafurahi mgombea wetu anaonyesha energy na mikutano mikubwa, upepo upo upande wetu.

SOMA ZAIDI HAPA ==>> TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top