Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MWENYEKITI WA CHAMA CHA DP AGOMA KUSAINI FOMU

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Wakati Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Christopher Mtikila akigoma kusaini fomu za kugombea urais akitaka ufafanuzi wa mgombea binafsi, Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa amekwama kwenye lifti za jengo lililopo katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi (NEC) kutokana na kukatika umeme.

Mchungaji Mtikila ambaye aliambatana na mgombea mwenza Juma Metu Juma, alitaka ufafanuzi wa kutokuruhusiwa kuwania urais akiwa mgombea binafsi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) imeruhusu.

“Siondoki hapa na wala sitaweza kuchukua hizi fomu hadi mniambie ni wapi nitapata jibu la tume la kukiuka maagizo ya mahakama ya Afrika.
“Waandishi embu subirini kwanza mkurugenzi wa uchaguzi aje hapa ilia atoe ufafanuzi na nyie msikilize mkaandike ukweli kwa sababu hii siyo haki ni sawa na kudharau mahakama,” alisema.

Baada ya kuzozana na maofisa waliokuwa wakimkabidhi fomu hizo, walilazimika kumuita mkurugenzi wa uchaguzi Kailima Ramadhani, ambaye alimwambia kwamba sheria hairuhusu.


“Sisi tunafuata sheria mwenyekiti kama hicho kipengele kingekuwapo tungekuruhusu uchukue fomu hizo, lakini hapa tunabanwa na sheria tunaruhusu kutoa fomu kwa watu wanaotoka kwenye vyama vyao,” Ramadhani
Alisema ni vizuri Mtikila angefuatilia kwa makini suala hilo ili sheria ipitishwe kwani NEC wanachokifanya ni kufuata sheria zilizopo tu na si vinginevyo.

Baada ya kumaliza maongezi Mtikila aliamua kuweka sahihi na kuchukua fomu hizo kwa shingo upande huku akisema atakiwakilisha vyema chama chake hicho.

Juni 13,2013 Mtikila alishinda kesi aliyofungua AfCHPR, mjini Arusha akidai Tanzania inakiuka demokrasia inapozuia wagombea binafsi.

Mchungaji Mtikila, ambaye ana historia ndefu ya kukwaruzana na Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), alifungua shauri mahakama ya Afrika mwaka 2011 baada ya jitihada zake za kupindua mabadiliko ya kikatiba yaliyofuta ugombea binafsi kugonga mwamba kwenye mahakama za kitaifa.
Chanzo cha habari hii ni mwananchi
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top