Wakati Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Christopher Mtikila akigoma kusaini fomu za kugombea urais akitaka ufafanuzi wa mgombea binafsi, Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa amekwama kwenye lifti za jengo lililopo katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi (NEC) kutokana na kukatika umeme.
Mchungaji Mtikila ambaye aliambatana na
mgombea mwenza Juma Metu Juma, alitaka ufafanuzi wa kutokuruhusiwa
kuwania urais akiwa mgombea binafsi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
wakati Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) imeruhusu.
“Siondoki
hapa na wala sitaweza kuchukua hizi fomu hadi mniambie ni wapi nitapata
jibu la tume la kukiuka maagizo ya mahakama ya Afrika.
“Waandishi
embu subirini kwanza mkurugenzi wa uchaguzi aje hapa ilia atoe
ufafanuzi na nyie msikilize mkaandike ukweli kwa sababu hii siyo haki ni
sawa na kudharau mahakama,” alisema.
Baada ya kuzozana na maofisa waliokuwa
wakimkabidhi fomu hizo, walilazimika kumuita mkurugenzi wa uchaguzi
Kailima Ramadhani, ambaye alimwambia kwamba sheria hairuhusu.
“Sisi
tunafuata sheria mwenyekiti kama hicho kipengele kingekuwapo
tungekuruhusu uchukue fomu hizo, lakini hapa tunabanwa na sheria
tunaruhusu kutoa fomu kwa watu wanaotoka kwenye vyama vyao,” Ramadhani
Alisema ni vizuri Mtikila angefuatilia
kwa makini suala hilo ili sheria ipitishwe kwani NEC wanachokifanya ni
kufuata sheria zilizopo tu na si vinginevyo.
Baada ya kumaliza maongezi Mtikila
aliamua kuweka sahihi na kuchukua fomu hizo kwa shingo upande huku
akisema atakiwakilisha vyema chama chake hicho.
Juni 13,2013 Mtikila alishinda kesi
aliyofungua AfCHPR, mjini Arusha akidai Tanzania inakiuka demokrasia
inapozuia wagombea binafsi.
Mchungaji Mtikila, ambaye ana historia
ndefu ya kukwaruzana na Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), alifungua
shauri mahakama ya Afrika mwaka 2011 baada ya jitihada zake za kupindua
mabadiliko ya kikatiba yaliyofuta ugombea binafsi kugonga mwamba kwenye
mahakama za kitaifa.
Chanzo cha habari hii ni mwananchi
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies