Namshukuru Mungu nimerudisha fomu salama.....
Nawaomba wanaCCM waniunge mkono kwenye mchakato huu...
Kuanzia 22/7/2015 Tume ya Taifa ya Uchaguzi itafanya zoezi la kuboresha
Daftari la wapiga kura kwa mfumo wa BVR mkoani DSM. Natoa wito kwa
wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha.
Eid Mubarak..
Hili
ni ombi maalum kwa wananchi wa Ukonga toka kwa meya huyo mstaafu wa
manispaa ya Ilala Mhe.Jerry Silaa wakati akijiandaa kurudisha form hizo
za kuomba kuteuliwa kugombea ubunge kupitia CCM kwa jimbo la
UkongaZifuatazo ni picha Mbalimbali zilizopigwa na Mpiga Picha Fred
Chegge kwa niaba ya Jerry Silaa Foundation katika tukio hilo la
urudishaji form hizo lilolofanyika leo katika ofisi za CCM wilaya ya
Ilala.
Masama
Blog inamtakia kila la kheri katika Hatua hii ya kuomba ridhaa ya
kuwatumikia wananchi wa jimbo la ukonga kwani tunaamini ameonyesha uwezo
mkubwa wa uongozi katika kipindi alichoweza kuwa meya wa manispaa wa
ilala.