Magazeti ya Tanzania July 28 2015 na
headlines zake kubwakubwa yako mtaani, hapa ninazo chache kwenye zile
zilizobebwa leo na kuchambuliwa Redioni.
Edward Lowassa rasmi UKAWA, muda wowote kutangazwa mgombea Urais huku akipewa nafasi ya kujiunga na CHADEMA.
Serikali imekanusha taarifa iliyochapishwa na moja ya Magazeti kuwa Rais JK ni miongoni mwa Marais 5 wanaoongoza kwa kulipwa misharaha mikubwa Afrika.
Wabunge 2 wawili viti maalum CHADEMA wahama Chama hicho kwa madai kuwa hawana nia ya dhati ya kupambana na Ufisadi, yuko Chiku Abwao aliyehamia ACT Wazalendo na Leticia Nyerere aliyeamua kurudi CCM.
Prof. Jay aibuka mshindi CHADEMA kwenye kura za maoni katika jimbo la Mikumi, michango ya Kampeni za kujinadi kwenye majimbo mbalimbali CCM zawaliza wagombea baada ya baadhi ya wagombea hao kudai kuwa michango hiyo ni mikubwa