Tanzania imeanza kupata mafanikio kwenye
juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa malaria, ugonjwa ambao unatajwa
kusababisha vifo vingi.
Hayo yameelezwa Jumatano jijini Dare s
salaam na wataalamu wa masuala ya afya, wakati wa uzinduzi wa ripoti
maalumu juu ya hali ya ugonjwa wa malaria, tangu kuasisiwa kwa azimio la
Abuja la mwaka 2000 lililopitishwa na viongozi wa umoja wa Africa.
Wataalamu wa afya wanasema kwamba,
mafanikio zaidi yameanza kujitokeza kwa makundi ya kina mama wajawazito
na watoto waliochini ya umri wa miaka 5, ambao ndiyo wanachukua asilimia
kubwa ya kuugua ugonjwa huo na hatimaye kupoteza maisha.
Takwimu za hivi sasa zinaonyesha kuwa,
karibu watanzania milioni 11 wameugua ugonjwa huo, na jambo la
kusikitisha ni kwamba kila mwaka watu 38,000 hupoteza maisha kutokana na
malaria.
Katika nasaha zake wakati wa uzinduzi wa
ripoti hiyo, Makamu wa Rais Dr Ghalib Bilal alitaja shabaha ya serikali
katika siku za usoni kujenga kituo maalumu kitakachozalisha dawa za
kukabiliana na masalia ya mbu waenezao malaria.
Wakati kukitajwa kuanza kupatikana
mafanikio kwenye juhudi hizo za kukabili ugonjwa wa malaria, hata hivyo
nchini nyingi za kiafrika ambazo zinachukua asilimia 80 ya vifo vyote
vya malaria dunia, zinakabiliwa na tatizo la uhaba wa mafungu ya fedha.
Miradi mingi ya kiafya inashindwa kuendelezwa kutokana na uwekezaji
mdogo unaofanywa kwenye sekta hiyo ya afya.
Kwa kulitambua tatizo hilo, mwakilishi
wa shirika la afya ulimwenguni WHO, Dr Robert Chatola, ametoa mwito
akitaka kuwepo mafungamano ya pamoja na kuongeza uwekezaji kwenye sekta
hiyo ya afya.
Kwa kiwango kikubwa Zanzibar inasalia
eneo pekee katika ukanda wa afrika mashiriki kupata mafanikio makubwa ya
upunguzaji wa vifo vitokanavyo na malaria.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies