Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

BUNGE WA ZAMANI WA SHINYANGA MJINI AFARIKI DUNIA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Mwanasiasa mkongwe n aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CCM mwaka 1995 hadi 2005 Leonard Derefa  amefariki dunia  leo asubuhi kutokana na ugonjwa wa shinikizo la damu muda mfupi baada ya kutoka uwani kujisaidia.
Leonard Derefa( Mwanaderefa) alizaliwa mwaka 1942 katika kijiji cha Bulima wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza na hadi umauti unamfika alikuwa anaishi katika mtaa wa Mbuyuni kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga.
Mmoja wa watoto wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Newe Derefa amesema baba yake alifikwa na umauti leo asubuhi saa 12.30 muda mfupi baada ya kutoka uwani kujisaidia.
Newe amesema kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na mama yake, Thereza Derefa mara baada ya mumewe kutoka uwani aliingia chumbani na badala ya kurejea kitandani alipiga magoti pembezoni mwa kitandani na kuanza kusali huku akitoka jasho jingi mwilini kiasi cha kulowana na aliamua kumgusa na kumsemesha ili kujua kitu gani kilichokuwa kikimsumbua lakini hakujibu kitu.
"Tulimchukua na kumpeleka katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga, madaktari walimpima ili kuelewa tatizo lakini walibaini tayari  ameishafariki”,amesema Newe.

Jina la Leonard Derefa siyo geni katika ulimwengu wa siasa nchini Tanzania ambapo kwa wafuatiliaji wa masuala ya siasa, hasa tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, watamkumbuka mwanasiasa huyo mkongwe kutokana na lafudhi yake ya Kisukuma iliyomfanya wakati mwingine apate ugumu kutamka baadhi ya maneno.


Tangu Tanzania ipate uhuru, Jimbo la Shinyanga Mjini limeongozwa na wabunge tisa ambao ni John Rupia, Bakari Msonde, Anna Tito Kachima, Ntemi Nyanda, Haninghton Mfaume, Paul Makune, Leonard Derefa, Dk Charles Mlingwa na sasa Stephen Masele.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top