Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MABASI YATEKWA NA MAJAMBAZI NA WANAWAKE KUBAKWA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Stori  Mwandishi Wetu, Mwanza

Roho mkononi! Jumla ya magari saba yakiwemo mabasi mawili yaliyokuwa yakitokea jijini Dar es Salaam kuelekea Mwanza, yametekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi usiku wa kuamkia Jumamosi ya wiki iliyopita, saa 6:30 usiku eneo la Ng’ungumalwa mkoani Mwanza.

Polisi wakiwa eneo la tukio.
Miongoni mwa magari yaliyotekwa, mawili yalikuwa ni mabasi ya abiria, Super Najmnisa na Princess Mnaa huku mengine yakiwa ni malori na gari dogo moja ambapo inaelezwa kuwa watekaji walitegesha mawe makubwa barabarani kabla ya kutekeleza tukio hilo.
Wakizungumza na mwandishi wetu aliyekuwepo eneo la tukio, baadhi ya madereva wa magari yaliyotekwa walieleza kwamba walipofika eneo hilo, walikuta mawe yakiwa yametegeshwa barabarani huku kukiwa na kundi la watu wenye silaha za aina mbalimbali yakiwemo mapanga, marungu na bunduki.
Baadhi ya abiria waliotekwa.
“Walitushusha kwenye magari na kututaka tusalimishe kila kitu tulichokuwa nacho zikiwemo fedha na simu za mkononi. Waliokuwa wakionesha ukaidi walikuwa wakipigwa na kujeruhiwa vibaya,” alisema dereva mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Madereva hao waliendelea kueleza kuwa kazi hiyo ya utekaji iliendelea kwa takribani saa nzima ambapo kila gari lililokuwa likija eneo hilo, lilikuwa likitekwa na watu kulazimishwa kushuka chini na kutoa kila walichokuwa nacho.
Msichana huyu alizimia baada ya kutekwa.
“Walikuwa na mifuko mikubwa miwili, mmoja ulijaa simu walizotupora na mwingine ulijaa fedha, kwa kweli lilikuwa ni tukio baya sana, wengi walijeruhiwa vibaya,” alisema dereva mwingine ambaye naye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.
Abiria wengine waliozungumza na Uwazi, walienda mbele zaidi kwa kueleza kuwa mbali na kupigwa na kuporwa, pia baadhi ya abiria wanawake walibakwa na kusababishiwa maumivu makali.
“Huu unyama tuliyofanyiwa wa kupigwa na kuporwa mali zetu huku baadhi yetu wakibakwa unatisha sana na unaonesha ni kwa jinsi gani nchi inaelekea kubaya, hakuna amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya,” alisema mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa waliotekwa, aliyejitambulisha kwa jina moja la Sara.
Abiria wakiwa wameduwaa
Abiria hao waliliambia Uwazi kwamba eneo hilo lina pori kubwa ambapo panahitajika doria za mara kwa mara za polisi kwani ni eneo ambalo limekuwa maficho ya majambazi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola alipopigiwa simu na kuulizwa juu ya tukio hilo, alikiri kuwa na taarifa na kueleza kuwa polisi walifika katika eneo la tukio muda mfupi baadaye baada ya kupata taarifa na kufungua barabara iliyokuwa imefungwa na kuruhusu magari kupita.“Msako mkali unaendelea kuwatafuta watuhumiwa katika Wilaya ya Kishapu na Kwimba,” alisema Kamanda Mlowola.


Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.

    
In order you follow me just click one of the Icon Button above.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top